Mchezo wa Kiduku Unavyowadhalilisha Wanaume

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
Mchezo wa Kiduku Unavyowadhalilisha Wanaume
4385238.jpg

Mtoto wa kiume akiwa amevaa kanga akikata mauno katika mashindano ya KIDUKU yaliyohudhuriwa na mamia ya watu Friday, April 23, 2010 12:14 AM
Fainali ya mashindano ya kucheza mtindo wa taarabu unaoitwa KIDUKU ambao vijana wa kiume huvaa nguo za kike na kukata mauno kama wanawake itafanyika mwanzoni mwa mwezi ujao huku shutuma kali zikiwaendea waandaaji wa mashindano hayo kuwa wana malengo ya kuwaharibu watoto wa kiume. Mtindo wa KIDUKU uliobuniwa na mtangazaji mahiri aliyekuwa akitangaza
katika kituo cha televisheni ya Afrika Mashariki EATV, Maimartha wa Jesse umekuwa gumuzo katika jiji la Dar es Salaam, kutokana na jinsi mchezo huo ulivyo wahusisha vijana wenye umri chini ya miaka 18.

Wengi wa vijana huwa ni watoto wa shule za msingi na sekondari wengine wakitokea tu mitaani kushindana kucheza mchezo wa Kiduku.

Hivi karibuni Maimartha aliandaa shindano la kumtafuta bingwa wa kiduku mwaka 2010 ambalo limewashirikisha vijana toka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

Miongoni mwa vikundi vinavyoshiriki ni Vidoleki, Mazombi, Wanaume fasti, Wakali wa kitengo, Wakupoteza, Stavanga na Mazombi.

Katika shindano hilo mshindi wa kwanza atapata zawadi ya dola 250, mshindi wa pili atapata music system na watatu ataambulia feni. Fainali ya mashindano hayo itafanyika Mei 2 mwaka huu katika ukumbi wa Travertine uliopo magomeni.

Hata hivyo shindano hilo wengi wamelibeza kutokana na kuonekana linawadhalilisha watoto wa kiume hasa hasa wanafunzi ambao huingia kushindana wakiwa wamevalia sare za shule.

Kwa upande mwingine wapenzi wa muziki wa taarab wamekuwa na maoni tofauti kutokana na vijana hao kucheza huku wakiwa wamevalia nguo za akina dada jambo ambalo wengi wanalihisi kuwa linaweza likawa ni njia mojawapo ya kuwapotosha vijana hao kwa kujiingiza katika njia ya uasherati ikiwa ni pamoja na kuwa mashoga.

Mmoja wa wazee aliyehudhuria katika mojawapo ya mashindano haya [Jina Kapuni] alisema kuwa wizara ya utamaduni, burudani na michezo inapaswa kuangalia na kupitia baadhi ya mashindano kama haya.

"Mashindano haya yalipaswa yawahusishe wanawake na si watoto, lingine angalia ndugu mwandishi vijana wanakesha hapa na wanakuja na sare za shule zao inamaana wakitoka hapa wanaunganisha kwenda shule je watasoma nini huku wakiwa na usingizi?", aliuliza mzee huyo.

Wadadisi wa mambo wameomba mchezo wa Kiduku usiwahusishe watoto wa kiume la sivyo vijana hao watakuwa mashoga kwani sehemu kama hizo huhudhuriwa na mashoga ambao wamekuwa wakiwarubuni vijana hao kwa vijisenti vidogo pia sehemu kama hizo ndizo zenya makuadi wa kutafuta vijana wanaotaka kwenda na wakati kwa kufanya mapenzi kinyume na maaumbile yao.

Mei 2 mwaka huu ndio fainali ya kumpata bingwa wa kucheza KIDUKU.
 
kwani sheria za tanzania zinasemaje? mtoto wa chini ya miaka 20 si haruhusiwi kuingia club? (au huo umekuwa categorized kuwa ni ukumbi?)

wanawake watu wazima walojaa ambao wako ready kufanya chochote unashindwa kuwahusisha na upuuzi huo unaenda kutafuta watoto? wanaume? umekusudia kuwafunza nini?
 
