MDAHALO: Kikwete akivunja baraza la mawaziri atathibitisha udhaifu wake

Labda ni wakati wa kuwaleta maadui wengine karibu zaidi; maana kuna wengine wanapiga kelele sana nje ya serikali sasa njia nzuri ni kuwaleta ndani... Fikiria wizara ya madini wakimtoa Ngeleja na kumuingiza mkosoaji wake mkuu; Ngeleja akiwa Mbunge atampa sapoti au na yeye atajitahidi kumsabotage?

Hakuna kitakacho badilika kwani yeyote atakayeteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini, ataendelea kuweka interest za wawekezaji mbele kwanza kabla za wenye rasilimali (watanzania). Kitakachobadilika labda ni uwiano tu wa 80:20, 70:30, n.k. Ngeleja ana mapungufu yake lakini Mbunge yeyoye atakayemrithi ni dhahiri hatoteuliwa based on Merit - kwa mfano the Mwanri's and Magufuli's haitatokea wakateuliwa kushika Wizara kama ya Nishati na Madini. Mbunge atakaye pelekwa pale lazima atateuliwa ili aende kwanza kulinda maslahi ya kisiasa, na pili, kuendelea kulinda maslahi ya wawekezaji, huku pia akiwa na jukumu la kuficha maovu yanayoendelea kule migodini, hasa ukweli kuhusu madhara ya kemikali kwa wananchi wasio na hatia. Kwa wenye rasilimali (watanzania wa maeneo yale), ni bahati mbaya sana kwamba watakachoendelea kuchuma itakuwa ni 'side effects'.

Vinginevyo iwapo atatoka, nadhani Ngeleja hatokuwa na la kufanya zaidi ya ku-adopt into siasa zisizofungamana na upande wowote kwani ni dhahiri kwamba bado 'atajali maisha yake na ya familia yake'.
 
Kuvunja baraza la mawaziri ni moja ya maamuzi magumu. Vunja na kila alieshindwa kufanya kazi yake kwa ufanisi asirudi tena

Asipovunja ni udhaifu, kwa kuwa hakuna asiyejua baraza la sasa lina upungufu mkubwa. Mawaziri wanaongea bila kuwa na utartibu maalumu wa kuongelea mambo na wanakinzana, na uwezo wao kiutendaji umeonekana kuwa mdogo, hawawezi kushughulikia ipasavyo mambo ambayo wanatakiwa kushughulikia. Mfano, mfumuko wa bei, mgomo wa madaktari etc, lakini Kibaya zaidi akilivunja ndio utakuwa udhaifu zaidi itathibitisha malalamiko ya watu kuwa lilikuwa baraza dhaifu, na huenda tutakachokiona hakitakuwa kuvunja bali itakuwa ni resshuffle, mbovu huyu kumhamishia pabovu pale, au kumuondoa anayefaa na kumwingiza asiyefaa, even worse uaweza kushangaa kuwa Lowassa waziri tena, kitu ambacho kitakuwa disaster. Ukiwa katika hali ya damn if you do, damn of you don't, ni bora kuacha hali hii ya sasa.
 
Kumekuwepo na tetesiza uwezekano wa kuvunjwa kwa baraza ka mawaziri wakati wowote kuanzia sasa. Na wapo watu ambao wametoa wito kwa rais kufanya hivyo. Je hoja ya mdahalo huu ni ya kweli au siyo kweli na kwa nini?

hoja hiyo inaweza kuwa kweli kulingana na kutofautiana kwa hali ya juu kwa baraza lake la sasa la mawaziri. Wakati mwingine hata ye m/kiti kuwatofauti na mawaziri wake!
 
Atakuwa anavunja baraza kila wakati bse anaowateu wengi hawastaili.
So wasi wasi wangu ni baada ya kuvunja atawachagua akina nani wakati system yake ya kuweka watu si ya kuzingatia criteria kama za waliomtangulia kama Mkapa,Mwalimu etc
 
Tatizo kubwa la kuvunja baraza la mawaziri kuwa atakapoamua kuunda baraza jingine ataangalia kutoka kwenye pool ile ile - Bunge. Sasa huko Bungeni ni nani ambaye tunaweza kusema anaweza kuwa tofauti na hawa waliopo sasa kiasi kwamba tunaweza kusema atafanya kazi tofauti na hawa? Hivi kama maji yamechafuka hata ubadilishe unachochotea bado utachota maji machafu!
 
Tatizo kubwa la kuvunja baraza la mawaziri kuwa atakapoamua kuunda baraza jingine ataangalia kutoka kwenye pool ile ile - Bunge. Sasa huko Bungeni ni nani ambaye tunaweza kusema anaweza kuwa tofauti na hawa waliopo sasa kiasi kwamba tunaweza kusema atafanya kazi tofauti na hawa? Hivi kama maji yamechafuka hata ubadilishe unachochotea bado utachota maji machafu!
Bado anazo nafasi 7 za kuteua watu wakawa Wabunge kisha akawateua kuwa mawaziri. Mara hii hatavunja Baraza la Mawaziri bali atafanya mabadiliko ya hapa na pale. Wizara zinazohitaji mabadiliko ni:
-Katiba na Sheria kwa ajili ya hitaji la Katiba Mpya. Asha Rose anatarajiwa kuwa hapa au atapewa Uenyekiti wa Tume kama SAS na Jaji Warioba watadengua.
-Wizara ya Nishati na Madini ambako waziri wake amepwaya kupita kiasi na anazitafuna taasisi zilizo chini ya wizara hii kama mtu asiye na akili nzuri.
-TAMISEMI ambako ubadhirifu umekithiri.
Jamaa wanaopigiwa upatu na wenyewe kuonekana wanapiga jaramba ni:
-Januari Makamba.
-Anne Kilango.
-Aggrey Mwanri
-George Simbachawene
-Dr AshaRose Migiro
-Zitto Kabwe. Mbowe na Dr Slaa wameridhia hili eti?
 
Hadi wazungu wa Uingereza na Marekani wanajua kuwa Kikwete ni Rais dhaifu sana asiye na upeo katika Africa. Pendelea kusikiliza maoni yao kunapotokea multinational event.
Hivi sasa wanamkubali zaidi Kagame wa Rwanda.
For them JK is their last selection if not
 
Je, unafikiri sasa hivi akivunja baraza la mawaziri au kufanyia kufanyia mabadiliko makubwa atajionesha kuwa ni kiongozi makini?
 
Kumekuwepo na tetesiza uwezekano wa kuvunjwa kwa baraza ka mawaziri wakati wowote kuanzia sasa. Na wapo watu ambao wametoa wito kwa rais kufanya hivyo. Je hoja ya mdahalo huu ni ya kweli au siyo kweli na kwa nini?

Hoja ya mdahalo ni ya kweli au si ya kweli fifty fifty.Kama atavunja baraza hili basi aunde serikali ya umoja wa kitaifa na cuf tu ili amchague Lipumba awe waziri wa uchumi,mipango na fedha,labda anaweza kumsaidia.Otherwise asivunje ili kumbikumbi waongezeke.
 
Nothing will change hata awe anavunja kila siku hilo baraza

The problem ni operating system tuliyoichukua, iko fragmented, porous, remotely controlled by dubious foreigners na system imeshindwa kutupa economic protetion wala advice, ila imejikita kwenye protection ya power ya politicians
 
hUO UTAKUWA UDHAIFU USIO MFANO...LAKINI NI BORA ALIVUNJE ILI IONEKANE ANAHUJUMIWA NA WATENDAJI WAKE KULIKO KUBAKIA NA BARAZA HILI LA SASA.

bARAZZA LIJALO AWAWEKE HATA WAPINZANI JUKWAANI NADHANI HALI ITAKUWA SHWARI TU

Mkuu wapinzani wa nini tena kwenye baraza la mawaziri la serikali ya CCM? Wapinzani si wanasubiri uchaguzi ili wakishinda waunde serikali yao. Wakiingizwa serikalini si itakuwa ni ndoa kama ile ya CUF na CCM kule visiwani?
 
Hakuna kitakacho badilika kwani yeyote atakayeteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini, ataendelea kuweka interest za wawekezaji mbele kwanza kabla za wenye rasilimali (watanzania). Kitakachobadilika labda ni uwiano tu wa 80:20, 70:30, n.k. Ngeleja ana mapungufu yake lakini Mbunge yeyoye atakayemrithi ni dhahiri hatoteuliwa based on Merit - kwa mfano the Mwanri's and Magufuli's haitatokea wakateuliwa kushika Wizara kama ya Nishati na Madini. Mbunge atakaye pelekwa pale lazima atateuliwa ili aende kwanza kulinda maslahi ya kisiasa, na pili, kuendelea kulinda maslahi ya wawekezaji, huku pia akiwa na jukumu la kuficha maovu yanayoendelea kule migodini, hasa ukweli kuhusu madhara ya kemikali kwa wananchi wasio na hatia. Kwa wenye rasilimali (watanzania wa maeneo yale), ni bahati mbaya sana kwamba watakachoendelea kuchuma itakuwa ni 'side effects'.

Vinginevyo iwapo atatoka, nadhani Ngeleja hatokuwa na la kufanya zaidi ya ku-adopt into siasa zisizofungamana na upande wowote kwani ni dhahiri kwamba bado 'atajali maisha yake na ya familia yake'.

Mkuu Mchambuzi umenena sawa. Lakini ina maana wewe unawaamini Mwanri na Magufuli?
 
Last edited by a moderator:
acha alivunje, asipolivunja maana yake anafurahishwa na uozo unaendelea, na ndio itakuwa anaizika ccm:bathbaby:
 
Labda ajipangue, na yeye mwenyewe asiwepo madarakani

I agree with you hapa, hivi bado kuna watanzania ambao hawana taarifa mpaka sasa kwamba rais wao ni dhaifu mpaka avunje baraza la mawaziri? Kama wapo basi ni wachache sana sana. Baraza hatavunja, actually sioni sababu kwanini avunje kwani kilichopelekea haya yote ni report ya CAG na kamati za bunge. Mambo haya yamekuwepo miaka yote ya awamu ya nne, report za CAG kila mwaka ni mbaya kuliko mwaka uliotangulia, alikuwa wapi kuvunja siku zote? By the way, hivi bado kuna watu wanaamini kwamba urais wa kikwete ni kwa ajili ya Tanzania na watanzania wake? Kama wapo mimi si mmoja wao. Kila kitu ni business as usual mpaka 2015.
 
Jamani tuwe wakweli, JK akilivunja baraza lake la mawaziri inabidi amrudishe Mh. Edward N. Lowassa kuwa waziri mkuu. Ndani ya CCM hakuna kama Lowassa kwa uchapa kazi.
 
jk ni dhaifu katika uongozi na pia anaweka maslahi binafsi mbele kuliko utendaji, hata akivunja na kuchagua baraza la mawaziri bado halitafaa kwa vile hawezi kulisimamia
 
Jamani tuwe wakweli, JK akilivunja baraza lake la mawaziri inabidi amrudishe Mh. Edward N. Lowassa kuwa waziri mkuu. Ndani ya CCM hakuna kama Lowassa kwa uchapa kazi.

Huwa sikuelewi mkuu. unanikumbusha enzi za farao.
 
Je, unafikiri sasa hivi akivunja baraza la mawaziri au kufanyia kufanyia mabadiliko makubwa atajionesha kuwa ni kiongozi makini?

MM, siku hizi sijui wanausemi gani! miaka ya 47 walitumia msemo huu "UKINIPIGA UMENIONEA, UKINIACHA UMENIOGOPA" Watakao teuliwa ikiwa atalivunja baraza la mawazili, tayari atakuwa amewawekea chip akilini kuwa wanawajibika kwake pekee!!!!!! kama inavyojidhihirisha kwa akina Maige, jairo, Ngeleja . . . . na mfano ulio wazi zaidi ni huu, Selina Kombani wakati fulani alituambia watanzania kuwa hakuna haja ya kuandika katiba mpya, Ndani ya muda mchache jk akamwagiza kupelega bungeni muswada wa kuandika katiba! hii ilikuwa contradiction kwa Kombani ambayo ingemlazimu kuvaa kinyago kuwaangalia usoni wale aliowaambia katiba NO! ama angejiweka pembeni! lakini kwa kuwa ana enmbeded operating system kwenye ubongo wake, yupo yupo tu kama zuzu! Akilivunja baraza ataharibu zaidi, na akiwalazimisha kujiuzulu atajitwika dhima ya makosa wayafanyayo mawaziri.
 
Mkuu Mchambuzi umenena sawa. Lakini ina maana wewe unawaamini Mwanri na Magufuli?

Binafsi sidhani kama wabunge/mawaziri wengi wanatetea maslahi ya umma per se. Wabunge wengi wa CCM pamoja na baadhi ya mawaziri ambao we perceive them kama wachapa kazi na wenye msimamo wanafanya hivyo ili kujijenga kisiasa kikanda au kitaifa; kwa wengi pia ni njia ya kujikinga na dhoruba la chadema huko majimboni mwao as we head towards 2015. Sitashangaa kuona wabunge wengi wa sasa CCM kuhamia Chadema katika kipindi cha mwisho mwisho kuelekea 2015. Hivyo Mkuu Kimbunga, sina ushahido tosha wa kuwaamini Mwanri na Magufuli kwa asilimia 100, wote hao nawaweka katika makundi hayo juu.
 
Back
Top Bottom