mchezaji wa yanga ajenga hotel ya kitalii

Ingekuwa bora kama angejenga hiyo hoteli Mwananyamala au angekarabati jengo la klabu jangwani ili kuepusha wachezaji kulala mzungu foo.

Mchezaji wa Yanga ya Dsm anajenga Kinshasa? Ova My Dedi Bode....
Kuna jamaa hapa ananiambia ile staili ya Yanga inaitwa "European Four". Labda wakienda mikoani tena watakuwa wanalala Kongo ili kuepuka "European Four" na kuogea kopo la kunywea mbege.
 
Kwa hadhi yake na timu alizochezea sikutarajia angezindua hotel hii ya kawaida kabisa ambayo wkinga wengi wanajenga hapo Dar..
 
Umeandaa habari nzuri ila umeshindwa kujieleza Nonda si mchezaji wa Yanga ila aliwahi kuichezea Yanga acha upenzi wa kijinga huna jipya
Mkuu umemuonea bure kwani Malimbukeni wanajua kujieleza. Kwa hilo naomba niwasaidie watani zangu.
 
Kwa hadhi yake na timu alizochezea sikutarajia angezindua hotel hii ya kawaida kabisa ambayo wkinga wengi wanajenga hapo Dar..
Kwao Yanga hiyo ni 5 star hotel, kama waliweza kuishi kwenye lile bonge la hoteli kule Mbeya watashindwa hicho kibiriti ambacho watanzania kibao wanaviangusha kila kukicha.
Waende Mwenge - Bamaga wakaone dada yetu wa kitanzania alichofanya sio hicho kibanda.
 
Hayo pekee ndiyo mafanikio ambayo watani zetu mnapaswa kujivunia lakini soka hakuna kajipangeni upya, lakini hapo si alifanya kupita tu hata uraia ni wa Kongo vipi kama angekuwa mbongo aliyelelewa na kuuzwa na Yanga kama ambavyo Simba wamefanya kwa akina Samata Magoli, Ulimwengu Tom na wengine wengi wanaoitikisa Dunia mngefanyaje?

Another version of ulimbukeni's revealed..

hapo kwa ulimwengu labda mi mgeni bongo hivi ashacheza simba nae?
 
Baada ya kuwatenda vibaya kwa Five O'clock na kuwastaafishia Fuso lenu kwa aibu, kila siku Okwi yupo vichwani mwenu, kwa taarifa yenu hatumuuzi kwa vihela uchwara kama nyinyi mpo tayari kutoa wachezaji wenu hata bure tena hata kwa kuwatoroka kwenda South Afrika halafu mnajisifu mmechina.
Kama angekuwa wa kwenu angekarabati hata lile bwawa la Kambare pale kaunda. El-nino inakuja tutaokota mpaka Sangara pale.

huyu okwi hivi mmeloga apa bongo make hata uganda anasugua benchi, ebu nipe jibu basi ilikuaje amekosa soko huyu mchezajo bora kadolora kabaki kutia huruma tu, ameshindwa kupata timu india ebu jibu wacha jazba
 
huyu okwi hivi mmeloga apa bongo make hata uganda anasugua benchi, ebu nipe jibu basi ilikuaje amekosa soko huyu mchezajo bora kadolora kabaki kutia huruma tu, ameshindwa kupata timu india ebu jibu wacha jazba
Nafikiri jibu zuri umeshapewa, wewe ndiyo hujatuambia ukarabati wa lile bwawa la kambare na sangara pale kaunda unaanza lini, el-nino inakuja
 
Nonda shabani "Papii" si jina geni kwa wapenzi wa soka wa bongo,huyu ni mchezaji wa zamani wa yanga ya dar es salaam ambae ameonyesha mfano wa kuigwa kwa wachezaji wetu wa bongo kutokana na mafanikio yake ya kisoka na maisha kiujumla.Nonda amezindua hotel yake ya kitalii hivi karibuni hapa kinshasa aliyoipa jina "VILLA FATUMA" uzinduzi uliohudhuriwa na watu wengi maarufu congo akiwemo mwanamuziki wa zamani wa bendi ya wenge musica ADOLPHE DOMINGUEZ.Gonga hapo chini utizame video ya uzinduzi wa hoteli hiyo ya kisasa na nzuri kuliko club za simba na yanga!



nilijua mbuyu tuite facebook... kumbe the don..
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri jibu zuri umeshapewa, wewe ndiyo hujatuambia ukarabati wa lile bwawa la kambare na sangara pale kaunda unaanza lini, el-nino inakuja

jibu bado sjapewa kua kwanini okwi kashindwa sajiliwa hata india alikoenda kwa majaribio? Msilukie mada zingine jibuni apo juu.
Kuhusu uwanja wetu kukarabati tutanza sambamba na waturuki wakianza jenga uwanja wa kusadikika pale bunju,
 
Mimi nilidhani Bahanuzi au Twite au Yondan, kumbe Nonda, kweli kaonyesha njia inabidi Kavumbagu naye atoroke kwenda South maana Nonda naye alitoka Atletico ya Burundi akaja Yanga ila akatoroka kwenda South ndo alikoanza kufanikiwa lakini sio pale kwenye majaruba.

acha fix nonda hakuwahi kucheza ligi kuu ya nchi yeyote kabla ya kucheza ligi kuu ya bongo,na yanga walimuokota mchangani mwananyamala,aliijipeleka yanga baada ya mzee tambwe leya kuita vijana wote wanaojiamini wanajua kucheza mpira,ndio akaenda jangwani kwenye mazoezi ya mchujo wa vijana karibu 100,ikumbukwe wakati huo yanga iliondokewa na wachzaji wengi mahiri baada ya mpondela kuwafurusha kina gulamali waliokua wanawamiliki hao wachezaji akiwemo lunyamila aliyekwenda malindi,said "magoli" mwamba aliyechukuliwa na simba,mzee leya akatengeneza kikosi cha pili cha yanga "black stars" then akawapandisha kuwa yanga kamili ikiitwa yanga yosso,so utaona ujio wa nonda yanga ni tofauti na kina kavambangu ambao wamenunuliwa wakiwa mastaa huko walikotoka,nonda was nothing na alijipeleka yanga bure then akajengwa yanga!
 
