Mchango wa redio za kijamii/mikoa katika maendeleo ya Taifa

Rutunga M

JF-Expert Member
Mar 16, 2009
1,769
1,382
Wakuu,nimekuwa tika mzunguko wa kikazi ulionifanya nizunguke nchi yetu takribani mikoa sita mfululizo,mara,mwanza,shinyanga,kagera,kigoma na rukwa.

Kikubwa nilichogundua ni kuwa kuna utitiri wa redio nyingi katika wilaya na mikoa hiyo na wanapiga miziki asubuhi mpaka jioni na vituo vyote hivyo havina matangazo ya biashara.

Mimi najiuliza hivi ni kwa nini tuwe na vituo vingi vya redio visivyo na tija kwani vingi vinajiunga na TBC wakati TBC inasikika vema katika maeneo hayo.

mathalan nimegundua kuwa mkoa wa kagera pekee kuna redio 5,kwizera(ngara),fadeco na karagwe fm(karagwe),kasibante na vision fm(bukoba mjini),

licha ya wingi huo wa vituo vya redio huwezi kusikia issues za maana katika redio hizo mbali na miziki tu.

TUTAFIKA?
 
Huo ndio ukweli, kakini agalia nani kaanzisha redio hizo? Nyingi zina mikono ya waheshimiwa, hivyo wanmeziweka strategically wakijua kuna wakati watazitumia kwa faida yao. Hawafanyi kazi ya hasara kwa upande wao japo wananchi hawafaidiki na chochote. Katika mkoa wa Kagera ni Radio Kwizera tu iliyofunguliwa kwa malengo maksusi. Ilawalenga wakimbizi hasa katika sula la reunification of the disintergrated families sababu ya vita. Ila hizo nyingine ni siasa tu.
 
Wakuu,nimekuwa tika mzunguko wa kikazi ulionifanya nizunguke nchi yetu takribani mikoa sita mfululizo,mara,mwanza,shinyanga,kagera,kigoma na rukwa.

Kikubwa nilichogundua ni kuwa kuna utitiri wa redio nyingi katika wilaya na mikoa hiyo na wanapiga miziki asubuhi mpaka jioni na vituo vyote hivyo havina matangazo ya biashara.

Mimi najiuliza hivi ni kwa nini tuwe na vituo vingi vya redio visivyo na tija kwani vingi vinajiunga na TBC wakati TBC inasikika vema katika maeneo hayo.

mathalan nimegundua kuwa mkoa wa kagera pekee kuna redio 5,kwizera(ngara),fadeco na karagwe fm(karagwe),kasibante na vision fm(bukoba mjini),

licha ya wingi huo wa vituo vya redio huwezi kusikia issues za maana katika redio hizo mbali na miziki tu.

TUTAFIKA?
Ndo maana kukawa na tume ya mawasiliano(TCRA), ambayo kazi yake ni kutoa regulatory standpoint ya ishu zote zinazohusu mawasiliano.
Kama redio hizi zinapiga muziki toka asubuhi hadi jioni, well ni sehemu ya kazi ya redio KUBURUDISHA(BADO HAWAJAVUNJA SHERIA SANA), lakini lazima kuwe na matangazo na vipindi-Elimishi baadaye, vinginevyo redio hizi zitashindwa hata kujiendesha!
 
Kuna redio fulani binafsi Mbeya iligundulika wanatangaza lugha native za Mbeya kwa lengo la kui'customize redio yao ipendwe zaidi maeneo yao!..Lakini walitiwa mkwara sana na Wizara ya habari, maana kutumia lugha za kienyeji kunaweza kuchochea maasi ya kikabila kama ilivyotokea huko Rwanda!
 
Waswahili husema mwanzo wa ngoma ni lele, nafikiri hii ni fursa nzuri sana kwa wafanya biashara kutangaza biashara zao mpaka interio. Ulitaka watafanya nini wenye vituo vya redio kama hakuna matangazo yakutosha kama sio kupiga huo muziki? Tena hii ni njia nzuri ya kujitangaza kwa jamii kwamba kunakitu kama hiki kinaendelea katika jamii husika. Take a look on RFA by 1997/98 lakini sasa wapo wapi? High Class
Nionavyo mimi ni kwamba kuna mambo mawili makubwa kutokana na hili.
  1. Nyingi zinatarajia kupata income kubwa hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu ujao kwa kufanya kampeni za vyama mbalimbali. huenda zikawa juu zaidi mara bada ya chaguzi hizi kupita.
  2. Waanzilishi a vituo hivi wameona kuna opportunities flani flani katika maeneo husika ndio maana wakaanzishahivi vituo. Huu ni ubunifu mzuri unaohitaji courages
Nakubaliana na PJ kwamba TCRA wana jukumu kubwa katika ku-make sure kwamba zinafuata utaratibu na kanuni zilizopo bila kusita wala kukosa. Nafikiri ni jambo zuri kuzi sapoti na kutoa taarifa sahihi kwenye vyombo husika juu ya waiwasi ama uvunjifu wa sheria ama uchochezi wa aina yeyote unaohisiwa kufanywa na mojawapo ya vituo hivyo popote pale hapa tanzania bila kujali vinamiikiwa na nani ama vipo sponsered na nani. Daima tupende nchi yetu kwa maslai ya watoto wetu hapo kesho.
 
Wakuu,nimekuwa tika mzunguko wa kikazi ulionifanya nizunguke nchi yetu takribani mikoa sita mfululizo,mara,mwanza,shinyanga,kagera,kigoma na rukwa.

Kikubwa nilichogundua ni kuwa kuna utitiri wa redio nyingi katika wilaya na mikoa hiyo na wanapiga miziki asubuhi mpaka jioni na vituo vyote hivyo havina matangazo ya biashara.

Mimi najiuliza hivi ni kwa nini tuwe na vituo vingi vya redio visivyo na tija kwani vingi vinajiunga na TBC wakati TBC inasikika vema katika maeneo hayo.

mathalan nimegundua kuwa mkoa wa kagera pekee kuna redio 5,kwizera(ngara),fadeco na karagwe fm(karagwe),kasibante na vision fm(bukoba mjini),

licha ya wingi huo wa vituo vya redio huwezi kusikia issues za maana katika redio hizo mbali na miziki tu.

TUTAFIKA?

Zama hizi ruksa kufungua Kituo chako cha Redio. Ni hela yako tu. Fungua stesheni yako mwenyewe halafu uwe unatuma vipindi vya kilimo bora cha mikorosho.
 
Back
Top Bottom