MDAHALO: Kikwete akivunja baraza la mawaziri atathibitisha udhaifu wake

Chintu uko sahihi kabisa na kumlinganisha SITTA na SLAA ni kumuonea SLAA kwani aliyezuia ile hotuba isijadiliwe ni nani kama siyo SITTA? kwa hiyo yale alisema kutukoga wabongo na Bongo zenye tongotongo (hatuoni)

kuhusu Magufuli; Huyu ndo hovyo kabisa maana yeye ni mkandamizaji mkubwa wa demokrasia na hasa inapofikia kusema lolote kuhusu CHADEMA. Kumbuka maoni yake dhidi ya Mnyika; Dhidi ya Mbunge wa Ukerewe na dhidi ya CHADEMA kwa ujumla. I declare my interest; Mimi ni mwanchama wa CCM lakini unafiki wa Magufuli na viongozi aina yake dhidi ya demokrasia vinanikera sana. Sijafikiria kuhama CCM wala sidhani kama nitafikiria lakini lazima tujue nchi inaliwa na mijitu michache.

Kikwete avunje baraza la Mawaziri; thubutu!!! Kuna kiongozi mmoja wa juu ndani ya CCM aliwahi kusema; Ukitaka Kikwete atoe maamuzi manzito basi ni lazima mumshikilie asipate nafasi ya kutoka hadi aamue vile mnataka na ndiyo maana kuvunja secretariet ya kamati kuu ya CCM ililazimu mikutano ya non-stop hadi saa 6 usiku ndipo akaamua kuvunja na hata aliposhauriwa baada ya kuvunja usimrudishe yeyote kati ya wale wa zamani; alipopewa upenyo tu; Aliwarudisha baadhi yao kama Pindi chana na Chiligati.

Akivunja baraza hili; basi Waziri mkuu atakuwa Lukuvi na huo ndo utakuwa mwisho wa Ujenzi wa Mpanda University; Waziri wa Nishati na madini January Makamba naibu Kafumu Dalai; mambo ya Nje Emanuel Nchimbi naibu Sophia Simba (utani huu); Elimu ya Juu Prof Peter Msolla Naibu...

Hawezi; Nasema hawezi!!!!!!

Nakubaliana nawe mkuu, Ni kweli Sitta ni miongoni mwa watu waliojichanganya sana kipindi cha Kikwete. Mimi simtetei Sitta ila nadhani Sitta angeweza kuwa spika mzuri zaidi kama kungekuwa na Rais jamii ya Dr Slaa. Alijaribu na ana-deserve credit katika hilo, lakini ukiwa mtu makini ni vigumu sana kufanya kazi na Rais asiye na userious kwa lolote, maamuzi mengi mabovu aliyokuwa akifanya Mh Sitta alipokuwa spika alikuwa akiyafanya bila ridhaa ya moyo wake bali shinikizo. Haikuwa kazi rahisi, si unakumbuka kuna kipindi aliomba kuongezewa ulinzi? wenye chama chao wakamtishia kumnyanganya kadi? there were a lot happening behind the scene - Ingawa nakubali alitakiwa abaki jasiri.
Juu ya Magufuli I have mixed feelings, and I think you have a point.
 
Kwa nini avunje sasa na toka mwaka jana???????

Binafsi naona
  • Kuvunja baraza katika mazingira haya kwanza haitampa credit yeyoye hata yeye. Its too late Kwenye ulimwengu huu TEKNOHAMA wanasema ukichelewa kufanya decision uliyotaiwa kufanya juzi ukaifanya leo ni madhara.
  • Pili tuki asasume its never late ambayo ndio kasumba yetu Swali likakuja akivunja option atakazokuwa nazo ni za kina nani? JK kamfanya PM wake ambaye kwangu namuona kama katika viongozi wachache waadilifu ameonekena "katuni". It tell a lot kuwa Pinda hakuwa chaguo la JK .