Halafu ikamtupa wapi? ingekuwa raha zaidi kama mafanikio hayo yengepatikana kwa m-bongo. Akiwa wa kigeni inakuwa haina mashiko sana, si unaona hata hotel yenyewe kajenga Kinshasa. Kwa nini asijengejenga Mwananyamala 'alikookwota'?

michezaji yenu haina nidhamu wala determination check haruna moshi na lile dili lake la ulaya alivyoliharibu...hao ndio wachezaji tulionao tz pia kumbuka nonda kwenda south aliondoka na nani wakitokea wote yanga?na je nini kilimtokea huyo mtanzania mwenzetu ambae kiukweli yeye ndio alikua star kuliko hata nonda japo walicheza namba tofauti...na pia kukumbusha tu hapo yanga nonda hakua super star kwenye hiyo black star ya mzee leya,kuna watz wenzetu walikua mastaa zaidi yake kama ali yufuf tigana na wengine lakini jiulize waliishia wapi?
 
Tatizo ni dogo. Hawa Simba huwa wanapenda sana sifa hata wasizostahili...so walipenda hii stori ya Nonda iwahusu wao.

Na ingekua wao ndio walimtoa tusingekunywa maji,tizama dogo mbwana samatta ambae anacheza hapo congo tu wala ulaya hajafika wanavyopiga mayowe utafikiri walimtengeneza wao kumbe wao walimsajili akiwa tayari star tofauti na nonda na yanga
 
Mchezaji wa Yanga? Hivi kumbe anaichezea Yanga? Mi najua alipitia Yanga kabla hajaenda alipostahili. Mchezaji wa Yanga akifanikiwa sana labda anunue Starlet na kakibanda ka rooms tatu, choo passport size.

Chezeya soka la bongo?

Kumbe na wewe una wivu!!!??? sikujua
 
Hayo pekee ndiyo mafanikio ambayo watani zetu mnapaswa kujivunia lakini soka hakuna kajipangeni upya, lakini hapo si alifanya kupita tu hata uraia ni wa Kongo vipi kama angekuwa mbongo aliyelelewa na kuuzwa na Yanga kama ambavyo Simba wamefanya kwa akina Samata Magoli, Ulimwengu Tom na wengine wengi wanaoitikisa Dunia mngefanyaje?

Another version of ulimbukeni's revealed..

Hee hii nilikua siijui kumbe hata ulimwengu mlimuuza nyie!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!basi kweli mnatisha ha ha haaaaaaa watu wa simba bwana,hebu fanyeni vizuri angalau mchukue kikombe cha afrika mashariki kagame cup,its long time toka mfanye hivyo,achaneni na samatta chezeni mpira,mashindano ya kimataifa yanawapa tabu sana,ligi ya ndani mnaiweza kwa msaada wa marefa wenu,wakija marefa wa kenya tu mnakwama sana.Halafu hivi ulimwengu alikua anacheza namba vile ndani ya simba??
 
Mi ndo maana nasemaga siku zote,mashabiki wa Simba hata mpira wenyewe hawaujui,huyu naye amekariri kila Mtanzania anayecheza TP Mazembe katoka Simba,poor grafani11 .....embu pata msaada kwa Mwana Msimbazi mwenzio Masuke kuhusiana na wachezaji mliowauzia Mazembe,achana na huyo Bwana Mdogo Ulimwengu aliyekuwa atue Yanga akazuiwa na safari yake ya kwenda kufanya majaribio Ulaya kabla ya kurudi na kuangukia TP Mazembe

mkuu unajichosha bure muulize tu ulimwengu alikua anacheza namba ngapi simba?that's it,uone kama atarudi tena.
 
Umeandaa habari nzuri ila umeshindwa kujieleza Nonda si mchezaji wa Yanga ila aliwahi kuichezea Yanga acha upenzi wa kijinga huna jipya
Habari ndio hii mzee we sijui umesoma habari ipi au ni wale wanaopenda kucomment kabla ya kusoma...nilichoandika ni hiki:

Nonda shabani "Papii" si jina geni kwa wapenzi wa soka wa bongo,huyu ni mchezaji wa zamani wa yanga ya dar es salaam ambae ameonyesha mfano wa kuigwa kwa wachezaji wetu wa bongo kutokana na mafanikio yake ya kisoka na maisha kiujumla.Nonda amezindua hotel yake ya kitalii hivi karibuni hapa kinshasa aliyoipa jina "VILLA FATUMA" uzinduzi uliohudhuriwa na watu wengi maarufu congo akiwemo mwanamuziki wa zamani wa bendi ya wenge musica ADOLPHE DOMINGUEZ.Gonga hapo chini utizame video ya uzinduzi wa hoteli hiyo ya kisasa na nzuri kuliko club za simba na yanga!
 
Kwa hadhi yake na timu alizochezea sikutarajia angezindua hotel hii ya kawaida kabisa ambayo wkinga wengi wanajenga hapo Dar..
ameinvest sana sehemmu nyingine duniani kutokana na political instability ya nchi yake hiyo,hako ni ka mradi kadogo tu alikojaribu congo ili kuona itakuaje
 
Back
Top Bottom