Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Hii ni sehemu ya hansard ya siku ya Julai 15, 2001 (Ijumaa iliyopita) ambapo Zitto alipata nafasi ya kutoa mchango kwenye mapendekezo ya bajeti ya Nishati na Madini. Amezungumzia kwa kirefu kuhusu sekta ya madini na kidogo amegusia suala la umeme. Maangalizi yake kuhusu suala la madini, mambo ya kodi kwenye sekta hiyo na hasa haja ya kuhakikisha kuwa utaratibu unawekwa ili kuwezesha dola kubakia nchini ni ya kuzingatiwa kwani ilivyo sasa naweza kusema (kama nimemuelewa vizuri) kuna "dollar flight" kitu ambacho kimechangia kukosokena kwa dola na hivyo kufanya bei ya dola nchini kuwa juu - hili lina matokeo makubwa kiuchumi.
Zaidi ya yote (na hapa amenigusa vizuri) ni kutaka serikali ifikee mahali iache kuzungumza na makampuni ya madini. Kimsingi anauliza haya mazungumzo ya tangu 2006 hayakomi tu? Amezungumzia mengine mengi japo kwa kupita au kwa haraka sababu ya constraint ya muda. Je yuko sahihi? na wapi anakosea?
Kwa maoni yangu, amekosea sana katika suala la Symbion. Baadhi yetu hatukuwa na tatizo na Dowans kwa sababu ya mitambo chakavu - kwa upande kwa mfano, sijawahi kuwa na issue na uchakavu wa mitambo ya Dowans. Wengi tulikuwa na tatizo na Dowans na Serikali kwa sababu mbili kubwa tu - mchakato wa Dowans was corrupt, na corruption can not be rewarded. Hivyo tukakataa serikali kufanya biashara na Dowans on that simple fact.
Symbion haijaingia kilaghai kama ilivyo ingia Dowans na unlike Dowans, Syimbon kama shirika linalofanya kazi na US government na kama shirika la Kimarekani linafungwa na sheria za Marekani zinazozuia makampuni yake kujihusisha na rushwa ya namna yoyote. Lakini zaidi ni kuwa Serikali ya Tanzania haijanunua mitambo ya Dowans kitu ambacho yeye alikipendekeza na sisi wengine kukipinga. Symbion ndio iliyonunua mitambo hiyo bila ya fedha za Watanzania kuingizwa tena kwenye mifuko ya makuwadi wa ufisadi wa Dowans wakiongozwa na kina Al Adawi na Rostam. Hivyo, basi serikali imefanya exactly kile ambacho sisi wengine tulikitaka, KUTOKUFANYA biashara na Dowans.
Nafikiri katika hili ni sisi wengine tumekuwa sahihi.
Hata hivyo, kama Symbion ina tatizo jingine- ambalo kwangu naona ni la aina mbili hasa kuhusiana na hukumu ya mahakama na pili ushindani wa kuweza kuingia nchini. Hili hata hivyo kama ni tatizo na ni la msingi haiwezekani kuwa ni kwa sababu ya Wamarekani. Nimesikitika kidogo ku-tubait na hoja ya Umarekani kwa sababu kila mtu anajua kabisa kuwa kabla ya Dowans kampuni ambayo ilituingiza kwenye vurugu zote hizi ni Richmond, ya Houston Texas, Marekani. Kumbe hoja ya Umarekani haina msingi in the context of what has transpired so far kwenye suala hili.
Kwenye hoja ambayo ameisema kwa kupita tu kuwa
Maoni yangu bado ni yale yale.
Zaidi ya yote (na hapa amenigusa vizuri) ni kutaka serikali ifikee mahali iache kuzungumza na makampuni ya madini. Kimsingi anauliza haya mazungumzo ya tangu 2006 hayakomi tu? Amezungumzia mengine mengi japo kwa kupita au kwa haraka sababu ya constraint ya muda. Je yuko sahihi? na wapi anakosea?
Kwa maoni yangu, amekosea sana katika suala la Symbion. Baadhi yetu hatukuwa na tatizo na Dowans kwa sababu ya mitambo chakavu - kwa upande kwa mfano, sijawahi kuwa na issue na uchakavu wa mitambo ya Dowans. Wengi tulikuwa na tatizo na Dowans na Serikali kwa sababu mbili kubwa tu - mchakato wa Dowans was corrupt, na corruption can not be rewarded. Hivyo tukakataa serikali kufanya biashara na Dowans on that simple fact.
Symbion haijaingia kilaghai kama ilivyo ingia Dowans na unlike Dowans, Syimbon kama shirika linalofanya kazi na US government na kama shirika la Kimarekani linafungwa na sheria za Marekani zinazozuia makampuni yake kujihusisha na rushwa ya namna yoyote. Lakini zaidi ni kuwa Serikali ya Tanzania haijanunua mitambo ya Dowans kitu ambacho yeye alikipendekeza na sisi wengine kukipinga. Symbion ndio iliyonunua mitambo hiyo bila ya fedha za Watanzania kuingizwa tena kwenye mifuko ya makuwadi wa ufisadi wa Dowans wakiongozwa na kina Al Adawi na Rostam. Hivyo, basi serikali imefanya exactly kile ambacho sisi wengine tulikitaka, KUTOKUFANYA biashara na Dowans.
Nafikiri katika hili ni sisi wengine tumekuwa sahihi.
Hata hivyo, kama Symbion ina tatizo jingine- ambalo kwangu naona ni la aina mbili hasa kuhusiana na hukumu ya mahakama na pili ushindani wa kuweza kuingia nchini. Hili hata hivyo kama ni tatizo na ni la msingi haiwezekani kuwa ni kwa sababu ya Wamarekani. Nimesikitika kidogo ku-tubait na hoja ya Umarekani kwa sababu kila mtu anajua kabisa kuwa kabla ya Dowans kampuni ambayo ilituingiza kwenye vurugu zote hizi ni Richmond, ya Houston Texas, Marekani. Kumbe hoja ya Umarekani haina msingi in the context of what has transpired so far kwenye suala hili.
Kwenye hoja ambayo ameisema kwa kupita tu kuwa
"Waheshimiwa Wabunge waliotangulia kuzungumza na napenda nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa vijana wenzangu wawili, nimewatangulia Bungeni kwa hiyo ni vijana wangu, Mheshimiwa Mnyika na Mheshimiwa Makamba kwa hotuba zao ambazo zinaonyesha dhahiri kwamba imefikia wakati sasa vijana wachukue utawala wa nchi hii."
Maoni yangu bado ni yale yale.