Mchambuzi wa soka wa ATN asiye na upeo

IshaLubuva

JF-Expert Member
Dec 4, 2008
250
11
Nianze kwa kuwashukuru kituo cha Runinga cha ATN kwa kutuletea uhondo wa ligi ya mabigwa wa Ulaya kupitia king'amuizi cha TING. Hata hivyo nawashauri wawe wanatafuta wachambuzi wenye upeo uliopevuka. Kwenye mechi ya leo kati ya Real Madrid na Olyimpic Lyion, mchamuzi wao aitwaye Musa amemponmda kocha wa Lyion kwa kumuanzisha mchezaji ambaye alikuwa majeruhi kwa kipindi cha miezi saba kwa maoni kwamba mchezaji anayetoka kwenye mapumziko ya majeruhi anatakiwa asianzishwe kwenye mechi bali aingizwe kama sub. Laiti huyu Musa anayejiita mchambuzi wa soka angekuwa mfuatiliaji mzuri wa soka asingetoa maoni hayo kwani tumemuona Steven Gerrald wa Liverpool akitoka kwenye kipindi kirefu cha likizo ya kuwa majeruhi na kuanza kwa mafanikio makubwa katikas mechi ya Liver na Man United ambapo alipiga bao. Jikumbushe bao la Stive kwa kubofya kwenye lionk hapo chini.

Steven Gerard free kick goal against Manchester United 15/10/11 - YouTube
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom