Media Manipulation by CCM!

Revolutionary

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
456
86
Part 1
Media manipulation ni njia mojawapo inayotumika katika Public Relations ambapo wanasiasa wamekuwa wakitengeneza picha au mantiki ambazo zinazolinda maslahi yao na vyama vyao.

Mbinu hizi zinahusisha matumizi ya upotofu/upotoshaji unaoleta maana (logic fallacies) na mbinu za propaganda, na mara nyingi hutumia kuzima habari zenye mguso wa uma zilizoenea kuhusu suala fulani (current public interest issues) na kuziondosha kabisa katika masikio ya tafakari za watu kwa kushawishi watu waweze kupuuzia mantiki ya habari hizo au tu kwa kuelekeza kwengine shauku ya watu katika masuala fulani yanayowagusa (diverting public attention elsewhere).

Kimsingi mbinu za kileo za Media Manipulation ni njia za kuwazugia watu zinazotumika kudivert attention yao kwa dhana kwamba umma una shauku yenye kikomo (the public has a limited attention span.)

Kumekua na mbinu na njia nyingi ambazo zimeuwa zikitumiwa na viongozi wa chama tawala akiwemo Mh Rais kumanipulate media kwa nyakati tofauti ili kulinda maslahi ya chama hicho.
Zifuatazo ni baadhi ya mbinu chache zinazotumiwa na chama tawala kumanipulate media na usambazaji habari zinazowafikia raia nchini.

1. Appeals to consensus
Vyanzo vunasema;
“By appealing to a real or fictional "consensus" the media manipulator attempts to create the perception that his opinion is the only opinion, so that alternative ideas are dismissed from public consideration.
kwa kutumia consesus kulazimisha na tengeneza mapokeo kwamba mtazamo na kinachosemwa na chama hiki ndicho kiko sahihi , na mitazamo mbadala (mfano wa kama ile inayotolewa na Chadema na wanaharakati) inapingana na matakwa ya umma.

Hii ni njia inayotumika kukwepa mijadala (debates) kwa kudai kwamba mambo yako sawa wakati sio uhalisia wa mambo.

Michael Crichton insists: Let's be clear: the work of science has nothing whatever to do with consensus.
Consensus is the business of politics. Science, on the contrary, requires only one investigator who happens to be right, which means that he or she has results that are verifiable by reference to the real world. In science consensus is irrelevant. What is relevant is reproducible results. The greatest scientists in history are great precisely because they broke with the consensus.


2. Fear mongering (kueneza uogofya) ni namna ya kutumia fear (uwezekano wa kutokea hatari au mambo mabaya) kushawishi mapokeo, mawazo, mitazamo na matendo ya watu ili yaegemee upande fulani.


Mfano ni namna viongozi wa CCM wakiongozwa na mwenyekiti wao, mh Rais wanaovyotumia dhana hii kuogopesha raia kuhusu maandamano ya Chadema na suala la udini.
Hapa kile kihachoogopwa (The feared object or subject) mara nyingi huwa kinakuzwa na katika mwendelezo wa kudia rudia katika vyombo vya habari mbalimbali (radio, luninga, gazeti n.k.) ili kuweza kuimarisha dhamira ya mbinu hii kuwaogopesha raia na kushawishi tuamini mitazamo yao kisiasa.


Mbinu hizi za siasa dhaifu na zinazoweza kuwa dhamira chafu zimekuwa zikitumika pia katika uchaguzi na matukio mengine. Hapa mtumiaji wa mbinu hii hueneza dhana kwamba kama kitu fulani kitafanyika au kisipofanyika madhara makubwa (disastrous event) yatatokea na husisitiza kwamba kwa kumpigia au kutompigia kura (kumchagua) mtumiaji wa mbinu hii basi madhara hayo yanaweza kuepusha.


