Mchungaji Mtikila ashinda kesi ya kumkashifu rais Kikwete

Kama kawa mh mtikila amemshinda dhaifu
hakuweza kukubabu sea! Au kukumwangosi!!!!
 
Duh sasa hii serikali niaje maana dowans wameshindwa,Mtikila kashinda,Nape atashindwa na kulipa fidia,Lema anashinda,Igunga Imeshindwa duh aibu iliyoje yaani unaumwa na mbwa wako mwenyewe
 
Kinachomfanya Mtikila kuishinda serikali kesi mbalimbali ni kutokana na serikali kukurupuka kumfungulia mashitaka bila kuwa na ushahidi wa kutosha,hii inaonesha wazi kuwa waendesha mashitaka wengi wa serikali hukurupuka katika kuwafungulia watu mashitaka.
 
mtikila.jpg
 
wenyewe wanasema hana madhara ndio maana huwa wanamwachia
Ni kigeugeu,wanajuwa hana madhara makubwa kwa serikali,lakini anayo madhara kwa upinzani kwasababu anatumika kuzigawa kura za upinzani na hatimaye ccm kushinda.Shida ni kwamba haaminiki huyu,na anapenda sana pesa kuliko hata hayo ya kuwakomboa watanzania,yeye anapiga kelele ili mkono uende kinywani,rejea ile issue ya RA,kule Mara kwenye uchaguzi wakati wa kifo cha Wangwe pamoja na ile kesi aliyoifunguwa eti amekamatwa makalio yake.Huyu ni pesa tu zinamzidia hata uzalendo.
 
...huyu jamaa ni kiboko ya serikali...profesa Paramagamba uko wapi baba hadi serikali inadhalilika mahakamani?...
 
mtikila huwa hawezi kuishi bila kuwa na kesi na serikali.

sasa hiv atalizua lingine ili wamfungulie kesi.

YY anaishi kwa fidia za kesi tu.
 
Mtikila is very daring. Lakini tatizo lake kubwa ni kula huku na kule. Ile ishu ya kuchukua hela kwa Rostam ilimweka pabaya sana kwenye jamii. Na hilo ni moja tu tunalojua, je yaliyojificha kuhusu activities za Mtikila?
 
Serikali haina jipya kesi nyingi inakurupuka na wataalam wa sheria wa serikali ni wanganga njaa hawanauwezo wamewekwa kindugu au hata kirafiki. Tusitegemee jipya kutoka kwa serikali iliojiishia kama mgonjwa wa HIV
 
Kweli Mtikila ni kiboko yao!
Big up Mtikila!

Mtikila was right!
 
andika zaid kama hivi watu wakaelewa:

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.

Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.

Akizungumza na mtandao huu baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema "Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu".




Yesu "alidesa" hiyo hukumu ? nyie watu mna utani mbaya !
 
huyu mtikila ni jembe lakini nashindwa kuelewa ni kwa nini inakuwa ngumu sana kumwingiza kwenye mapambanao na makamanda wenzake,jamaa anafaa sana kutetea anachokiamini,wapi Kayinga msaidizi wake,nakumbuka enzi zile alikuwa mchungaji pale shule ya uhuru Kayinga alikuwa habanduki ubavuni mwake


Huyu jamaa is a GREAT HERO! Tatizo lake ni kuamini kuwa vita ya ukombozi wa taifa hili anaweza kupigana pekeake. Angeweza kuungana na wenzie angefanya kazi nzuri zaidi!
 
Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imesema Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Part(DP), Mchungaji Christopher Mtikila ana kesi ya kujibu katika kesi ya kuchapisha na kuusambaza waraka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete.


Uamuzi huo ulitolewa na Hakimu Mkazi Sundi Fimbo ikiwa ni siku chache baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wake baada ya kuwaleta mashahidi watano kutoa ushahidi wao.

Hakimu Fimbo alisema baada ya kupitia ushahidi wa upande wa Jamhuri,amefikia uamuzi wa kumuona Mtikila ana kesi ya kujibu na kwamba maana hiyo Mtikila atatakiwa na mahakaa hiyo kupanda kizimbani Aprili 11 mwaka huu kwaajili ya kuanza kujitetea.


Baada ya Hakimu Fimbo kutoa uamuzi huo, Mtikila alidai kuwa anatarajia kuleta mashahidi 10.

Februali mwaka huu, Mtikila alikiri maelezo aliyochukuliwa na afisa wa polisi ni yake na kwamba hana pingamizi nayo na hivyo mahakama iliyapokea kama kielezo cha upande wa jamhuri.Mtikila katika maelezo hayo ya onyo alikiri kuwa ni kweli aliuandaa waraka huo na kuusambaza ila akakanusha waraka huo si wa uchochezi ila unahusu maneno ya mungu.

Mtikila alikiri maelezo hayo yaliyosomwa na kutolewa mahakamani kama kielelezo baada ya shahidi wa Jamhuri, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Ibeleze Mrema (54) kudai kwamba Aprili 15, mwaka 2010 akiwa kituo cha polisi kikuu jijini Dar es Salaam, aliitwa na mkuu wake wa kazi na kumpa kazi ya kumhoji Mtikila kuhusu tuhuma za kukutwa na waraka wa uchochezi.

Alidai kuwa wakati akimhoji mtuhumiwa huyo alikiri kuhusika na nyaraka hizo na kwamba alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya kuokoa wakristo na alisaini yeye waraka huo.

“Mtikila alikiri kuhusika kuandaa waraka huo kama mwenyekiti alisaini kwa niaba ya wengine … nilipomhji walichapisha wapi mtikila hakupenda kusema bali alidai kuwa zilikuwa nyaraka 100,000 ambazo zilisema kwamba Rais Kikwete anaangamiza ukristo na amekuwa jasiri kuingiza uislamu katika katiba ya Jamhuri” alidai Mrema kupitia maelezo hayo yaliyotolewa na Mtikila.


Mrema aliendelea kudai kupitia maelezo hayo kwamba, Mtikila alikuwa anahamasisha wakristo wajitoe mhanga kukomesha ugaidi na wamuweke rais mkristo Ikulu.

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari mwaka 2009 na Aprili 17, mwaka 2010 jijini Dar es Salaam, kwa nia ya uchochezi mshitakiwa alisambaza kwa umma nyaraka zilizosema 'Kikwete kuuangamiza ukristo', 'wakristo waungane kuweka mtu Ikulu' alinukuliwa Mtikila.

Katika shitaka la pili, Aprili 16, mwaka 2010 eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam, bila kibali alikutwa akimiliki waraka wenye uchochezi kwa jamii.Na katika kesi hii Mtikila hana wakili wa kumtetea na anajitetea mwenyewe.
 
Back
Top Bottom