Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,444
UONGOZI wa Kanisa la Evangelistic Assembles Of God Tanzania Jimbo la Dodoma, limemsimamisha na kumfutia leseni ya huduma ya kiroho nchini mchungaji wake kutokana na kupatikana na hatia ya uzinzi.
Uamuzi huo umetokana na mchungaji huyo kukutwa akifanya tendo la ndoa katika nyumba ya wageni iliyopo mjini hapa.
Akitangaza kumfukuza na kumzuilia huduma mchungaji huyo, Askofu wa Jimbo la Dodoma, Jackson Madelemo, alisema kanisa kupitia uongozi wa ngazi ya jimbo umeamua kumsimamisha na kumfukuza kutokana na tabia hiyo ambayo haiendani na huduma ya kiroho.
Askofu Madelemo alisema kitendo cha mchungaji huyo kimeliaibisha kanisa na kwamba hawezi kuendelea na kazi ya kumtumikia Mungu.
Akitoa taarifa ya mwenendo wa mchungaji wa kanisa hilo mbele ya waumini waliohudhuria ibada, Askofu Madelemo alisema mchungaji huyo amekuwa akituhumiwa kwa makosa mengi ya uzinzi, lakini kwa kuwa uongozi wa jimbo haukuwa na ushahidi ulijaribu kufumbia macho huku akiitwa katika vikao vya mara kwa mara.
Sisi kama viongozi wa kiroho tulijitahidi kuhakikisha tunamweka chini mchungaji wetu ili aweze kufanya kazi ya Mungu kwa uaminifu na kumsihi kuachana na tamaa za mwili, lakini dhambi hiyo imeendelea kumtafuna mpaka leo hii tunapochukua hatua ya kumfutia huduma yake, alisema.
Source: Tanzania Daima
Uamuzi huo umetokana na mchungaji huyo kukutwa akifanya tendo la ndoa katika nyumba ya wageni iliyopo mjini hapa.
Akitangaza kumfukuza na kumzuilia huduma mchungaji huyo, Askofu wa Jimbo la Dodoma, Jackson Madelemo, alisema kanisa kupitia uongozi wa ngazi ya jimbo umeamua kumsimamisha na kumfukuza kutokana na tabia hiyo ambayo haiendani na huduma ya kiroho.
Askofu Madelemo alisema kitendo cha mchungaji huyo kimeliaibisha kanisa na kwamba hawezi kuendelea na kazi ya kumtumikia Mungu.
Akitoa taarifa ya mwenendo wa mchungaji wa kanisa hilo mbele ya waumini waliohudhuria ibada, Askofu Madelemo alisema mchungaji huyo amekuwa akituhumiwa kwa makosa mengi ya uzinzi, lakini kwa kuwa uongozi wa jimbo haukuwa na ushahidi ulijaribu kufumbia macho huku akiitwa katika vikao vya mara kwa mara.
Sisi kama viongozi wa kiroho tulijitahidi kuhakikisha tunamweka chini mchungaji wetu ili aweze kufanya kazi ya Mungu kwa uaminifu na kumsihi kuachana na tamaa za mwili, lakini dhambi hiyo imeendelea kumtafuna mpaka leo hii tunapochukua hatua ya kumfutia huduma yake, alisema.
Source: Tanzania Daima