Ni wazi tunakumbuka katika uchaguzi CCM wakiongozwa na Mh Rais wamekuwa wakiwashawishi kuwa Chadema wanaendeza suala hatari la udini na hivyo wasiwachague kwa kuwa wataitumbukiza nchi katika hatari kubwa. Viongozi hao wa CCM wamekuwa wakieneza haya bila kuwa na mifano halisi kudhihirisha kwamba hii ilikuwa tu ni mbinu tu kisiasa kuwatisha watu ili raia waichague CCM kuepukana na hayo.


Hatima yake ni kwamba wapiga kura wataingiwa woga na kuogopa na kuwashabikia na kuwapigia kura wale wagombea wanaofaa. Hii ilidhihirika wazi siasa chafu zilizokuwa akifanyiwa Dr Slaa katika uchaguzi.


Mbinu hii ni hufanikiwa kushawishi raia/watu wenye mitazamo myepesi myepesi, wasiokuwa na uelewa wauhalisia wa mambo kwa kuwa wao huamini kwa kwamba kwakwa kuwa viongozi wanasema hivyo basi watakuwa sahihi na kweli na wao huamini hivyo haswa katika nchi hii iliyo na elimu ndogo ya uraia kiasi kwambaraia wengi hawajui hata katiba ina rangi gani


Hatari ya mbinu hii chafu ni kwamba inaweza kutengeneza kitu kinachoitwa “A SELF FULFILING PROPHECY”. Ambapo tunaweza kufanikikisha kutokea kwa jambo Fulani kwa kujibashiria wenyewe. Yaani yaweza kuwa suala la udini halipo na kutokana na sisi wenyewe kuanzisha mjadala huu wa kiutechonganishi basi akili na matendo yetu yakaanza kuelekea kule ambako jambo hili litaukuja kuwa tatizo kweli, tafakari!


Elimu ya uraia inahitajika sana kuwafanya raia wawe na uelewa mkubwa siasa za nchi na uhalisia wa mambo ili kuwafanya raia wawe na fikra HURU haswa tunapoelekea katika kuadhimisha miaka 50 ya UHURU Disemba 9 mwaka huu. Napongeza jitihada binafsi za Chadema na viongozi wake katika kuelimisha raia kitu ambacho ni muhimu kwa nchi yoyote yenye demokrasia ya kweli kinyume na inavyoitwa na CCM na viongozi wake kuwa ni kueneza uchochezi na chuki dhidi ya serikali.


Baadhi ya mifano ya mbinu hizi chafu zilizotumiwa na viongozi duniani
"If we don't approve the McCarran Internal Security Act the Soviets will take over America."
"We cannot wait for the final proof – the smoking gun – that could come in the form of a mushroom cloud." (US President George W. Bush, making the case for declaring war on Iraq)
3. Distraction by nationalism (Demonisation of the opposition)

Hii ni njia inayotumika kuwashawishi raia kwa kigezo au kisingizio cha utaifa. Wanaopinga chama tawala wanafanywa kuonekana kama watenganishi au wenye chuki na hivyo kuwataka watu wawakatae na kuwapuuza.
Njia hii imekuwa ikitumika kuzima ushawishi wa mitazamo mbadala ya vyama pinzani kama ilivyo katika McCarthyism ambapo yeyote asieafikiana na serikali anafanywa aonekane kuwa ni mtenganishi yaani “Anti Tanzanian” au mdini, au mbinafsi au kumuita jina lolote chafu kama mmoja wa kiongozi wa CCM aliyefananisha Dr. Slaa na Savimbi, muasi wa Namibia.
Mifano ya mbinu hii iliyotumika sehemu nyingine duniani;
- "Your idea sounds similar to what they are proposing in Turkey. Are you saying the Turks have a better country than us?"


- "The only criticisms of this proposed treaty come from the United States. But we all know that Americans are arrogant and uneducated, so their complaints are irrelevant."
- The "Support Our Troops" campaign created by the Republican party (USA) during the War on Terror implies that opposing the war effort detracts support away from the individual soldiers fighting the war. Thus patriotic support of the troops becomes a form of support for the war in general.