Kifupi Jk anaweza kuchange sura za watu(Kisiasa) lakini ni yeye mwenye anatakiwa kuwabadilika kuwa leader ili kuwepo na communication na utendaji wa cabinet kama ni weli ndiyo nia yake.

kwa tetesi siwezi kukataa kuwa siku nyingi sana (Toka sakata la Jairo) PM Pinda alishaomba kuachana na sanaa za JK . Sasa hii ya Posho za bunge.

So hapa nadhani PM kaomba kujiuzulu lakini kwa hesima ya rais na Ikulu inabidi movie ibadilishwe kwa kuvunhja baraza la mawaziri na isionekaa uwa ni PM kaomba kujiuzulu....
 
Hakuna baraza wala rais wote ni hopeless moving figure,kikubwa hapa ni kuendelea kujipanga kuyatoa haya mafisadi.mawaziri hawa mkumbuke wanatoka CCM,watakaoteuliwa watatoka CCM,Rais anatoka CCM,hapo mnategemea kitu kipya kitoke wapi?maana msisahau kuwa wanatoka chama kinacholea na kufuga mafisadi,na wao wote ni mafisadi,hakuna msafi hapo,na mfumo wao wa uongozi ni wa kifisadi na ni lazima watetee mafisadi.mimi sioni kana kutakuwa na jipya wala hakuna tofauti,akilivunja ni Rais dhaifu na asipolivunja baraza la mawaziri bado ni Rais dhaifu.
kwangu mimi atakuwa imara kama atakubali kushindwa na kuchukua uamuzi wa kupisha watu makini kutoka chama makini waongoze nchi.
 
Hii ilikuwa wakati wa Nyerere tu. Hata ukiambizwa kwamba utateuliwa nafasi fulani halafu ukaenda ongea na mkeo na yeye akaipeleka kwa mashoga na majirani, uteuzi wako unafutwa. Uteuzi au kufukuzwa kazi vilikuwa vinasikika kwenye redio tu, hasa saa mbili usiku.

hili kweli kabisa; kuna watu walikuwa wakiitwa Ikulu walijua kuna mawili tu - kupandishwa cheo au kuondolewa! Ukisikia mtu ameitwa Ikulu hucheki hadi akirudi!
 
Kumekuwepo na tetesiza uwezekano wa kuvunjwa kwa baraza ka mawaziri wakati wowote kuanzia sasa. Na wapo watu ambao wametoa wito kwa rais kufanya hivyo. Je hoja ya mdahalo huu ni ya kweli au siyo kweli na kwa nini?
Kwa upeo wangu mdogo, huwa nafikiria kwamba Asha Rose akirudi nyumbani, mheshimiwa atalazimika kufanya mabadiliko kwa ajili ya kumu accomodate. Akili yangu fupi inaniambia kwamba Dr. Asha lazima atateuliwa kuwa mbunge na hapo hapo kupewa Wizara muhimu kama vile Viwanda, na pengine Fedha. Kama akili yangu ina usahihi kidogo, basi itamlazimu Mheshimiwa avute subira mpaka hapo Dr. Asha atakaporudi ili atumie nafasi hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja.

Vilevile akili yangu inanifanya nione kama mheshimiwa pia itabidi kuvuta muda ili kuangalia hali za kiafya za Mwandosya na Mwakyembe maana kuwaacha hawa ina maana wanapoteza kwa kiasi fulani matunzo ya serikali ki-afya. Hii ni hatari hasa ikizingatiwa kwamba kuna tetesi mkono wa mtu umewadhuru hawa. Lakini ngumu zaidi ni kwamba kujaza nafasi ya uwaziri kutoka moja wa wabunge wa Mbeya itakuwa ngumu kwani hakuna wabunge waliosalia kule ambao wana sifa za uwaziri na kumrudisha Mwakyusa itakuwa ni kichekesho kwani wengi watahoji, kwanini aliachwa?
 
......... Lakini ngumu zaidi ni kwamba kujaza nafasi ya uwaziri kutoka moja wa wabunge wa Mbeya itakuwa ngumu kwani hakuna wabunge waliosalia kule ambao wana sifa za uwaziri na kumrudisha Mwakyusa itakuwa ni kichekesho kwani wengi watahoji, kwanini aliachwa?

kwani akiondoka waziri Mwa...... lazima nafasi yake izibwe na Mwa.....
 
Kwa upeo wangu mdogo, huwa nafikiria kwamba Asha Rose akirudi nyumbani, mheshimiwa atalazimika kufanya mabadiliko kwa ajili ya kumu accomodate. Akili yangu fupi inaniambia kwamba Dr. Asha lazima atateuliwa kuwa mbunge na hapo hapo kupewa Wizara muhimu kama vile Viwanda, na pengine Fedha. Kama akili yangu ina usahihi kidogo, basi itamlazimu Mheshimiwa avute subira mpaka hapo Dr. Asha atakaporudi ili atumie nafasi hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja.

Vilevile akili yangu inanifanya nione kama mheshimiwa pia itabidi kuvuta muda ili kuangalia hali za kiafya za Mwandosya na Mwakyembe maana kuwaacha hawa ina maana wanapoteza kwa kiasi fulani matunzo ya serikali ki-afya. Hii ni hatari hasa ikizingatiwa kwamba kuna tetesi mkono wa mtu umewadhuru hawa. Lakini ngumu zaidi ni kwamba kujaza nafasi ya uwaziri kutoka moja wa wabunge wa Mbeya itakuwa ngumu kwani hakuna wabunge waliosalia kule ambao wana sifa za uwaziri na kumrudisha Mwakyusa itakuwa ni kichekesho kwani wengi watahoji, kwanini aliachwa?

Mchambuzi,

..hivi Dr.Migiro hawezi kupewa tume ya katiba?

..kwa kumbukumbu zangu Dr.Migiro alikuwepo kwenye tume ya Justice Kisanga na kutokea huko ndiyo nyota yake kisiasa ikaanza kung'ara.
 
Kumekuwepo na tetesiza uwezekano wa kuvunjwa kwa baraza ka mawaziri wakati wowote kuanzia sasa. Na wapo watu ambao wametoa wito kwa rais kufanya hivyo. Je hoja ya mdahalo huu ni ya kweli au siyo kweli na kwa nini?
...Labda tujiulize, "Je, kuna faida yeyote itakayopatikana kwa kuvunja baraza la mawaziri?"

...On this one, i'm indifferent.
 
una maono makubwa sana kijana
umenikuna na maneno yako
Kuna mdahalo mmoja wa wagombea urais mwaka 1995 Mh Mrema aliongea point moja muhimu sana kama unakumbuka. Alisema watamnzania wasifanye utani katika kuchagua Rais, kwa sababu Rais ndiyo dira ya nchi itakavyoendeshwa. Mkichagua mtu wa mzahamzaha hata wezi na mafisadi wanajua kuwa aliyepo pale juu ni mtu wa mizahamizaha tu - hawamwogopi. mkimchagua mtu asiye na utani kuhusu ujambazi, hata majambazi pia yanajua kuwa aliyepo pale juu hana utani na majambazi, na alitoa mfano kuwa kipindi alichokuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa na uwezo wa kuwaamrisha majambazi warudishe silaha na walirudisha kwa sababu walimjua hana mzaha na ujambazi.
Leo hii Mafisadi wakisikia Dr Slaa anaingia ikulu wala hutahitaji kuwaambia acheni ufisadi, utashangaa tu kila aliyekuwa fisadi anaanza kubehave. Sura ya Rais inabidi iwe na ujumbe kwa waovu wote ndipo nchi itaenda. Watu walishatilia mashaka sura ya Rais wetu tangu anaingia madarakani 2005, alipodokezwa kuwa watanzania wakiisoma sura yako hawaoni ujumbe wowote zaidi ya mizaha akang'aka na kusema wasubiri waone. Tukasubiri kweli,na bahati nzuri wala haikuchukua muda mrefu ikaja EPA si unakumbuka siku alipohutubia bunge kwa masaa matatu na kuhitimisha kwa kusema mafisadi wana haki zao, halafu akawapa muda warudishe walichoiba mwisho October? Sitta akasimama akamuangalia usoni hakummaliza kwa sauti iliyoonyesha wazi alivyombore akamuomba Mheshimiwa hizo sheria si utuletee tukutengenezee maana hiyo ndio kazi yetu kama bunge - Ile hutuba ilizuiliwa kujadiliwa na bunge na kuna tetesi walikataza isichapwe kwenye hansard kuepusha aibu. Kuna mengi yameendelea kutokea baada ya hilo ambapo Rais wetu ameendelea kuonyesha mizaha na udhaifu mkubwa. Mawaziri wanajua hivyo ndio maana wanaiogopa CDM zaidi kuliko hata aliyewateua. Hivi sasa nchi inaongozwa na CDM. Rais anaiogopa CDM, mawaziri pia wanaiogopa CDM kuliko hata aliyewateua maana wanamjua hana noma! Mi nadhani tatizo kubwa tulilonalo waTz ni Rais na wala si mawaziri. Nina imani mawaziri serious (e.g Magufuli) wanapata shida sana kufanya kazi chini ya Rais wetu, tuna Rais ambaye tunajua anavyovipenda tu lakini hatujui anachokichukia (ukiacha kile kigoda cha Mwl Nyerere).
 
kwani akiondoka waziri Mwa...... lazima nafasi yake izibwe na Mwa.....

Hahaha. Basi angalau huyo mwingine awe 'Mwi' ili mradi awakilishe mkoa wa Mbeya. Uteuzi wa mawaziri lazima uwakilishe mikoa/makabila. Hii sio sheria rasmi lakini practice huwa ipo hivyo. Ndio maana unaweza kukuta kuna mawaziri wengine bogus kabisa lakini wanabebwa na suala la uwakilishi.
 
Mchambuzi,

..hivi Dr.Migiro hawezi kupewa tume ya katiba?

..kwa kumbukumbu zangu Dr.Migiro alikuwepo kwenye tume ya Justice Kisanga na kutokea huko ndiyo nyota yake kisiasa ikaanza kung'ara.

Inawezekana kabisa lakini siasa za nyakati hizi mimi nadhani zimekaa zaidi mkao wa 'unataka nini' kuliko merit au experience.
 
Kumekuwepo na tetesiza uwezekano wa kuvunjwa kwa baraza ka mawaziri wakati wowote kuanzia sasa. Na wapo watu ambao wametoa wito kwa rais kufanya hivyo. Je hoja ya mdahalo huu ni ya kweli au siyo kweli na kwa nini?

Kwanza tujiuliza 'red flag' hapa ni jambo gani? Sakata la Jairo? Mgomo wa madaktari? Mkanganyiko wa posho za waheshimiwa na kauli tata za madame spika na waziri mkuu? Hivi kweli haya yanatosheleza kuvunja baraza!

Labda tuseme akafanya RESHUFLE ya kawaida tutasema kavunja baraza? au kuna tetesi za kumpiga chini mtoto wa mkulima na hiyo hadi avunje baraza zima?
 
Rais wetu hajaprove failure kwenye uongozi tu bali pia teuzi zake mbalimbali zimekuwa hazina tija kwa taifa.Watu makini ambao wangemsaidia hawana sifa zake na pia wale makini anaowabahatisha hawaperform kama ambavyo ilitegemewa(Magufuli).Serikali yake yote inaenda kwa "the common failed ways"!Hata akifanya mabadiliko sidhani kama itamsaidia kupata timu nzuri kwa kuwa tu ni yeye mwenyewe ndiye atakayeteua kwa vigezo vilevile vinavyomfelisha kila siku.Hataweza kuepuka ulegelege kwa kubadilisha wachezaji wote dk ya 63 wakati timu ambayo yeye ndiye kocha mchezaji imeshafungwa mabao tisa kwa bila!Either aendelee hivyohivyo au abadilishe yeye na timu yake wote ni legelege.Angalau tungesema timu mpya iingie na kepteni mwingine labda ingesaidia.Maadamu ni yeye basi atakuwa yuleyule jana,leo na hata kesho.Tusubiri dk 27 tuingize timu mpya na kepteni mpya hawa wa sasa haiwezekani tena kutuokoa.Inawezekana tukawa tumeshashuka daraja mpaka mwisho lakini tukipata timu nzuri tunaweza kupanda vizuri tu.Udhaifu wa Kikwete hautafutwa kwa kubadilisha sura za mawaziri bali ni kukubali kuwa ameshindwa aachie ngazi.
 
Hahaha. Basi angalau huyo mwingine awe 'Mwi' ili mradi awakilishe mkoa wa Mbeya. Uteuzi wa mawaziri lazima uwakilishe mikoa/makabila. Hii sio sheria rasmi lakini practice huwa ipo hivyo. Ndio maana unaweza kukuta kuna mawaziri wengine bogus kabisa lakini wanabebwa na suala la uwakilishi.

Na hili ndio Gonjwa lingine lilalotutafuna.

Mi nitapenda kusiaki katika baraza Jipya JK mwenyewe ajipe uwaziri wa mambo ya Nje. Hizo kofia mbili zina mfit. Atashrikianana naibu waziri kuendesha wizara bila tatizo.......
 
Afanye atakavyo na baraza la mawaziri but nothing will change kwanza watu wenyewe wanawindana na sumu za panya!

Kwangu mimi nadhani muhimu kabisa kwenye katiba inayokuwa tupunguze muhula wa urais toka miaka 5 hadi minne. Miaka 10 ya legelege is a very loooong time.
 
Tatizo ni kuwa hata likivunjwa,tunaowategemea wapya ni kina nani kama sio sampuli ile ile tu.
Kuvunja baraza itakuwa njia sahihi angalau kuja na timu nyingine itakayoleta tija kwa miaka iliyobakia ya utawala wake. na sababu za kufanya hivyo ni wazi zipo kutokana na mambo yaliyojitokeza karibuni,
-Sakata la madaktari,
-Sakata la Sitta na Mwakyembe
Lakini pia sidhani kama kuna ufanisi wa kuendelea na mawaziri ambao dhahiri wameonyesha moja kwa moja kushindwa kutekeleza majukumu yao.
 
Afanye atakavyo na baraza la mawaziri but nothing will change kwanza watu wenyewe wanawindana na sumu za panya!

Kwangu mimi nadhani muhimu kabisa kwenye katiba inayokuwa tupunguze muhula wa urais toka miaka 5 hadi minne. Miaka 10 ya legelege is a very loooong time.
FJM

Tatioz ni uongozi na mtu na sio muhula . kwa taifa masikini kaaletu tunahitaji rais mzuri hata kwa muhula wa miaka sita au hata saba.

Kwa wanasiasa na Kisiasa ni rahisi kuamua hata muhula wa miaka mitatu. Lakini gaharama yao na fedha wanzotumia hao walistaafu ni kubwa sana. This should not be an option.

Kudeal na muhula ni kukwepa tatizo halisi. Jibu Ni kutafuta namna ya kumuwajibsha kiongozi mzembe . Atlest kuwe na option akiboronga hata baadhi ya stahiki zake zinafutwa. Si tunaona hata EL anaitwa mstaafu.. Wafanyaazi wa kawiada akifukuzwa hata NSSF wengine hawapati.........
 
Labda ni wakati wa kuwaleta maadui wengine karibu zaidi; maana kuna wengine wanapiga kelele sana nje ya serikali sasa njia nzuri ni kuwaleta ndani... Fikiria wizara ya madini wakimtoa Ngeleja na kumuingiza mkosoaji wake mkuu; Ngeleja akiwa Mbunge atampa sapoti au na yeye atajitahidi kumsabotage?
 
Back
Top Bottom