Elections 2010 Mdahalo mwingine kabla ya siku kupiga kura kwa dr slaa - muhimu sana!

Not_Yet_Uhuru

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,304
431
Mpendwa sana dada Rose, na Team yako yote (Mh Ulimwengu, na Tanzania Foundation for Civil Society) iliyoandaa kazi ambayo ni exceptional Tanzania, yaani Debate ya jana Usiku kwa Dr Slaa (mgombea wa Chadema na Rais wetu Mtarajiwa). Nyie ndio icons na Materials ambayo taifa bora na makini linawatafuta na litawaenzi katika historia ya Taifa na katika mioyo ya watanzania wote. Kumbuka Uchaguzi wa Marekani na role ya Debate kwa wapiga kura wote hasa wale ambao ni undecided (ambao hawajaamua bado).

NYIE NI WATU MAKINI SANA TUNAWAHITAJI, NA TAIFA LETU LIMEPATA HISTORIA MPYA YA WATU WABUNIFU NA MAKINI WASIOBURUZWA NA MAFISADI AU WA WATAWALA MAFIDHULI kama hawa waliokuwa madarakani kwa sasa, wanaogopa kila kukicha, wana-distract attention ya watanzania kwa propaganda za uzushi, kesi za kupanga na uchochezi usioisha. Wanaogopa, wanaoelekea kushindwa vibaya.

HAKIKA, JK na CCM wajiandae tu kukabidhi Madaraka kwa Rais Mpya, Rais Makini - kama Rais John Kufour wa Ghana alivyofanya kwa ustaarabu mkubwa kukabidhi kwa John Atta Mills! Dunia inamuenzi Kifour na anaheshimika kimataifa popote aendapo. Sio mbinu chafu na ufidhuli wa mafisadi kama wanavyoichezea chi yetu hapa. Kikwete akijiandaa kukabidhi kwa amani na utulivu uongozi wa nchi atawekwa ktika historia ya taifa, na kuenziwa na vizazi, asiogope wanaomsukuma na kumpa matarajio yasiyofikiwa. Akumbuke itakayokwenda ICC (Mahakama ya Kimataifa), kama CCM na JK watakwama kukubali matakwa ya watanzania, au njama na uharibifu, itaanza na JK mwenyewe, na kufuatia wanaomsukuma. Itakuwa aibu sana na historia itawaweka katika giza nene lisilokwisha.

Wapendwa sana dada Rose, na Team yako yote (Mh Ulimwengu, na Tanzania Foundation for Civil Society), Tunakuombe upange MDAHALO MWINGINE wa mwisho ijumaa usiku AMBAO UTAKUWA 'FUNIKA YA YOTE' kwa Faida ya Taifa nzima na pia kwa ajili ya wale walionyimwa haki kwa kukatiwa umeme na Tanesco jana usiku ili wasitazame TV kumwona mkombozi wao. Tanesco ni chombo cha CCM, na Taifa ni zaidi ya kikundi cha Waoga hawa. Tanzania ni immortal (haifi milele) ila hawa wote watakufa na historia itawasahau mara moja! (Kitendo cha Tanesco kinatukumbusha tukio la TBC1 kukata matangazo makusudi, siku ya ufunguzi wa kampeni -Jangwani).

Tunaomba MDAHALO MWINGINE KABLA YA SIKU KUPIGA KURA, ili Rais mtarajiwa afunge kitabu cha historia ya ukombozi na kila mtanzania ampe kura ya NDIYO hapo 31 Oct. Ndiyo fursa pekee ya kufa au kupona kwa taifa letu.

ITV, Mwakitwange, Ulimwengu na waandaaji wote, hongereni sana. Tunao Watanzania mamilioni ambao bado hawajaamua (undecided), na Mdahalo wa Mwisho ndio Pigo la Mwisho kufunika ukurasa wa mwisho wa kitabu cha Historia ya Tanzania.

Tupeni tena raha Ijumaa usiku tafadhali. Kama sio kupitia ITV, basi hata chanel nyingine kama STAR TV, Tumaini au hata Mlimani TV.

YOTE YANAWEZEKANA, KWA MASKAHI NA MUSTAKABALI WA TAIFA LETU! CHONDE-CHONDE!

MUNGU IBARIKI TANZANIA, TUJALIE RAIS BORA NA MAKINI, LINDA AMANI, UTULIVU NA MAFANIKIO YETU.

Nawasilisha!
 
Huu sasa ni uhuni, sasa hii ni Breaking News au hatujui matumizi yake?
 
Correct me if am wrong.. hivi Dr. wa ukweli alishafanya mdahalo wowote mpaka mtoa mada akasema kama ufanyike mwengine? Unless kama alikusudia kusema waandae mazungumzo mengine ya ana kwa ana na wapiga kura wake.!
 
Back
Top Bottom