MDAHALO: M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?

Change always starts with someone or lather somethig! Unajua system change inakuwaje? Inaanza na ideal!
 
Huwa unanifurahisha kwa maoni yako lakini maoni yako mara nyingi sana lazima kuwe na statement inayotoa picha harisi ya namna unavyoichukia chadema. Hivi kwanini usiyaangalie yale magwanda ya Chadema kwa mtazamo wa kwamba chadema wameshona sare zao kwa kitambaa kigumu kwasababu hawana uwezo kama CCM hivyo wanataka zidumu zaidi?
Mkuu Tempolale, kumbe umegundua jinsi ninavyoichukia Chadema!.
Sisi watu wa kanda fulani, kuna wakati tukionyesha chuki, hiyo ndio namna yetu ya kupenda!.
Mfano wakati makabila mengine hutongoza kwa kubembeleza, sisi huwa tunawabaka tuu kwenye chagulaga!. Tukifiwa badala ya kulia lia, huwa tunakunwa sana na kuimba, unaweza kufikiri ndio tunafurahi, kumbe ndio tunahuzunika!.
Kwa vile unaamini naichukia sana Chadema!, kwa hiyo mimi ndio naipenda sana CCM na ndio maana chaguo langu kwa mgombea wa CCM ni EL if not Membe!.
 
Joka Kuu,

Kwa akili ya kawaida tu, ndani ya Tanzania ya leo, whether CCM ndio Maasisi wa neno Mapinduzi katika nchi yetu (sina uhakika ni CCM) au La, kilicho dhahiri zaidi kwa watanzania wenye upeo japo kidogo tu ni kwamba CCM haina tena yote haya yafuatayo when it comes to usage of the term Mapinduzi: CCM:


  • Haina tena CREDIBILITY;
  • Haina tena LEGITIMACY;
  • Na ilishapoteza AUTHORITY yote ya kusimamia Mapinduzi kwa vitendo;
Nilitarajia unaelewa fika kwamba kwa miaka mingi sana, tangia Marehemu Kolimba atoe kauli yake kuhusu CCM kutokuwa tena na Dira, CCM has been Facing A Crisis in its Political Hegemony; The fact kwamba Joka Kuu halioni hili, lazima nikiri kwamba ni mshangao mkubwa sana kwangu;

Kutokana na hili, nadhani ili kuondoa upotoswaji wa mada yangu, ningependa kwenda ndani kidogo kuelezea matumizi ya dhana ya Mapinduzi ndani ya CCM. Ni matumaini yangu kwamba pengine hii itatuweka mimi, wewe (Joka Kuu), na wadau wengine, katika nafasi nzuri zaidi ya kupima na kubaini iwapi neno MAPINDUZI katika nyakati hizi, is An ASSET or A LIABILITY, to Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tuanze na mtazamo na pia msimamo wa CCM juu ya Mapinduzi katika mazingira ya utawala na siasa kwa ujumla. Kwa mujibu wa Mwongozo wa CCM (1982), CCM inatamka hivi:

"…Ndipo tarehe 12.1.1964 Chama Cha Afro-Shirazi kikafanya mapinduzi halali ya silaha yaliyoitokomeza Serikali haramu ya Sultani mwezi mmoja baada ya Sultani na vibaraka wake wa Nationalist Party kukabidhiwa uhuru wa bandia na Waingereza."
"…Kwa hiyo, mara baada ya mapinduzi ya Zanzibar, Serikali ya TANU iliyatambua mapinduzi hayo na kuyaunga mkono kwa vitendo."
************

Tukizidi kuingia kwa undani juu ya matumizi ya CCM ya neno MAPINDUZI, tunaidi kubaini kwamba, kinyume na mtazamo wako, matumizi ya dhana ya MAPINDUZI kwa CCM ya leo ni Jambo la Kuliogopa kama UKOMA. Mwongozo wa CCM unazidi kutamka kwamba:

"Serikali ya Mapinduzi ya ASP haikuchelewa kuchukua hatua za kuimarisha ushindi iliyoupata dhidi ya usultani. Hatua muhimu katika fani za siasa, uchumi na ustawi wa jamii zilichukuliwa kama msingi wa kwanza katika kazi ngumu ya kuijenga jamii mpya ya haki na usawa. Ardhi ilitaifishwa na hodhi kubwa za makabaila wa kiarabu waligawiwa umma wa wananchi wasiokuwa na ardhi. Wakati huo huo mabenki na biashara ya nje zilitaifishwa na vyombo vya umma kuundwa."
******

Umaarufu wa CCM ulijengwa na Azimio la Arusha. Kwahiyo ebu tutazame matumizi ya dhana ya MAPINDUZI ndani ya mazingira ya Azimio la Arusha, Azimio ambalo mimi, wewe, wadau wengi humu, lakini pia viongozi wakuu wa CCM ya leo wote wana ufahamu kwamba CCM haitaki tena kulisikia wala kuhusishwa nalo [rejea Mazishi ya Azimio la Arusha Zanzibar 1992, na Kuzaliwa kwa Azimio la Zanzibar (1992), ambalo mpaka leo ndi limekamata kasi na kuzaa ufisadi unaowapa Chadema mtaji wa kisiasa Tanzania. Mwongozo wa CCM (1982) unasema:

"Kielelezo kimoja kikubwa cha uwezo wa Chama kukua na nyakati na kuelewa mahitaji halisi ya maendeleo ya mapinduzi ya umma ni Azimio la Arusha juu ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Kwa uamuzi huo, msingi mipya na ya kimapinduzi ya kulijenga na kulilinda Taifa iliwekwa hadharani. Kutaifishwa kwa mabenki, biashara ya nje na mashamba makubwa ya mabepari, kuundwa kwa mashirika ya umma na kuanzishwa kwa viwanda vya umma ni baadhi tu ya mambo yaliyodhihirisha nia ya Chama ya kuunda mfumo mpya wa uchumi utakaofanana na jamii ya kijamii inayodhamiriwa kujengwa."
*****

Mwisho, tutazame dhana hii ya Mapinduzi, hasa kwa ujumla wake katika utekelezaji wa sera za UKOMBOZI wa MTANZANIA ambapo iliaminiwa kwamba njia pekee ya kufikia ukombozi huo ni kwa: KUJENGA MSINGI WA UCHUMI WA UJAMAA NA TAIFA LINALOJITEGEMEA. Mwongozo wa CCM unatamka hivi:

"Lengo kuu la mapinduzi ya Tanzania ni kujenga nchi ya ujamaa ambamo unyonyaji wa mtu na mtu utakuwa umetokemezwa, ambamo uchumi wa taifa utakuwa unamilikiwa na kudhibitiwa na umma wa wakulina na wafanyakazi washiriki na ambamo uhusiano wa watu katika jamii utakuiwa ni wa udugu na kushirikiana kwa maendeleo ya wote na ambamo kati imepewa hadhi ya kuwa wajibu wa kila mtu."

Baada ya kujadili haya, Joka Kuu, sasa nadhani tupo katika mazingira bora zaidi ya kupitia item by item hoja zako kuu nne kama ifuatavyo:

..isije ukawa unatumia neno mapinduzi ili kuwatisha watu.

Joka Kuu, hauoni kwamba wenye kutishika na dhana hii ya MAPINDUZI ni CCM yenyewe na Viongozi Wake kuliko Chadema na Umma wa Wanyonge?

...najua nyinyi wana-CCM ni wajanja sana kutumia maneno na kuhadaa na kuwatisha wananchi.

Nyinyi wana-CCM ni kina nani hao? Ujanja, Hadaa na Vitisho ipo wapi? Naomba ufunguke zaidi ju ya hili;

..kumbuka kwamba CCM maana yake Chama Cha Mapinduzi.
Sio tu kwamba NAKUMBUKA, bali pia NAFAHAMU hilo na nilitegemea wewe pia ungekuwa na ufahamu wa hili, hasa the fact kwamba for the past 20 years or so, CCM is Facing A Crisis in its Political Hegemony, na ni moja ya sababu kubwa kwanini upinzani unazidi kushika kasi;

Vinginevyo sehemu pekee iliyobakia kwa CCM kutumia neno Mapinduzi ni completely out of Political and Social Contexts; Ni katika mazingira niliyojadili katika my original post, hasa Mapinduzi ya Kilimo. Lakini iwapo Viongozi hao hao wanaoaminiwa na wanachama wa CCM na sehemu kubwa ya jamii, wao kwao wao wanagongana tena kuhusu Mapinduzi ya Kilimo dhidi ya ELIMU KABLA, bado unadhani kweli dhana ya Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 ni ASSET kwa CCM hata nje ya social and political contexts? To me, katika nyakati hizi, matumizi ya neno MAPINDUZI kwa CCM, ni LIABILITY in a 360 degree context!!!

