Mdahalo: Ndugai vs Lissu - Jumamosi Julai 30

Status
Not open for further replies.

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
TAASISI ya Vox Media Centre Tanzania na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI) kwa ushirikiano na kituo cha Star TV kesho wataendesha mdahalo wa kibunge, mada ni ‘Bunge la 10 na Tanzania tunayoitaka’. Taarifa kwa vyombo vya habari iliyopatikana Dar es Salaam jana kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Vox Media, Ansbert Ngurumo, inaeleza kuwa mdahalo huo utafanyika kwenye ukumbi wa Mtakatifu Gaspar mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa Ngurumo katika taarifa hiyo, wazungumzaji wakuu kwenye mdahalo huo ni Naibu Spika Job Ndugai na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Tundu Lissu, huku wananchi 200 wakipata nafasi ya kuwauliza maswali; mdahalo huo utarushwa hewani kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 1:50 usiku. Inaelezwa kwenye taarifa hiyo kuwa ni fursa nyingine kwa wananchi kujadili masuala nyeti yanayohusu uhai wa taifa kwa kumulika, kuhoji na kutafakari namna Bunge linavyowawakilisha.

“Ni fursa yetu kupima utendaji wa wabunge na kuhoji kama wanakoelekea ndiko tunakopaswa…ni fursa pia kwa wazungumzaji wetu kusisitiza yanayopaswa na kukosoa yanayopotoshwa au kukosewa kuhusu Bunge, ni fursa kwa wabunge kujipima kwa maoni ya wananchi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Katika mdahalo huo Mkurugenzi Mtendaji wa EABMTI, Rosemary Mwakitwange, ataongoza mdahalo huo kwa kushirikiana na wajumbe wengine wa taasisi hizo. Mwaka jana taasisi hizo ziliaandaa midahalo kadhaa wakati wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu iliyohusu wagombea urais wa Tanzania.

Tanzania Daima
 
Hakuna jipya kwani Tundu Lissu hawezi kufananishwa na Ndugai kwa lolote labda umri tu. Ndugai kilaza na kuthibitisha hilo mliona jana alivowatoa kafara wapigania haki za wananchi!
 
Hapo ni kazi si utani .Ndugu gani ? Maana si Ndiugani.Jamaa ni mtupu na sina hakika kama atakubali mh
 
Waiting for this moment to come and see degrees of arguments and issues presentation , ila am sensing power blackout hiyo kesho ikifika!


OPTION,mdahalo urushwe kwnye redio pia,kwani endapo umeme utakatwa itakuwa easy kusikiliza mdahalo kupitia simu.
 
Mama Mary, tafadhali uendeshe mdahalo huu vizuri, isiwe kama ule wa Freeman Mbowe na Hamad Rashid. Ulianza vizuri baadaye ukashindwa kuongoza kisa vimaneno na kulalamikalalamika kwa wana-CUF.
 
Eshacky,

Acha kujifanya Nabii na Mtume,
Unataka kuniambia kwamba ukiwa umelala ukajiwa ktk maono ukaona mtu kama vile Naibu Spika akiukimbia huo Mdaharo kwa kivuli cha kupata udhuru au sijakuelewa vizuri? ha, ha, haaaaaaaaa. asikimbie mtu hapoooooo, TANESCO msiokoe aibu kwa kutuzimia umeme muda huo ukitimu.


Asikimbie mtu, maana hapo hakuna kuruka aya!
 
Lissu amtolee uvivu huyu Naibu Spika na amuulize kama macho yake yana uwezo wa kuuona upande mmoja tu yaani upande wa CHADEMA & NCCR- Mageuzi.
 
kwa sheria za bunge Tundu ataumbuka, hazijui, ama sheria za nje ya bunge Tundu anazifahamu sema tatizo lake hajui kujenga hoja kwa lugha ya kawaida huwa anajenga hoja kwa lugha ya jaziba sana. kitu ambacho mimi siamini kama mtu kujenga hoja mpaka utumie jaziba
 
i cant wait to see this battle. najua utakuwa mdahalo wa upande mmoja sababu Ngugai yupo empty kumpambanisha na Lissu. by the way hawa jamaa si walikataa midahalo kwenye uchaguzi watakubali kweli kuja?
 
TAASISI ya Vox Media Centre Tanzania na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI) kwa ushirikiano na kituo cha Star TV kesho wataendesha mdahalo wa kibunge, mada ni ‘Bunge la 10 na Tanzania tunayoitaka'. Taarifa kwa vyombo vya habari iliyopatikana Dar es Salaam jana kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Vox Media, Ansbert Ngurumo, inaeleza kuwa mdahalo huo utafanyika kwenye ukumbi wa Mtakatifu Gaspar mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa Ngurumo katika taarifa hiyo, wazungumzaji wakuu kwenye mdahalo huo ni Naibu Spika Job Ndugai na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Tundu Lissu, huku wananchi 200 wakipata nafasi ya kuwauliza maswali; mdahalo huo utarushwa hewani kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 1:50 usiku. Inaelezwa kwenye taarifa hiyo kuwa ni fursa nyingine kwa wananchi kujadili masuala nyeti yanayohusu uhai wa taifa kwa kumulika, kuhoji na kutafakari namna Bunge linavyowawakilisha.

"Ni fursa yetu kupima utendaji wa wabunge na kuhoji kama wanakoelekea ndiko tunakopaswa…ni fursa pia kwa wazungumzaji wetu kusisitiza yanayopaswa na kukosoa yanayopotoshwa au kukosewa kuhusu Bunge, ni fursa kwa wabunge kujipima kwa maoni ya wananchi," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Katika mdahalo huo Mkurugenzi Mtendaji wa EABMTI, Rosemary Mwakitwange, ataongoza mdahalo huo kwa kushirikiana na wajumbe wengine wa taasisi hizo. Mwaka jana taasisi hizo ziliaandaa midahalo kadhaa wakati wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu iliyohusu wagombea urais wa Tanzania.

Tanzania Daima
huyu mama wakati mwingine huharibu mdahalao this tym awe fair, ukikumbuka ule mdahalo wa mbowe na hamad rashid unatilia shaka huu kama atauendesha vyema. KIKUBWA TANESCO TU WASICHEZE RAFU HAPA.
 
Wakuu, huo muda mbona mimi nauona ni mfupi sana! Yaani kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 1:50 usiku! Sidhani kama saa 1 na dk 50 zitatosha kujadili mambo ya msingi kabisa na pia hao watu 200 watakaokuwepo ukumbini kupata nafasi ya kuwasilisha michango yao. Nina mashaka ya muda kuisha wakati mdahalo ndo kwanza unaanza.
 
aahhhh .... wataleta wale vitoto vidogo kwenda kujaza nafasi ..... ndugai hana charisma ya uongozi kama wa uspika
 
Nashukuru Mungu CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO(CHADEMA) Tumepewa fursa nyingine kuonyesha uwezo wetu wa kuwatetea watanzania pia ni nafasi nyingine adimu ya kuuanika usanii wa chama cha magamba(ccm) hadharan, Pls wanaJF tusikosee hiiii! Jobless Ndugugani baada ya Mbowe kukushika na kukuaibisha juu ya tafsiri ya kambi rasmi ya upinzani bungeni,unashikwa pabaya tena kesho na Tundu Lissu . . . . . ,
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom