Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Tangu historia ya kale Visiwa vya Zanzibar zimeishi na kufanikiwa kwa kutegemea bara (eneo la mwambao wa Afrika ya Mashariki) na hata maeneo ya ndani ya Afrika. Kufanikiwa kokote kule kunakotajwa kuhusu Zanzibar kumetokana daima na mahusiano yake ya karibu na bara.
Bila Bara Zanzibar haiwezi kufanikiwa hata leo hii. Lakini zaidi mafanikio yake ya huko nyuma yalitokana sana na Zanzibar kuwa na ukuu wa kutawala maeneo ya bara. Haijawahi kufanikiwa bila kuwa na nguvu ya kiutawala au kisiasa huko bara.
Hili linaonekana hata leo hii katika MUungano wetu ambapo Zanzibar bado wanaonekana kuwa na maamuzi mengi kuhusiana na bara na wanafanikiwa zaidi kwa mgongo wa bara na sasa wapo wanaotaka izidi kufanikiwa kwa kile wanachokiita "kuondolewa kero za Muungano".
Hata Muungano ukivunjika bado Zanzibar itajikuta inaitegemea bara kwa namna nyingi zaidi - kiuchumi, ongezeko lake la watu, kiusalama n.k Hii ni kweli isiyopingika.
Kubali au kataa.
Bila Bara Zanzibar haiwezi kufanikiwa hata leo hii. Lakini zaidi mafanikio yake ya huko nyuma yalitokana sana na Zanzibar kuwa na ukuu wa kutawala maeneo ya bara. Haijawahi kufanikiwa bila kuwa na nguvu ya kiutawala au kisiasa huko bara.
Hili linaonekana hata leo hii katika MUungano wetu ambapo Zanzibar bado wanaonekana kuwa na maamuzi mengi kuhusiana na bara na wanafanikiwa zaidi kwa mgongo wa bara na sasa wapo wanaotaka izidi kufanikiwa kwa kile wanachokiita "kuondolewa kero za Muungano".
Hata Muungano ukivunjika bado Zanzibar itajikuta inaitegemea bara kwa namna nyingi zaidi - kiuchumi, ongezeko lake la watu, kiusalama n.k Hii ni kweli isiyopingika.
Kubali au kataa.