Mohammed Hamad
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 3,988
- 1,304
Tulikuwa wahisani wenye mapenzi tele
Ukanipa mapenzi na mkate wa mchele
Leo nini kimesibu waniona uwele?
Au tofauti zetu dini wanipigia makelele
Kina unapokomenti unanichanja chale
Unipokea kwa wingi huba jamvini
Leo nini kimesibu unanitoa mavini
Ungekuwa mwanaume ningesema nimekuhini
Ni ngedhani ni mapenzi tumegombea vimini
Leo nakuuliza mbona nimekutoka moyoni
Jamvi naliona chungu nahisi ni motoni
Kila ninacho kinena hila wakitia
Awali sikubaini nkaona watania
Muda ukawadia nikaona yako nia
Kwenye hoja hunirukia tena kwa kunikamia
Hata iwe nadhamani hila yeye hulitia............
Ukanipa mapenzi na mkate wa mchele
Leo nini kimesibu waniona uwele?
Au tofauti zetu dini wanipigia makelele
Kina unapokomenti unanichanja chale
Unipokea kwa wingi huba jamvini
Leo nini kimesibu unanitoa mavini
Ungekuwa mwanaume ningesema nimekuhini
Ni ngedhani ni mapenzi tumegombea vimini
Leo nakuuliza mbona nimekutoka moyoni
Jamvi naliona chungu nahisi ni motoni
Kila ninacho kinena hila wakitia
Awali sikubaini nkaona watania
Muda ukawadia nikaona yako nia
Kwenye hoja hunirukia tena kwa kunikamia
Hata iwe nadhamani hila yeye hulitia............