Mchungaji KKKT jela kwa rushwa ya ngono

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Mchungaji KKKT jela kwa rushwa ya ngono
Na Eliasa Ally, Iringa

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, imemhukumu kifugo cha miaka mitano Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Michael Ngilangwa, baada ya
kupatikana na hatia ya kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi ili amsaidia masomo.

Mchungaji Ngilangwa alikuwa mwalimu wa sekondari ya Pomerini iliyopo wilaya ya Kilolo.

Akitoa hukumu hiyo mjini hapa jana, Hakimu wa Mkazi wa Mahakama Iringa, Bi, Martha Mpaze, alisema mshitakiwa wakati wote wa kesi hakuwa na shahidi, ambapo alijitetea mwenyewe.

Upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi watano. Alisema mshitakiwa katika utetezi wake, alisema kesi hiyo ni ya kubambikizwa kosa hilo kutokana na wivu uliokuwepo kati yake na baadhi ya walimu wa sekondari ya Pomerini kumfanyia.

Alidai walimu hao walifanyia fitina baada ya kuteuliwa kuwa Makamu wa Mkuu wa Shule Pomerini, hatua iliyomwongezea maadui ambao walikuwawakimfanyia fitina na kuandaa mazingira ya mtego ili ili akamatwe na mwanafunzi.

Alisema katika utetezi wake, Mchungaji Ngilangwa alidai baada ya kushika wadhifa huo wazazi wengi walikuwa wakimpelekea matatizo ya watoto wao, akiwemo mzazi wa mwanafuzni aliyemshitaki kwa madai ya kumuomba rushwa ya ngono.

Alisema siku ya tukio mshtakiwa aliyokamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) alipigiwa simu na mama wa mwanafunzi huyo kuwa wanatoka Dar es Salaam hivyo aliomba awatafutie vyumba katika nyumba za kulala wageni.

Katika utetezi wake alidai kwamba alikwenda nyumba ya wageni na kuchukua vyumba viwili kimoja cha kulala watu wawili.

Alidai kwa kuwa ulikuwa ni usiku, alichukua chumba namba 4 kwa ajili yake.

Bi. Mpaze alisema mshtakiwa anaonekana kuwa na makosa kwa kuwa katika kitabu cha wageni alijaza kuwa anatoka Njombe kwenda Iringa wakati siyo kweli.

Alisema ukweli ni kuwa mshtakiwa alikuwa anatoka Pomerini kwenda Iringa mjini.

Alisema kuwa ushihidi mwingine ambao unamtia hatiani Mchungaji Ngilangwa ni ule wa TAKUKURU kumkuta na vidonge vya kuzuia mimba, ambavyo alimpatia mwanafunzi wake ameze kwa kuwa wangefanya ngono bila kutumia kondomu.

Hakimu huyo alisema ushahidi mwingine ni ule wa ujumbe ambao TAKUKURU ilinasa sauti walipokuwa wakiongea na mwanafunzi wake.

Hakimu huyo alikuwa akimwambia mwanafunzi huyo aende chumba namba nne ndiko wangelala.

"Mshtakiwa anatiwa hatiani kwa ushahidi mwingine ambapo TAKUKURU ilimkuta akiwa na mwanafunzi wake huyo saa 5:00 usiku wakati sheria ya nyumba hiyo ya kulala wageni walipokutwa inakataza watu wasio wanandoa kulala chumba kimoja.

Hakimu huyo alisema kama TAKUKURU wasingewahi mwanafunzi huyo angebakwa na azma yake ya kuomba rushwa ya ngono ingetimia.

Mshtakiwa huyo alipotakiwa kujitetea aliomba mahakama imfikirie kwa kuwa ana watoto wanne wanaomtegemea, wawili wanasoma sekondari na wengine shule ya msingi.

Mchungaji Ngilangwa aliongeza kuwa mzazi wake ni mzee wa miaka 82, hivyo hana mtu wa kumtunza.

Akitoa hukumu Hakimu Bi. Mpaze, alisema mahakama imezingatia kuwa mkosaji wa mara ya kwanza lakini akahukumiwa adhabu wa miaka mitano jela.

Katika kesi ya pili ya kuomba rushwa ya ngono mshtakiwa atatakiwa kulipa faini ya sh. 500,000 au endapo atashindwa atatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela.
 
Duu, mchungaji alitaka kutoa upako.
Pole mchungaji, hiyo ni ajali kazini. naihurumia familia yako.
 
