Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
- Idadi ya raia waliouawa kwenye mikono ya vyombo vya dola kati ya utawala wa Mkapa na Kikwete inazidi kwa mbali sana idadi ya waliouawa na vyombo vya dola kwa zaidi ya miongo miwili ya utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
- Kiasi hicho pia kinazidi sana kile cha wale ambao hukumu ya kifo dhidi yao imetekelezwa.
- Idadi ya watu waliotekelezewa hukumu ya kifo chini ya utawala wa Kikwete inazidi pia wale waliotekelezewa wakati wa utawala wote wa Nyerere.
- Idadi ya watu waliohamishwa katika makazi yao kupisha wawekezaji wakubwa wa kimataifa chini ya utawala wa Kikwete na Mkapa inazidi sana watu waliohamishwa kwa ajili ya kujenga vijiji vya ujamaa (siyo kupisha wawekezaji).
- Waandishi wa habari ambao wamejikuta matatani mahakamani na hata kupoteza maisha idadi yao ni wengi zaidi wakati wa Mkapa na Kikwete kuliko wakati wa Nyerere.
- Mahasimu wengi wa serikali ya Nyerere wameishi na kuzeeka wakiishi wakiwa huru; wengi makubwa yaliyowapata ni ama kwenda uhamishoni au kuhamishwa na kutupwa maeneo ya pembezoni. Yanayowakuta sasa hivi wapinzani wa Kikwete na yaliyowakuta wapinzani wa Mkapa....
Lakini ni Nyerere ambaye anatajwa kuwa ni dikteta na kuwa alikuwa anakandamiza haki za wananchi. Inawezekana