Mchana kweupe wamekufa zaidi ya 100..je meli ingezama usiku wangekufa wangapi??

TATOO

Senior Member
Jul 1, 2012
113
21
Nchi hii serikali yake haina jipya na hata haina lepe la aibu na haina cha kutueleza wananchi,,ikumbukwe mwaka 1996 Mv Bukoba ilimaliza roho za watu zaidi ya 2800,Tren ikamaliza maisha ya watu zaidi ya 1200,,mwaka 2011 Meli ya Mv Islender imekata roho za watanzania hawahawa zaidi ya 2000 na leo hii 2012 watanzania walewale zaidi ya 100..wametolewa uhai na kukatisha maisha yao kizembe hivi matukia yote haya ni bahati mbaya na serikali haijajua tatizo ni nini?? hapa napo panahitajika tume za kula pesa? kwanini hii pesa ya kulipa hizi tume isingetumika kuweka kikosi cha uokoaji???

Ni aibu kwa viongozi wa nchi hii kujitokeza mbele ya runinga kusema wanatoa pole kwa ndugu jamaa na wahanga huu ni unafiki wa waziwazi kabisa,,hawa VIONGOZI wanatakiwa wajue kwamba sisi wananchi hatuna shida na pole zao kwakuwa pole hazina tija sisi tunataka huduma za kuokoa maisha ya wananchi tu basi na sio pole mnazotoa na suti za gharama huku wengine wanaliwa na samaki majini....hayo machozi ya wananchi hayaendi bure,,
 
Back
Top Bottom