Sipingi na wala sitapinga wagonjwa kumiminika kwenda Loliondo kupata dawa ya magonjwa sugu inayotolewa na Mch. Mstaafu Ambilikile. Lakini kama anayosema ni kweli basi Mungu aliyempa uwezo huo atakuwa ni Mungu ambaye mm simuabudu. Tujiulize ni Mungu gani atampa mtu kuponya watu na kumzuia mtu huyo kuitoa dawa hiyo nje ya mazingira yale aliyopo? Mungu wa Mch. Mwasapile ni mchoyo kwa sababu kulazimisha dawa hiyo itolewe eneo moja tu ni uchoyo na upendeleo. Najiuliza wagonjwa mahututi walio kule Mtwara wataweza kusafiri mpaka Loliondo kupata hiyo dawa. Uchoyo mwingine wa Mungu wa Mwasapile ni kwamba kama dawa yake haiwezi kutolewa na mtu mwingine then Hospitali zetu za kule Songea haziwezi kunufaika nayo. Je mchungaji akipatwa na umauti sasa ni nani atatibu badala yake kama ni yeye tu anaruhusiwa na huyo Mungu wake kutibu? Bado Yesu alipewa uwezo wa kuponya lakini alikuwa anaweza kutoa uponyaji popote duniani? Nahitimisha kwa kusema Mch. Mwasapile ni mungu-mtu na anatumia matatizo ya binadamu vibaya na naapa kuwa Mungu wa Mchungaji huyu siwezi kumuabudu.
Na kuunga mkono.Mungu wa Mchungaji huyu sio Mungu wa Isaka na Yakobo,na yes,siwezi kumwabudu.And let me be straight,he is using demonic powers !