kaa naye mwambie mwanzo hadi mwisho ajue wajibu wake ikiwezekana wasiliana na mama yake amkalishe chini amwonye au amfunde asijekuwa mzigo kwa baadaye ndo hawa ambao huwaachia wasichana wa kazi kufua hadi nguo za ndani pole kaka yangu mi na ushahidi wa watu ambao mpaka anaingia chuo hajui kupika wengine wako rafu wavivu hadi nashangaa nasema wanaume wa na kazi kwa kuchagua wa chumba ndo hivyo usione ua lachanua kwa nje tu hasa wakina dada wa leo tena wale waliosoma ndo balaa wavivu hakuna. jamani wadada hawa wanakera tena sana
Hakuna kitu kilichonifurahisha kama self analysis yako na kukubali mapungufu.
You are one step ahead, ninakushauri kaa mjadili bila kutumia ukali; make her reason with you na especially hiyo ya kula junk food. Lakini kama wote ni wafanyakazi, mnaweza kuhire a help, mtu akawa anakuja anafanya usafi na kufua at least 4 times a week, huku mkijipanga jinsi ya kujitegemea.
Nina uhakika sababu ya kumpenda ni zaidi ya kuwa mfanyakazi wa nyumbani; hivyo basi, hizo shughuli mjadiliane zitafanyika vipi coz lazima zifanyike; mwambie aje na suggestion.
kaunga hata kama wakiajili majukumu ya mwanamke ndani ya nyumba lazima ayatimize yani hata kufua nguo za mmewe waajili mtu! msaidizi anakuwepo na uwajibikaji nao unakuwepo ndo maana muda mwingine tunalaumu wanaume kwa kuwa na nyumba ndogo kama masuala yenyewe ndo haya hebu imagine ndo wamepata mgeni ataenda kununua chips.yeye akae naye ampe makavu laivu bila chenga kwa kweli namchukia mwanamke mvivu ukute hata kupika hajui
The secretary mi hapo sioni matumaini ya mtu kubadilika. Unadhani mama yake alomlea toka utotoni na hakumfundisha kuwa msafi na mchapakazi; ataweza leo hii kumpa crash program eti kisa kapata mchumba. Hao wazazi wamemlea hivyo alivyo na kuna possibilty kubwa hawaoni hizo kasoro anazolalamikia jamaa. Si unajua like mother like daughter.
yaelekea wewe ni msafi kupitiliza na kwa mimi wanaume wa jinsi hiyo huwa ni wasumbufu sana kwa wapenzi wao ama inawezekana wewe ni bahili sana sasa kutaka mkale chips anakukomoa tu, jirekebishe upande wako halafu na yeye mueleze ukweli lakini pia usifanye haraka kutangaza ndoa. mpaka sasa naamini hamuendani!
Kichwa kinauma.
Sioni tatizo hapo mkuu, sio lazima mwanamke ajue kufanya yote hayo siku hizi ndio maana kuna 1.kusaidiana 2.housegirl na boy, 3.mighahawa, 4.dobi nk nk. hauko pekeyako hebu tafuta kitabu cha James Hadley Chase "Believe this, you will believe anything" kuna dada anatwa Rhoda hebu kisome hicho
Maoni yenu ninayafanyia kazi. Nitakaa nae chini kwa upole na kwa lolote nitaleta kilichojiri mnipe ushauri zaidi. I'm so confused.
yaelekea wewe ni msafi kupitiliza na kwa mimi wanaume wa jinsi hiyo huwa ni wasumbufu sana kwa wapenzi wao ama inawezekana wewe ni bahili sana sasa kutaka mkale chips anakukomoa tu, jirekebishe upande wako halafu na yeye mueleze ukweli lakini pia usifanye haraka kutangaza ndoa. mpaka sasa naamini hamuendani!
hivi upo serious na ukisemacho? kama hakuna haja ya mwanamke kujua hayo yote kwani huyu housegirl yeye si mwanamke .kwa hiyo dobi ndo atamfulia hadi nguo za ndani? hawa wasaidizi ndo wamfanyie usafi hadi ndani binafsi mi hata kufuliwa nguo zangu na mtu yoyote haiwezekani labda kama ni mgonjwa hata mafundisho ya dini yanakemea uchafu na uvivu na kuonyesha wajibu wa mke katika familia
unajua shida ya kuishi na jitu lenye maneno ya kejeli wewe? Mbona mwenzio anakuvumilia na udhaifu wako?
Ukitaka mwanamke/mwanaume perfect muumbe wa kwako, la sivyo maisha ni kuvumiliana.....
Kuhusu kufua simple si wote mna kazi changeni laki nane nane mmnunue mashine ya kufulia....
Zungumza nae kuhusu kupika (ila mmmh huyo nae uvivu kapitiliza hata kupika??????) je anarudi amechoka sana?
Kama kuna wanawake watu wazima kwao zungumza nao, waketi nae na kumfundisha majukumu ya mke kwenye nyumba.....
Na kama mna uwezo wekeni house girl, maana kumbuka wewe unafanya kazi yeye anafanya kazi, mkirudi ofisini wewe unachukua remoti na yeyeaingie jikoni kupika, aoshe vyombo, asafishe nyumba, uwanja, apige pasi mwisho ya siku atachoka ashindwe kukupa unyumba urudi hapa na thread mpya......
Swali la nyongeza, mnaporudi ofisini unamsaidia kazi? Au wewe miguu juu mwenzio ahenyeke?
mkuu, watu wote hawapo sawa! sasa unataka kuniambia asiyejua kupika au kufua haolewi? halafu nani amuoe? we mwenyewe ushasema unadharau, hasira nk nk... unadhani nani anapenda kuolewa na mtu mwenye tabia kama zako??? Hapo hamna cha dini wala nini, ingekua unafuata dini basi wewe unatakiwa kula kwa jasho na yeye atulie nyumbani kukufulia nyumba kubwa , Blaki Womani
Maoni yenu ninayafanyia kazi. Nitakaa nae chini kwa upole na kwa lolote nitaleta kilichojiri mnipe ushauri zaidi. I'm so confused.