..we just need a better Tanzania…

Hakuna anayelikataa hili, vinginevyo kubali tu kwamba A BETTER TANZANIA ENTAILS SOME RADICAL CHANGES; how Radical? That's the essence of this debate; Na hoja yako kwamba "…we just need a better Tanzania" maana yake ya msingi kabisa ni kwamba Tanzania kama Taifa, hasa walio wengi, wanahitaji mabadiliko, sio mabadiliko ya mtu mmoja mmoja; Na tunarudi pale pale - ili kufanikisha mabadiliko kwa magnitude au kiwango kinachotarajiwa na UMMA, hilo haliwezi kutokea nje ya MAGEUZI au MAPINDUZI.

…sasa wewe ukiita mageuzi, mageuko, mapinduzi, hiyo ni juu yako.

Hili suala sio OPINION – RALATED, bali ni FACT – RELATED, and the essence of this deate pia ni a FACT FINDING MISSION, to shed more light in the Facts that are already known; Suala la msingi hapa ni sote kwa pamoja kuweka jitiada kuelewa maana ya dhana hizi mbili (Mageuzi na Mapinduzi) as Factual Matters, sio kwa maoni yangu au as you put it "juu yangu"; Lakini iwapo utaniruhusu niamzime hili neno lako la "JUU", basi niseme tu kwamba hatima juu ya Aina ya mabadiliko pamoja na Mbinu zinazohitajika kufikia kwenye mabadiliko tarajiwa ni "JUU" ya umma wa watanzania; Umuhimu wa M4C ni kuwaelimisha tu watanzania juu ya nini kinachoendelea, hasa wajibu wao kama raia ni nini, haki zao kama raia ni nini (social, political and economic justices), na muhimu zaidi, wajibu wa serikali kwa wao kama Raia ni nini.

Vinginevyo mkuu Joka Kuu, please try to spend a few seconds more to read posts kama hizi and also digest kwani lazima kuna posts nyingine utaona kuna some OBJECTIVITY, kwani sio kila Uzi wenye heading ya Chadema, Dr. Slaa, Zitto au M4c, ni Uzi wenye malicious intentions kwa Chadema, hence demokrasia yetu; Vinginevyo kukubali Kukosolewa and what transpires out of that should become one of Key ASSETS for Chadema kujipanga katika harakati zake za kuwaletea wananchi UKOMBOZI, 2015 and beyond.


Natanguliza samahani iwapo kuna lolote katika majibu yangu limekukwaza.
 
Chadema wanapozungumzia (M4C) wana maanisha nini? M4C inasimama badala ya movement for Change ina maana kubwa.

Mabadiliko kama mabadiliko yana maana na dhana kubwa mno ambayo inahitaji umakini kujadili kwa kina.

Dhana ya M4C ya chadema sijaielewa kabisa. Ndio maana mimi naiita "movement for power" na hii M4C ni kivuli tu cha kufikia malengo yao ambayo kwa uhakika sio yenye malengo ya kuleta mabadiliko katika nchi yetu.



Mimi siongelea kuhusu hisia hapa naongelea ''fact'' huo ndio ukweli.Wanachofanya ni kutaka kuondoa Regime tu lakini hakuna specific program ambazo watakuja ku implement ili ku transform jamii yetu.
.
.
Maadili pia ndani ya chama ni mabovu kama chama hakina order na discipline wakati hakiko madarakani kikiingia kitafanya nini? Chama chochote kitacho komboa Taifa hili ni kile viongozi wake wana maadili, kina Order na discipline ndani yake na viongozi wake wanaheshimiana na wanaongozwa na dira moja tu Utanzania.

Mtoa mada unasema kuwa M4C huielewi au unaielewa ??
Hapo juu kwenye blue, unasema huielewi !!
Halafu tena hapo kwenye red, unasema unaongelea fact !! Fact ya kitu usichokielewa ?? Au fact ya kitu gani ??
Rudi ukaeleweshwe vema kuhusu M4C. Ukishaielewa, uichambue, ndio uje na facts za M4C hapa JF.
Huwezi kusema unaleta facts za kitu ambacho wewe mwenyewe umesema hukielewi !!
Kwa kukusaidia tu, moja wapo za facts za M4C ni kuondoa utawala wa mafisadi na kuweka utawala adilifu wenye kuleta maendeleo ya Watanzania wote, sio maendeleo ya mafisadi. Hiyo ndio Change !!
 
ushauri:
mabadiliko ni zoezi kero na kadhia kubwa ktk jamii na hata makazini hata ktk jamii.. Ili'mabdaliko yaweze kutendeka thinkers wa zamani walisha weka hatua kadhaa ambazo bila kuzifuata hutapata mabadiliko kamwe. Hizi hatua kifupi ni kama ifuatavyo: 1. Waelimishwe watu kwa nini nia ya mabadiliko/mageuzi 2. Mwelekeo mpya 3. Kuungwa mkono 4. Kusimamia utekelezaji transition
5. kusimamia badiliko hilo.
6. Kujipima mara kwa mara kama usahihi upo

Mtoa mada pamoja na ana kuwa na nia nzuri ana tatizo la kuwa mbele ya ratiba na pengine hofu alipaswa kuchimba maandiko na hotuba kadhaa za viongozi wa cdm. Kumbuka ufafanusi anaoutaka hauna maana kama umma haujaunga mkono hoja, pia mengine ni ingredients under the ideology ambayo cdm tayari imeshaitangaza kwamba 'kuweka uchumi chini ya wananchi na serikali inayoendeshwa kwa nguvu za umma' . Baada ya hapo utajua hoja zote zinajijibu, kuwa hakuna nafasi ya kiongozi. kujilimbikizia mali akabaki salama wananchi wakilalama . Soma ilani za uchaguzi za cdm utafunguka.
 
Ngoja tuone nimetoa maono yangu. Chadema ikiingia madarakani tutaona. Lakini sina tumaini hilo la Mageuzi ya kweli. Kutokana na character zilizopo.
 
Mchambuzi,

..Thank u.

..binafsi nimekuelewa, lakini wasiwasi wangu ni kwa umati wa wa-Tz walioko vijijini ambao ndiyo wanaotakiwa kuya-execute hayo mapinduzi/mageuzi unayoyazungumzia.

..zaidi nakubaliana na wewe kuhusu umuhimu wa wananchi kuweza kutambua na kuwa na uelewa zaidi juu ya HAKI na WAJIBU wao kama raia wa Tanzania.

..mwisho, kuna ulazima wa sisi kama taifa kuamua tunataka kujenga jamii au taifa la namna gani. Horace Kolimba alipozungumzia CCM kukosa dira alikuwa anazungumzia CCM kukiuka misingi ya kuanzishwa kwa chama hicho.
 
Last edited by a moderator:
Mtoa mada naona kajipange upya, huelewi M4C halafu unaadika makala nzima kwa kitu usichokielewa! Kwa nini usiulize tu watu wanaoelewa wakueleweshe?
Halafu kwani hujui lengo la M4C ni kufanya Mapinduzi ya kidemokrasia na kuchukua uongozi wa nchi ili kuleta maendeleo ya nchi? Inabidi tu na wewe ujiunge na M4C kwa sababu na wewe ni mtanzania unahitaji kukombolewa badala ya kujiweka hofu na kuendelea kulalamika
 
Mtoa mada v4c vp? We waionaje na unashauri nini uwapo wa ccm na maendeleo yaliopo kwa miaka 50. Very low ms sayu. AGrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Mkuu huna haja ya kuzunguka zunguka; Kwa ufupi M4C inalenga kuleta mageuzi makubwa nchini katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa kupitia Mapinduzi ya kidemokrasia.
 
Mkuu huna haja ya kuzunguka zunguka; Kwa ufupi M4C inalenga kuleta
mageuzi makubwa nchini katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa kupitia Mapinduzi ya kidemokrasia.

Ili hoja yako hii ieleweke, ni muhimu ukatuzungusha japo kidogo KWA HOJA, vinginevyo ulichokisema hakijitoshelezi kwani CCM imekuwa inatekeleza mageuzi makubwa kwa miaka 26 sasa, na moja ya mageuzi hayo kwa mfano ni ya kisiasa ambayo yalipelekea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hence ujio wa Chadema 1995, mageuzi ya uchumi ambayo yameruhusu vyama vya upinzani mfano Chadema kuweza uza itikadi zao nje ya ile ya Ujamaa na Kujitegemea, n.k; nadhani you get my point- ili ueleweke, kuna umuhimu wa kuzunguka KIHOJA, vinginevyo ulichozungumza hapa hakina maana, na ni rahisi sana kika potoshwa na kikawekwa completely out of Context; Ni kwa sababu ya kuzunguka zunguka, ndio maana ni wachangiaji wachache sana humu ambao wananiuliza maswali, vinginevyo niliyosema kupitia mzunguko wa Hoja, kwa wengi yanajitosheleza na ndio maana tunaendesha Mdahalo tukiwa ukurasa Mmoja;mfano rejea post No.35 ya uzi huu by karug;

