kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
KATIKA kuhakikisha inapambana na kero ya msongamano wa magari Dar es Salaam, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni iko katika hatua za mwisho za kuanza mchakato wa ujenzi wa barabara zake kwa kiwango cha lami, ikiwamo ya Kimara Temboni hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Ilala.
Barabara nyingine zinazotarajiwa kujengwa kwa kiwango hicho ni ile ya Mbezi Loius kwenda
Mbezi Beach.
Hayo yameelezwa kwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda aliyesema kwamba, kazi hiyo inaweza kuanza wakati wowote kuanzia mwezi ujao.
Kikao cha tathmini ya mwisho kitaketi hivi karibuni ili kujua gharama halisi na umbali utakaojengwa kwa kiwango cha lami katika barabara za pembezoni ndani ya manispaa yetu, alisema Mwenda.
Alisisitiza kuwa, dhamira kuu ni kuzifanya barabara za Kinondoni kuwa za uhakika na zenye kusaidia kuondoa msongamano katika Jiji la Dar es Salaam ambazo kwa kiasi kikubwa zinatokana na uchache wa barabara za uhakika.
Kwa kuanzia, Februari mwaka huu tumetilia mkazo kutengeneza barabara inayotoka Kimara Temboni kuelekea uwanja wa ndege na barabara inayotoka Mbezi Louis kuelekea Mbezi Beach, nina imani zitasaidia sana kupunguza adha hii, alisema Mwenda.
Na miezi mitano baadaye, yaani kuanzia Julai mwaka huu, halmashauri hiyo imepanga
kutengeneza barabara za pete na kurekebisha madaraja yaliyopo barabara ya zamani ya Bagamoyo.
Sehemu kubwa ya gharama za ujenzi huo inatarajiwa kubebwa na Manispaa ambayo ina vyanzo 34 vya mapato yake na tayari imejiwekea lengo la kuboresha mikakati ya kuongeza mapato kuanzia mwaka ujao wa fedha.
Barabara nyingine zinazotarajiwa kujengwa kwa kiwango hicho ni ile ya Mbezi Loius kwenda
Mbezi Beach.
Hayo yameelezwa kwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda aliyesema kwamba, kazi hiyo inaweza kuanza wakati wowote kuanzia mwezi ujao.
Kikao cha tathmini ya mwisho kitaketi hivi karibuni ili kujua gharama halisi na umbali utakaojengwa kwa kiwango cha lami katika barabara za pembezoni ndani ya manispaa yetu, alisema Mwenda.
Alisisitiza kuwa, dhamira kuu ni kuzifanya barabara za Kinondoni kuwa za uhakika na zenye kusaidia kuondoa msongamano katika Jiji la Dar es Salaam ambazo kwa kiasi kikubwa zinatokana na uchache wa barabara za uhakika.
Kwa kuanzia, Februari mwaka huu tumetilia mkazo kutengeneza barabara inayotoka Kimara Temboni kuelekea uwanja wa ndege na barabara inayotoka Mbezi Louis kuelekea Mbezi Beach, nina imani zitasaidia sana kupunguza adha hii, alisema Mwenda.
Na miezi mitano baadaye, yaani kuanzia Julai mwaka huu, halmashauri hiyo imepanga
kutengeneza barabara za pete na kurekebisha madaraja yaliyopo barabara ya zamani ya Bagamoyo.
Sehemu kubwa ya gharama za ujenzi huo inatarajiwa kubebwa na Manispaa ambayo ina vyanzo 34 vya mapato yake na tayari imejiwekea lengo la kuboresha mikakati ya kuongeza mapato kuanzia mwaka ujao wa fedha.