Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Igunga kuna Uarabuni, Dodoma kuna Uhindini, Tanzania nzima ni uswahilini.
Tanzania na Mtanzania ni nani?
Unafahamu chanzo cha hayo majina ya uhindini na uarabuni huko Igunga na Dodoma?
Igunga kuna Uarabuni, Dodoma kuna Uhindini, Tanzania nzima ni uswahilini.
Tanzania na Mtanzania ni nani?
Mwalimu sihitaji kufanya ligi na wewe, tuendelee na mengine kwani naona kama una nia ya kuharibu mjadala huu, inawezekana hujaupenda.
Tunapopiga kelele kila siku hapa jf wachaga, wachaga, wachaga, wachaga mbona sijawahi kukuona ukisema huo ni ubaguzi?? Mkuu una maslahi na makundi tajwa??
Hapan usipindishe maneno, hakuanzisha kuwazungumzia wahindi na waarabu, soma vizuri post yake: 'watanzania waarab au "watanzania wahindi".
Sasa hao Watanzania Waarab au wahindi" unawa define vipi? rangi? nywele? lugha? nationality mbili?
Unaonesha hukijui unachokiuliza. By waarabu unamaanisha kina nani? Kwa lugha, kwa rangi? maana Uarabu si Utaifa.
Utakuwaje Mtanzania halafu uwe Mwaarabu? huo Uarabu ni nini na Utanzania ni nini? ikiwa unaongelea racial minorities, kwanini tusianze na Wahutu na Watutsi waliopo Tanzania?
hahahaha kazi ipo hapaTena si ndogo!
Said Arfi ni Mtanzania Muarabu?
Salim Ahmeid Salim ni Mtanzania Muarabu?
Mohammed Dewji ni Mtanzania Mhindi?
Said Bakhressa ni Mtanzani Muarabu?
Rostam Aziz ni Mtanzania Mhindi? Mtanzania Muarabu? Mtanzania Muajemi?
Watoto wa hao waliotajwa nao wataendelea kuwa ni Watanzania Waarabu na Watanzania Wahindi? Hadi lini? Na weusi wa rangi zao unahusikaje?
Tungekuwa tunazungumzia Wahindi na Waarabu wala hakuna shida katika hilo, wanajuulikana ni watu gani na wana patikana wapi duniani.
Tunachozungumzia hapa ni Watanzania Wahindi na Watanzania Waarabu.
Hapo ndipo tunaposhindwa kuwajua watu hawa ni nani? Na rangi yao kama si nyeusi ni rangi gani?
* Mwanakijiji yeye kawaita "Waarab" ambalo hata si neno sahihi kwa Kiswahili
wao wenyewe wanatubagua, ma binti zao hawataki kuolewa na ngozi nyeusi hasa wa indi ndo usiseme. Utakuta binti atakuta binti yupo tayari kuolewa hila wazazi hawataki kabisa, wannasema eti " watachafua mbegu".
haya mambo mengine ni sifa za mtu tu, wapo kina profesa shivdi UDSM na wengine wengi wapo serekalini. Wakijitokeza kugombea katika nafasi mbalimbali mimi naamini watachaguliwa, au wanaweza kuteuliwa kutokana na jinsi wanavyo jituma. chakusikitisha zaidi wao wenyewe wanatutenge na kuunda kundi lao la watu wa Asia.
Hapo nilitaja wahindi na waarabu moja kwa moja kwa sababu nilikuwa namjibu ribosome katika hoja yake ya wahutu na watutsi.
Kama MMKJJ amekosea kuwaita waarab, inaweza kuwa kweli lakini hiyo haibadilishi content ya kinachozungumzwa hapa.
Hakuna cha kupinda hapo, nilikuwa natoa ufafanuzi wa hoja yako uliyokuwa umeizua kutaka na wengine nao wajadiliwe, nadhani unaona mwenyewe ulichoandika hapo chini.
Hata wamasai hawataki binti zao waolewe na wabantu (wafupi, wana pua pana) watachafuwa mbegu. Au hujui hilo?
Kwako wewe Mtanzania Mhindi au Mtanzania Muarabu ni yupi?
Kwa wengine hii kukaa tu ukamwita mtu kwa kuongezea suffix mbele ya uraia wake ni sifa moja wapo ya ubaguzi na kuwabagua
Mbona hatukai hata siku moja tukaanza kutaja Watanzania Wachaga wala Watanzania Wasukuma?
Kama hujaelewa mtanzania muarabu na mtanzania mhindi basi nenda chit chat kuna mada za wewe kuchangia......Sasa unataka kunipangia cha kufanya?
Nauliza tena Mtanzania Muarabu na Mtanzania Mhindi ni nani?
Ahsante
Robisome siyo kweli, jokes aside, nafahamu watu wengi sana ambao mama ni mmasai lakini baba ni mmbantu, mimi mwenyewe mmojawapo.
Kama hujaelewa mtanzania muarabu na mtanzania mhindi basi nenda chit chat kuna mada za wewe kuchangia......
Watanzania Waarabu, hebu wa define pachanga za nini? halafu hata hilo jina lako linaonesha na wewe una asili ya nje ya Tanzania, sijui tukuiteje? Mtanzania Mtutsi? au Mtanzania Mwaarabu?
watanzania wenye asili ya ashia.....otherwise uwe unataka ligi na nipo tayariWewe uliyeelewa tujulishe!
mkuu! mama yake Kinje siyo muhindi! ni chotara wa Kigiriki na Mhaya Mweusi toka Kamachumu huko Kagera.Na mimi nafahamu wengi sana ambao mama ni muhindi baba ni mbantu. Mmoja wapo ni maarufu sana, kwa jina Kinje Kingunge Ngombale Mwiru. Na pia nawafahamu wengi zaidi ambao ni wa asili za Oman, Yemen lakini mama au baba zao ni wabantu au wamasai au wanyamwezi au wanyalukolo.
Wapo na si odd ni very common Tanzania. Said Arfi? Zakia Meghji? Shamim Khan? Zahra Nuru? Dokta Slaa?