Ushauri wangu ni - jaribu kuzunguka zunguka kidogo, KWA HOJA, ili ueleweke vyema;
 
CCM wanatamani kutawala milele. Mtoa hoja unajichanganya kujadili kitu usichokielewa na hii inatokana na aidha umetumika ama chuki binafsi na mabadiliko ya kifikra waliyonayo watanzania na kampeni za M4C. Naamini lengo kuu la kuanzisha M4C ni kuwafikia watanzania wengi hasa walio vijijini na kuwapa elimu ya uraia, jambo hili kwa muda mrefu halijafanywa na viongozi wa siasa hasa wa upinzani, sasa wameamua kwa dhati kufanya mnawapinga kwa kalamu na hata risasi.. Nimeamini ukombozi wa kweli unahitaji uvumilivu wa hali ya juu kupatikana.
 
Sijui Kama utanipata mimi kwa propaganda zako hizo
Mwanzo mulikuwa munasema mutatawala milele sasa mumeona moto munasema vyama vyote viko sawa usitucheleweshe kwenye mabadiriko M4C kuwa movement for power kuna kosa gani chama chchote cha upinzani kazi yake kubwa ni kukiondoa kile kinachotawala
Unasema chadema hawana nidhamu kichama kwa hiyo wakiwa madarakani hakutakuwa na jipya unathibitisha kwamba lengo lako ni kutaka chama tawala kibaki madarakani
 
Kwanza nimekugongea like kwa kunisemea Mkuu. Pili nawasemea watanzania wa level tofauti, watz Kama wewe haupo ni wewe ila waliowengi hawajali kuwa ni mapinduzi Au mageuzi wanachotaka ni ccm ife waanze upya. Tuanze na slogan ya I can't but we can, and yes tz we can without being beggars of IMF, western country and Europe we can do it only if we want it. Tatizo lililopo ni nani aanze... Napita tuu



Nakubaliana na wachangiaji wenzangu. Kitu ambacho hatuelewi watanzania hasa viongozi na wasomi ni kuendelea kufikiri maendeleo yataletwa na hiyo mikakati inayotoka world bank na kwingineko i.e. Mkukuta, tasaf etc.

Haya mataifa yanayotoka eg china, korea, india hata iran kwa asilimia kubwa wamepiga hatua kwa kutumia bongo zao wenyewe ikiwa ni pamoja na kununua au kuiba technology ambayo wanajua itawatoa!

Mapinduzi ninayofikiria mimi ni katika elimu, mtoa mada huenda wewe ni mhadhiri chuo fulani, tunahitaji mfumo utakaofanya watanzania wafikir kwa akili zao namna ya kutoka (to progress) kama wachaga wanavyoanza kwa kuuza karanga barabarani, kaduka, duka, retail, whole sale etc.

Kwa kweli wananchi tumechoka kiasi kwamba hayo mageuzi au mapinduzi yaje tu tuone the other side of the coin. Will be positive with positive thinking (which we lack), negative if we continue the way we think now!
 
Labda niseme tu kwamba,ni wazi kwamba watanzania wanahitaji mabadiliko,na Chadema kikubwa kilichfanya mpaka sasa, ni kuonyesha au kudhihilisha mabaya ya selikali ya CCM ,naipongeza sana kwa hilo,kwa maana hii ni hatua ya mwanzo. Kama Chadema kweli ni Chama cha kuiongoza, au kuikomboa Tanzania, basi mimi niseme sio kwa mwaka 2015.Imekuwa ni kawaida sana kwa viongozi wengi wa nchi za Africa kutaka kushika dola,au madaraka pasipo kuwa au kuonyesha mbinu mbadala (kwa uzito unaostahili) kwamba watafanya nini tofauti na wale walio madarakani.Nchi za Africa zina matatizo makubwa ambayo majibu yake sio ya rahisi.Ni muda wa kuelimisha,na kujijuza kuona nini ni ufumbuzi wa matatizo yetu.Sio kuchukua muda mwingi kupigania kuongoza nchi!!Utaongoza vipi watu ambao hujawatayarisha kifikra(kwa kuwapa mipango yako sasa) kabla hujashika dola!!?..watakushinda!!,hutawapeleka popote!Chadema(au chama kingine chochote) kinahitaji kuja na maono,mikakati,au majibu ya changamoto za sasa na za kesho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom