Mchakato wa katiba mpya na vipindi vya Tbc1

Maengo

JF-Expert Member
Jul 7, 2011
280
29
Ni juzi tu niliwasikia wabunge wa CCM wakiishambulia ITV kwa madai kuwa inafanya uchochezi kwa kurusha vipindi vya makongamano yanayopotosha wananchi yanayohusu upatikanaji wa katiba mpya. Na walienda mbali zaidi kwa kuisifia TBC1 kuwa imekuwa na vipindi vizuri sana....! Leo jioni hapa nyumbani nilikuta wenzangu wakiangalia kipindi cha CHEREKO kinachorushwa na tbc1 kila jumapili, ndipo hapo nikakumbuka zile sifa ambazo tbc1 ilimwagiwa na wabunge wa CCM!
Hivi kipindi kama CHEREKO kina manufaa gani kwa taifa ukizingatia ile ni tv ya taifa? Je, ni vipindi hivi hivi ambavyo wabunge wa CCM walikuwa wanatetea?
m
 
Wabunge wa ccm wana
boa sana, sipendi kuwasikia. Wanapenda kutetea ujinga sana, hamkumuona jenista na wanae walivyokuwa wanaonyesha jinsi wanavyo2ibia?
 
Mimi sipingi kuwepo kwa vipindi vya cherekochereko TBC1 ninachokipinga kuhusu tbc1 ni kule kujigeuza kuwa agent wa ccm kila kitu hata kama kina masilahi kwa taifa lakini kina hatarisha ustawi wa ccm kitawekwa pembeni na vipindi visivyo na maana vitawekwa. mfano; mimi sioni sababu ya tbc kujiweka upande wowote katika suala hili la katiba kama chombo cha taifa ndicho kilitakiwa kiwe mstari wa mbele kuandaa makongamano na kuwasikiliza watu wanataka katiba ya namna gani!! hata hiyo tume ikisha undwa tayari kutakuwa na idea kuwa wananchi wanataka kuwe na nini na kusiwepo na nini kwenye katiba mpya. lakini kinachoonekana tbc1 + mibunge ya ccm hawajui kuwa suala la katiba ni beyond political parties, ni suala la kitaifa zaidi!! lakini wao wameligeuza kuwa ni vita kati ya chama fulani na chama fulani, huu ni upuuzi wa hali ya juu, na kama itv na redio wani nao wakaamua kufuta ujinga huu basi watanzania tutakosa pa kusemea hivyo tutakufa kiume au kibudu.
 
Back
Top Bottom