mchungaji naye huyo yupo kwenye system! kesho mtasikia majibu yake! kama kova tu,sema yeye ataanzia mwisho kuja mwanzoni!:spy:
mkuu inategemeana na mazingira ya tukio lenyewe,kova alisema jamaa alikutwa kanisani,kwaniyo kanisa nayo inaplay part yakeSasa jamani,tangu lini taarifa za kiintelijensia zikatolewa kanisani?
na wewe unaenda kusali au kutafuta habari?
..Ukitulia na kufikiria kwa undani sana unaweza kuona hii picha kwamba imetengenezwa kati ya polisi na huyo mchungaji. Subirini mtaona
Kova amejichanganya sehemu mbaya .....atajuta kulihusisha hili kanisa la gwajima..tutegemee makubwa kesho...
Baada ya kufanya bidii za maksudi kutaka kujua sakata hili la shambulizi la Mwenyekiti Wa Jumuia ya Madaktari TZ, Dr. Steve Ulimboka pamoja Na madai yaliyotolewa Jana Na Kamanda Kova kwamba Kuna Mtu anaedaiwa kuhusika Na utekaji Na shambulizi Hilo aliyejitokeza kujisalimisha ndani ya Kanisa linaloongozwa Mch Josephat Gwajima, pamoja Na utata uliosambaa juu ya matamshi hayo, nimebahatika hatimae kuongea na Mchungaji huyo..
Yeye mwenyewe Kwanza amekiri kusikia taarifa hizo Na pia maelfu ya watu miongoni mwao ni washirika NOa watu wengine nje ya Kanisa nao wamekuwa wakimtafuta ili kupata ukweli Wa matamshi hayo ya Polisi
Mchungaji huyo ambaye Kwa mtazamo ni mpole, mkimya Na mwenye maneno yaliyonyooka, akasema kwamba kuna taarifa aliletewa Na walinzi wa Kanisa kwamba kuna kijana mdogo tu alikuwa akidai yeye ndiye Kinara wa sakata Hilo la kumteka daktari huyo..Na walinzi Hao wakampeleka kituoni Na kumkabidhi huko.. Sasa cha Ajabu ni taarifa ya Jana ya jeshi la polisi juu ya uhusika wa tukio Hili..
Na yeye Kama kiongozi imemgharimu kuwaita Upya wale walinzi Na kupata kutoka kwao taarifa hiyo Na hatimae kesho kwenye Ibaada maalum ataelezea Mkasa wote ulivyokuwa ili jamii ielewe nini kilichojiri..
Nimepitia comment nyingi za watu humu kila Mtu akinadi Na kusema lake, wapo wanaotukana Na wapo wanalalamika Kwa namna wajuao.. Labda nitoe rai kwamba ni vema tuwe Na subira Na kupata Picha kamili hiyo kesho..
Mimi mwenyewe nitawahi mapema Na Kama kawaida ya TAMKO nitawajuza kila kitu..matusi kejeli si mahali pake nadhani kuna kamchezo kanaendelea ambako lazima kafichuliwe sasa.. Jambo Hili si Dogo linagusa masikio ya mataifa mengi Kwa sasa..
..
FJM , usiwe mwepesi Wa kuongea, sidhani Kama kuna Mtu ana lazimishwa kutoa Sadaka
Huyo mchungaji anataka sadaka kubwa kesho.
Mtazamo wangu unafanana na wako. Na taarifa kawapa mapemaaa-Kesho! Wahi Upate Story Live; Usisubiri kusoma katika magazeti ya udaku!
..We ndo gwajima?
Kova amejichanganya sehemu mbaya .....atajuta kulihusisha hili kanisa la gwajima..tutegemee makubwa kesho...
..
Ha ha Haa.. Haya bwana mkulu, ila Kwa Jinsi Bukoba ilivyo Na wasomi wengi waliotulia sidhani Kama mbichwa huu unatokea pande hiyo.. Nakwambia kesho ntakuwa hapo live nikikujuza kila kinachoendelea halafu wewe unasema mimi ndiye yeye.. Sasa yeye atakujuza vipi Na hapo hapo anaongea.. Vichwa vingine BWANA havipendi kabisa kufikiri