Pamoja na mbinu hizi CCM kimekuwa kikitumia “Spin Doctors” ambao hutumika kuleta danganya toto (distract or divert public attention) na kufanya watu wazugike na jambo fulani ili kusahau matukio muhimu. Mfano mzuri wa Spin Doctors wa CCM ni Mh Chenge katika uchaguzi wa Spika wa bunge na namna alivyotumika kudistract watu kufanikisha fitna iliyomuondoa Mh Samuel Sitta katika kinyanganyiro hicho. Wako wengine wengi kama Mh Pinda, Abdulrahman Kinana, Makamba, Mh Anne Makinda na wengine wengi wanaotumika kuzima masuala muhimu yasiendelee kuzungumzwa katika jamii


Nitawaongelea zaidi Spin Doctors wa CCM katika makala zijazo.


Part 2
Ni wazi kuwa chama tawala kimefanya mengi mazuri ya kupongezwa lakini kimsingi mazuri hayo hayabatilishi mabaya ya kunuka yafanywayo na na chama hiki pia hasa kwa kutumia mianya inayoletwa na katiba iliyoundwa na chama hicho.

Katiba hii inatumika kama kiboko cha kuadhibu, kunyamazisha wale wanaopingana na serikali ya chama tawala ili kulinda maslahi ya chama hicho kama inavyoonekana wazi sasa hadi kupelekea malalamiko mengi kuhusu mapungufu makubwa katika katiba hii kiasi cha CCM wenyewe kukiri kuwa katiba mpya ni suala la lazima ingawa haikuwa katika ajenda yao ya uchaguzi.

Ni wazi ili tuweze kuwa na uwanja wa haki katika maneno na matendo yetu tunahitaji katiba mpya kwanza ambayo pia nina mashaka na mfumo utakaotumika kuiunda kutokana na ubinafsi wa viongozi wa chama tawala na vipengele dhaifu vya katiba ya sasa vinayoweza kuleta katiba mpya itakayokuwa na matakwa ya wengi. Baada ya kuwa na muongozo mpya (katiba mpya) ndipo tutaweza kuongea kama wamoja na kusema hiki ni sahihi hiki si sahihi tofauti na sasa.

Chama tawala kimekuwa kikitumia njia mbalimbali ambazo zimeoteshwa mizizi na katiba hii dhaifu iliyompa raisi na chama tawala nguvu kubwa kuendesha vyombo mbalimbali vya utawala kama vyombo vya kusimamia haki, taasisi za kiusalama na kuzuia rushwa, vyombo vya kusimamia uchaguzi na demokrasi n.k.

Ni wazi kuwa wa vyombo hivi hauko HURU kiutendaji kutokana na mwingiliano wa maslahi na chama tawala kwa kuwa rais ndiye wa chama tawala ndiye anayeteua na kusimamia utendaji wake. Na kwa demokrasia yetu changa si rahisi kwa vyombo hivi kutetea maslahi kusimamia haki sawa na kutuhudumia bika upendeleo.

Niulize, Je ni raisi gani duniani atakayeteua wasimamizi wa idara za serikali wasiokuwa na mlengo wa kutetea maslahi yake na ya chama chake? Ambao inapobidi watatetea bila kujali maslahi ya chama pinzani na ya raia wasioshabikia siasa za raisi huyo na chama chake?, tusijidanganye!
Vyombo vya habari ndivyo vimekuwa vukitumika kueneza propaganda mbalimbali kwa uharaka na uzio mkubwa kieneo. Kama iliyo katika katiba, vyombo vya habari vinapotumika kwa maslahi ya kugemea upande fulani huweza kuleta kubwa kwa ubinafsi kulinda maslahi na upotofu wa wachache.

