Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,906
- 22,048
Mbwa wa Iringa wapoteza urafiki Send to a friend FRM MWANANCHIWednesday, 29 September 2010 09:41 0diggsdigg
Tumaini Msowoya, Iringa
ZAIDI ya watu 250 wamejeruhiwa kwa kuumwa na mbwa kati ya mwezi Januari na Septemba mwaka huu, katika Manispaa ya Iringa kwenye matukio mbalimbali.
Ilielezwa kwamba moja ya sababu ni tabia ya wafugaji wa mbwa kuwaacha wanyama hao wakizurura mitaani kinyume cha sheria.
Akizungumza katika kilele cha wiki ya maadhimisho ya kichaa cha mbwa duniani, daktari wa mifugo katika manispaa hiyo, Nikolas Mgumba alisema watu wengi wamekuwa wakingatwa na mbwa hao kutokana na wafugaji kutokuwa makini na mbwa wao, jambo ambalo ni hatari.
Alisema mbwa wengi wamekuwa wakizurura kutokana na ukweli kwamba wanaowahudumia mbwa hao ni vijana wadogo ambao muda mwingi huwa shuleni.
Alisema kutokana na hali hiyo, Manispaa ya Iringa kupitia idara ya kilimo na mifugo imefanya msako na kuwaua mbwa 36 wanaozurura mitaani.
Akizungumzia chanjo, alisema kuwa manispaa hiyo yenye mbwa 2,758 ilichanja mbwa 1,694 ambao ni sawa na asilimia 61, huku asilimia 39 wakiwa hawajachanjwa jambo ambalo ni hatari.
Alisema jitihada kubwa za manispaa hiyo ni kuhakikisha mbwa wote wanachanjwa sambamba na kutunga sheria zitakazowabana wamilikiwa wa mbwa kuhakikisha wanachanja mbwa wao.
Hata hivyo aliwashauri watu wanaongatwa na wanyama hao kutoa taarifa haraka kupata huduma ya haraka ya kukamuliwa damu katika eneo lililongatwa ikiwa ni pamoja na kuosha kwa maji safi yenye sabuni, ili kupunguza sumu ikiwa mbwa aliyemngata ana kichaa.
Tumaini Msowoya, Iringa
ZAIDI ya watu 250 wamejeruhiwa kwa kuumwa na mbwa kati ya mwezi Januari na Septemba mwaka huu, katika Manispaa ya Iringa kwenye matukio mbalimbali.
Ilielezwa kwamba moja ya sababu ni tabia ya wafugaji wa mbwa kuwaacha wanyama hao wakizurura mitaani kinyume cha sheria.
Akizungumza katika kilele cha wiki ya maadhimisho ya kichaa cha mbwa duniani, daktari wa mifugo katika manispaa hiyo, Nikolas Mgumba alisema watu wengi wamekuwa wakingatwa na mbwa hao kutokana na wafugaji kutokuwa makini na mbwa wao, jambo ambalo ni hatari.
Alisema mbwa wengi wamekuwa wakizurura kutokana na ukweli kwamba wanaowahudumia mbwa hao ni vijana wadogo ambao muda mwingi huwa shuleni.
Alisema kutokana na hali hiyo, Manispaa ya Iringa kupitia idara ya kilimo na mifugo imefanya msako na kuwaua mbwa 36 wanaozurura mitaani.
Akizungumzia chanjo, alisema kuwa manispaa hiyo yenye mbwa 2,758 ilichanja mbwa 1,694 ambao ni sawa na asilimia 61, huku asilimia 39 wakiwa hawajachanjwa jambo ambalo ni hatari.
Alisema jitihada kubwa za manispaa hiyo ni kuhakikisha mbwa wote wanachanjwa sambamba na kutunga sheria zitakazowabana wamilikiwa wa mbwa kuhakikisha wanachanja mbwa wao.
Hata hivyo aliwashauri watu wanaongatwa na wanyama hao kutoa taarifa haraka kupata huduma ya haraka ya kukamuliwa damu katika eneo lililongatwa ikiwa ni pamoja na kuosha kwa maji safi yenye sabuni, ili kupunguza sumu ikiwa mbwa aliyemngata ana kichaa.