nitonye
JF-Expert Member
- Dec 18, 2011
- 7,273
- 3,750
Wana bodi,
Naomba tujadili suala hili maana limekuwa ni janga la kitaifa. Kuanzia kwa raisi hadi mwananchi wa kawaida ndani yaJF tulijadili kwa kina. Mods naomba usihamishe mada hii sababu ni suala la kisiasa zaidi.
Naomba tujadili suala hili maana limekuwa ni janga la kitaifa. Kuanzia kwa raisi hadi mwananchi wa kawaida ndani yaJF tulijadili kwa kina. Mods naomba usihamishe mada hii sababu ni suala la kisiasa zaidi.
Mosi ni uwekezaji kidogo katika sekta binafsi, ikumbukwe kwamba hii ndio sekta ambayo imekuwa ikitajwa kutoa nafasi kubwa ya ajira ukilinganisha na upande wa serikali.
Uwekezaji huu mdogo ni kutoka katika makampuni ya kigeni pamoja na ya kizalendo. Pili ni ukosefu wa mitaji watanzania walio wengi wanashindwa kujiajiri wenyewe kwa kushindwa kupata mikopo kutoka bank na mashirika mengine ya fedha kwa kukosa vigezo.
Chukulia kijana (wa maskini ambao ndio wengi) aliyehitimu chuo chochote hapa nchini anaambiwa ajiajiri mwenyewe, kijana huyu ataanzia wapi?! Ajabu watoto wa hao viongozi wanaohubiri vijana kujiajiri wao hawajajiajiri utawakuta bot na sehemu nyngne nzuri kama hizo.
Kwa kweli kilichobaki ni kupambana kwa namna yoyote inayofaa ili kujikwamua na hali hii kwani nchi ishauzwa, ukiisubiri serikali umri utakutupa mkono na hatimaye utakufa fukara