Mchezaji Bora Africa..., Je hii ni Sahihi ?

PascalFlx

Member
Feb 11, 2009
68
5
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana uteuzi wa mchezaji bora Duniani katika mabara mbalimbali ila mpka sasa nashindwa kuelewa ni vigezo gani wanavitumia wenzetu wa mabara mengine kwani uteuzi wao ni tofauti kabisa na unaofanywa na bara la Africa CAF.
Ukiangalia orodha ya wachezaji bora katika mabara tofauti South America South American Footballer of the Year - Wikipedia, the free encyclopedia
Europe :Ballon d'Or - Wikipedia, the free encyclopedia Asia : Asian Footballer of the Year - Wikipedia, the free encyclopedia

Ukianza na Brazil Kaka, Ronaldinho, Ronaldo na wengine wengi wote hao wamewahi kuwa wachezaji bora DUNIANI ila hata mara moja hawajawahi kushinda tuzo ya mchezaji bora America ya Kusini, kwanini...?
Sababu ni moja wao na wengine woote isipokuwa Africa, wanathamini mashindano yanayofanywa ndani ya mabara yao na best player anatokana na katika mashindano ya vilabu ndani ya bara lao.
Tukirudi Ulaya wachezaji wote niliowataja hapo juu wa brazil pamoja na waafrika kama George weah wamewahi kuwa wachezaji bora Ulaya ingawa wao sio wazaliwa wa hapo..., Simple because wanacheza katika vilabu vya Ulaya.

Sasa iweje huku kwetu Africa kila mwaka mchezaji bora wa Africa anatoka Ulaya? je wanatumia vigezo gani kumpata huyo mchezaji? mwisho kwa mchezaji aliyekuwa anachezea ndani ya bara la Africa kuwa mchezaji bora ilikuwa mwaka 1985 mchezaji toka Morocco Mohammed Timoumi aliyekuwa akiichezea FAR Rabat ndiye alishinda tuzo hiyo..., je hii ni sawa?

ni sawa kulinganisha wachezaji wanaocheza Champions league, EPL, La Liga na makombe yetu ya vilabu Africa..?,
Je huyu tumuite Mchezaji bora wa Africa au Mchezaji bora Muafrica.., maana kwa utaratibu huu hata kaka akija kucheza Africa hawezi shinda tuzo hii maana inaonekana jambo la kwanza hapa tunaloangalia ni uafrica na sio mchezaji anachezea wapi

Wana Jamii hebu nisaidieni katika hili labda mimi sielewi vizuri
 
Ndo ligi kubwa zinazokubalika kuwa zina top quality players duniani kwa hiyo ukicheza huko unakua unacheza against top opposition so naona ndo inavyotakiwa.
On another note alitakiwa kushinda Eto mwaka huu sielewi kabisa Adebayor atakuaje bora kuliko Eto????
 
Si kila kitu lazima tuige Ulaya. Kama Ulaya wao kigezo ni mchezaji awe amecheza ligi ya nchi mojawapo ya Ulaya, Afrika nayo inaweza kuwa na vigezo vingine ikiwa pamoja na kumtaka mchezaji husika awe mwenye uraia wa nchi mojawapo ya Afrika bila ya kujali anacheza ligi gani (maybe). Labda hutokea hivyo tu kwa sababu za kimaslahi, kwa kuwa si rahisi mchezaji ambaye anajiona bora aje kucheza ligi ya nchi za Afrika ambako hatalipwa vizuri kama angecheza Ulaya, otherwise huenda hata akina Ronaldo na Ronaldinho wangepewa uchezaji bora wa Afrika kama wangekuwa wanachezea Mwanamotapa ya Zimbabwe au Mundu ya hapo Zanzibar !!
 
Labda kama JF tungeliwaandikia barua hawa watu wanaofanya huu uchaguzi na kuwapa habari yao. Kwanza kuwachagua wachezaji kutoka Africa itawapa nafasi wengine kujulikana na hatimaye kwenda ligi kubwa. Sasa unapompa Etoo ushindi, au Adebayor, mchezaji anayepata paundi tuseme 20,000 kwa wiki si anakuwa anaichukua na kuipeleka kwa mama yake na kuiacha huko?
Tubadilike. Wazo zuri.
 
Tunzo hii ni kwa ajili ya wachezaji wa Africa popote ambapo watakuwepo lakini wawe ni waafrica, Lakini tunzo ya Mchezaj bora wa Ulaya yani (Baloon) ni kwa ajili ya wachezaji wote wanaocheza ulaya ukitoka popote.
 
Nathani CAF wangefanya kuwa African Player of the Year atoke katika ligi za Afrika, possibly from the Afrikan CL. Lile taji aliloshinda Mohammed Aboutrika la Club Player of the year ndilo lingeshindaniwa for the African Player of the Year Outside Afrika or Afrikan Player of the Year Abroad.

Read this for more thoughts on this year's Afrikan Player of the Year: African Debate: CAF Bungles Awards Yet Again - Goal.com
 
Back
Top Bottom