Ni wazi changamoto kubwa tuliyonayo haswa tunapojiandaa kuadhimisha miaka 50 ya UHURU wa taifa letu ni kukosekana kwa UHURU wa kweli katika mifumo inayotumika kuendesha nchi, mifumo ya kusimamia haki, demokrasia, uchumi, uwajibikaji, elimu, na HABARI (kwa uchache). Hili linasimamiwa na katiba isiyo kuwa na maadili yanayolinda UHURU wa raia kulinda maslahi yao na kutoa maoni yao ikiwemo UHURU wa vyombo vya habari (husisha kesi ya vitisho vya serikali kwa gazeti laMwananchi). Hili limeendelea kudhihirika kupitia kilio kikubwa cha watanzania kutaka mabadiliko ya kikatiba.

Ni kweli kuna mengi lakini leo tuzingimzie namna ambavyo CCM imekuwa ikitumia media kueneza na kulinda maslahi yake kwa namna inayoonekana ni ya kutawaliwa na dhana (theme) dhaifu ya vitisho na kuogofya (fear).
 
Ukweli uliyoje! Lakini hizo njia huchelewesha mageuzi ya kweli tu.... haziyazuii na consequnses zake ni mbaya saaaaaana yapotokea.
 
Macho ni kweli hizi njia huchelewesha mageuzi ndio maana elimu ya uraia ya kuelezana na kuwekana wazi hata kama itaitwa ni ya uchochezi inahitajika sana! Raia wakisha jua nini kinaendelea wataweza kufanya maamuzi sahihi tu!
 
This 2011. Wanachokifanya ni kijipotezea muda kwani babu na bibi yangu peke yao ndio walionyuma miaka hii. Waliwaonea mababu na mabibi zetu kwa kutumia "fear and waliwa-feed wrong information" Ni ukweli propagandas za ccm zipo na zinaendela kila mahali hasa ndani ya vyombo vya serikali ambavyo vilitakiwa kufanya kazi kusema ukweli na kutetea nchi yao, sababu moja tu - wanalipwa na kodi za wananchi. The problem ya tbc na magazeti kama dairy news ni kwamba Katiba ya Tanzania ndio inawakandamiza, wote walioajiliwa ndani ya vyombo vya habari vya serikali lazima waonekane wapo na wana-support ccm. Mkurugenzi wa shirika la habari la Tanzania anateuliwa na Kikwete, what do we expect? Hakuna freeodom ya wafanyakazi wa vyombo hivi, wakifukuzwa kazi baada ya kukataa au kutoripoti au kutoonyesha picha ya Kikwete amekaa kama vile anafanya kazi, si watafukuzwa. Hakuna opportunities za kutafuta kazi katika private sectors za waandishi wa habari na hii inachangiwa na philosophy ya ccm na Kikwete kuongoza Tanzania. Nia ya ccm ni kuhakikisha serikali inabaki inanguvu kupita instututions zozote zile Tanzania. Hili jambo la media na propagandas za ccm tuendelea kulisikia na tunashahuri Chadema na wao waunde powerful media to counter ccm propagandas.
 
Great thinking by you Niweze, Ni kazi kwetu wananchi kuyajua haya hasa kabla hata ya kuandika katiba mpya ambayo nayo kwa kupitia mwongozo wa katiba ya sasa mpya haiwezi kumaliza kero.

Uzuri ki kwamba kizazi kipya kinajua nini kinaendelea. Uzuri zaidi si vijana tu hata kina mama nao wamechoka ushuhuda ninao, kabla ya uchaguzi wengi walimpenda Kikwete ingawa ukiwauliza wanashindwa kusema wanampendea nini , leo wao wenyewe wakiona anaongea kwenye TV wako radhi hata waizime anavyowaboa.

Elimu ya Uraia inahitajika saaaana! Each one Teach one!

Chadema wana Kazi ya kuwa na umakini na kuweza kubuni counter CCM propagandas, very true!
 
Back
Top Bottom