Mchungaji KKKT jela kwa rushwa ya ngono
Na Eliasa Ally, Iringa

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, imemhukumu kifugo cha miaka mitano Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Michael Ngilangwa, baada ya
kupatikana na hatia ya kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi ili amsaidia masomo.

Mchungaji Ngilangwa alikuwa mwalimu wa sekondari ya Pomerini iliyopo wilaya ya Kilolo.

Akitoa hukumu hiyo mjini hapa jana, Hakimu wa Mkazi wa Mahakama Iringa, Bi, Martha Mpaze, alisema mshitakiwa wakati wote wa kesi hakuwa na shahidi, ambapo alijitetea mwenyewe.

Upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi watano. Alisema mshitakiwa katika utetezi wake, alisema kesi hiyo ni ya kubambikizwa kosa hilo kutokana na wivu uliokuwepo kati yake na baadhi ya walimu wa sekondari ya Pomerini kumfanyia.

Alidai walimu hao walifanyia fitina baada ya kuteuliwa kuwa Makamu wa Mkuu wa Shule Pomerini, hatua iliyomwongezea maadui ambao walikuwawakimfanyia fitina na kuandaa mazingira ya mtego ili ili akamatwe na mwanafunzi.

Alisema katika utetezi wake, Mchungaji Ngilangwa alidai baada ya kushika wadhifa huo wazazi wengi walikuwa wakimpelekea matatizo ya watoto wao, akiwemo mzazi wa mwanafuzni aliyemshitaki kwa madai ya kumuomba rushwa ya ngono.

Alisema siku ya tukio mshtakiwa aliyokamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) alipigiwa simu na mama wa mwanafunzi huyo kuwa wanatoka Dar es Salaam hivyo aliomba awatafutie vyumba katika nyumba za kulala wageni.

Katika utetezi wake alidai kwamba alikwenda nyumba ya wageni na kuchukua vyumba viwili kimoja cha kulala watu wawili.

Alidai kwa kuwa ulikuwa ni usiku, alichukua chumba namba 4 kwa ajili yake.

Bi. Mpaze alisema mshtakiwa anaonekana kuwa na makosa kwa kuwa katika kitabu cha wageni alijaza kuwa anatoka Njombe kwenda Iringa wakati siyo kweli.

Alisema ukweli ni kuwa mshtakiwa alikuwa anatoka Pomerini kwenda Iringa mjini.

Alisema kuwa ushihidi mwingine ambao unamtia hatiani Mchungaji Ngilangwa ni ule wa TAKUKURU kumkuta na vidonge vya kuzuia mimba, ambavyo alimpatia mwanafunzi wake ameze kwa kuwa wangefanya ngono bila kutumia kondomu.

Hakimu huyo alisema ushahidi mwingine ni ule wa ujumbe ambao TAKUKURU ilinasa sauti walipokuwa wakiongea na mwanafunzi wake.

Hakimu huyo alikuwa akimwambia mwanafunzi huyo aende chumba namba nne ndiko wangelala.

"Mshtakiwa anatiwa hatiani kwa ushahidi mwingine ambapo TAKUKURU ilimkuta akiwa na mwanafunzi wake huyo saa 5:00 usiku wakati sheria ya nyumba hiyo ya kulala wageni walipokutwa inakataza watu wasio wanandoa kulala chumba kimoja.

Hakimu huyo alisema kama TAKUKURU wasingewahi mwanafunzi huyo angebakwa na azma yake ya kuomba rushwa ya ngono ingetimia.

Mshtakiwa huyo alipotakiwa kujitetea aliomba mahakama imfikirie kwa kuwa ana watoto wanne wanaomtegemea, wawili wanasoma sekondari na wengine shule ya msingi.

Mchungaji Ngilangwa aliongeza kuwa mzazi wake ni mzee wa miaka 82, hivyo hana mtu wa kumtunza.

Akitoa hukumu Hakimu Bi. Mpaze, alisema mahakama imezingatia kuwa mkosaji wa mara ya kwanza lakini akahukumiwa adhabu wa miaka mitano jela.

Katika kesi ya pili ya kuomba rushwa ya ngono mshtakiwa atatakiwa kulipa faini ya sh. 500,000 au endapo atashindwa atatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela.

acha kututoa kwenye reli ww habari ya miaka ya 2011 ndo unatuletea hapa
 
Back
Top Bottom