Chadema itajijenga vizuri na kushinda kwa urahisi Urais wa mwaka 2015. Mimi napendekeza, Chadema itangaze mwaka kesho wanaotaka urais wajaze fomu. Baada ya hapo hatua ya pili iwe ni wananchi kuchukua kadi za chadema ili waweze kupiga kura ya kumchagua mgombea. Hatua nyingine iwe ni wagombea kuanza kupita kila kata ya Tanzania kwa ajili ya kupigiwa kura za maoni. Kwa hiyo inahitajika miaka miwili kupita kata zote Tanzania kupigiwa kura. Sasa hii itasaidia sana kwani wakipita kwenye kata wanapiga kampeni ya kukijenga chama, kuandikisha wanachama na kukitambulisha chama na mgombea wake. Hadi uzunguko ukiisha tayari chadema itakuwa imeenea. Hata chama kinaweza kuweka utaratibu kuwa hata siku ya kupiga kura za maoni mtu anaweza kujiunga na chama siku hiyo hiyo na kuruhusiwa kupiga kura,
Itakuwa gharama kubwa lakini itakuwa mbadala wa operesheni sangara. Watu wote hata Shibuda waruhusiwe kugombea ili mradi tu katika kampeni mtu aseme atalifanyia nini taifa na si kupiga vita wagombea wengine
Itakuwa gharama kubwa lakini itakuwa mbadala wa operesheni sangara. Watu wote hata Shibuda waruhusiwe kugombea ili mradi tu katika kampeni mtu aseme atalifanyia nini taifa na si kupiga vita wagombea wengine