Sheria za Tanzania haziruhusu mtu akatazwe kufanya usanii ilimradi havunji sheria zilizopo. Huo ni usanii kuburudisha watu na kujiongezea kipato. Maimatha anastahili pongezi kwa ubunifu wake. Kila kitu kikitumiwa vibaya hudhalilisha, lakini kikitumiwa vema huleta heshima. Kuwowa sio kitu kibaya, lakini ukiwowa hadharani unajidhalilisha na unaidhalilisha jamii. Hao vijana walaa!
 
kubinika ungefurahi mwanao wa kiume kwenda kucheza kiduku kwa kugombea dola 250?

tanzania we have a long long way to go
 
Jamii isiojali utu utaijua tuu..Ukiangalia larger picture utabaini tatizo lipo hasa kwenye jamii yenyewe kutaka mambo marahisi na shortcut ya kupata fedha za haraka haraka, in the process bila kujali kaa jamii inafaidika au la, na fmatendo yetu ya leo yata-affect vipi future yetu na vizazi vyetu. Na viongozi wetu ilimradi kitu hakiwagusi matumbo yao they will allow everthing else regardlessly..Hii ndio anarchy society.
 
Mi sioni tatizo lolote wacha watu wabuni mbinu za kupata kipato,labda hao watoto wa shule wanatakiwa waondolewe ila kwa upande mwingine hakuna tatizo
 
Jamii isiojali utu utaijua tuu..Ukiangalia larger picture utabaini tatizo lipo hasa kwenye jamii yenyewe kutaka mambo marahisi na shortcut ya kupata fedha za haraka haraka, in the process bila kujali kaa jamii inafaidika au la, na fmatendo yetu ya leo yata-affect vipi future yetu na vizazi vyetu. Na viongozi wetu ilimradi kitu hakiwagusi matumbo yao they will allow everthing else regardlessly..Hii ndio anarchy society.
angalia avatar yako mkuu naamini umejiongelea na wete pia
 
Jamii isiojali utu utaijua tuu..Ukiangalia larger picture utabaini tatizo lipo hasa kwenye jamii yenyewe kutaka mambo marahisi na shortcut ya kupata fedha za haraka haraka, in the process bila kujali kaa jamii inafaidika au la, na fmatendo yetu ya leo yata-affect vipi future yetu na vizazi vyetu. Na viongozi wetu ilimradi kitu hakiwagusi matumbo yao they will allow everthing else regardlessly..Hii ndio anarchy society.

Thumbs up....
:A S thumbs_up:


WTF is this? watu wameshidwa kutumia brain and show us some creativeness? This should be banned, ppl shouldnt entertain this..
 
nimeachana na hayo mambo........mimi ni janadume la haja
sherehe kubwa inafanyika mbinguni, malaika kwa furaha wanaimba wakisema 'aliyepotea tazama ameonekana,mwana mpotevu ameiona njia na kurudi nyumbani kwa baba yake'
hureeeeee!
 
ugumu wa maisha ndio unasababisha yote hayo.

kupenda reeereeeee

maisha yalikuwa na yataendelea kuwa magumu kwa hiyo tu-justfy tu upuuzi kwa kisingizio maisha magumu.

kupenda mteremko ndo shida yetu (just like DECI n the like)

Mai unachokifanya haipendezi wala kustahili sifa............ni vile tu huna uchungu na hao vijana...

u are as selfish as most of us!!!
 
haya mashindano hayakubaliki kabisaa!inasikitisha,wanatuharibia ndugu zetu,ndio nini hiyo eti watoto wakiume wavae mavazi ya kike wakate viuno,no way labda maimartha aseme mabasha wamemuomba awaandalie hili shindano!hayafai yanatakiwa yapingwe vikali!
 
Back
Top Bottom