Mbwa daima si huwa na mmiliki wake?

Dopas

JF-Expert Member
Aug 14, 2010
1,151
392
WanaJF salam

Ninavyofahamu kati ya wanyama wafugwao, mbwa hufugwa kwaajili ya ulinzi. Mbwa mlinzi mzuri huwafahamu mabosi wake, kwa kawaida mbwa huwafahamu wakazi wote wa nyumba kupitia kwa bosi wake. Kama mbwa anakuwa rafiki wa kila afikaje nyumbani sio tena mbwa mlinzi, bali 'pet'.

Ikiwa mbwa anambwekea mgeni na hata kumng'ata mgeni il hali bosi wake anatazama tu, wa kulaumiwa kwa kawaida si mbwa bali ni bosi wake.

WanaJF wiki yote tumeshuhudia matusi ya UVCCM hususan yaliyoelekezwa kwa baadhi ya wazee wa chama chao. Lawama nyingi tumewatupia hao vijana kwa kukosa adabu hiyo. Hapo hatuzunguzumzii waliyosema kuhusu upinzani hasa Chadema. Pengine tungeona hiyo ni kawaida, tumezoea.

Kweli matusi wanayowaelekezea wazee wao hadharani ni bure? Hiyo UVCCM ndiyo chombo cha juu katika uongozi wa CCM? Kama sio chombo cha juu hayo matusi wanayotoa mabosi wao wameridhia? Kama hawajaridhia mbona hatuoni hata moja akiomba walau msamaha kwa niaba ya hao vijana waoliopotoka? Kama hawajapotoka, na wanachofanya ni sahihi nani kawatuma? Wanapata nguvu wapi ya kuwatukana wazee wa nyumbani mwao hadharani? Je, kama wamefanya hayo kwa wazee wa nyumbani mwao- tena waasisi wa chama chao, itakuwaje kwa vyama vingine?

WanaJF, ndiyo maana sasa naanza kuamini walichosema katika kikao chao cha Dodoma kuwa wanajipanga kuwa kila hali kupambana na Chadema.

Tutashangaa nini kwa chochote kutoka kwa hao vijana ambao wameonesha utovu wa adabu hadharani dhidi ya wazee wao, wakiwafanyia chochote Chadema?

Nadhani inatosha kuwalaumu hao vijana. Inafaa kumtambua aliye nyuma yao. Kwa bahati mbaya yeyote ambaye yuko nyuma yao hatambui anaongeza mgawanyiko ndani ya chama chao na kuharakisha kifo chake. Leo ni zamu ya Sumaye na Sita kutukanwa, kesho itakuwa zamu yake. Anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga. Tusubiri...

Tutafakari haya kwa mtazamo wa siasa, na sio vinginevyo.
 
WanaJF salam

Ninavyofahamu kati ya wanyama wafugwao ambao hufugwa kwaajili ya kazi muhimu ya ulinzi ni mbwa. Mbwa ili aweze kuwa mlinzi mzuri ni lazima awafahamu mabosi wake, kwa kawaida mbwa huwafahamu wakazi wote wa nyumba kupitia kwa bosi wake. Kama mbwa anakuwa rafiki wa kila afikaje nyumbani sio tena mbwa mlinzi, bali 'pet'.

Ikiwa mbwa anambwekea mgeni na hata anaenda kumng'ata mgeni il hali bosi wake anatazama tu. Wa kulaumiwa kwa kawaida si mbwa bali ni bosi wake.

WanaJF wiki yote tumeshuhudia matusi ya UVCCM hususan yaliyoelekezwa kwa baadhi ya wazee wa chama chao. Lawama nyingi tumewatupia hao vijana kwa kukosa adabu hiyo. Hapo hatuzunguzumzii waliyosema kuhusu upinzani hasa Chadema. Pengine tungeona hiyo ni kawaida, tumezoea.

Kweli matusi wanayowaelekezea wazee wao hadharani ni bure? Hiyo UVCCM ndiyo chombo cha juu katika uongozi wa CCM? Kama sio chombo cha juu hayo matusi wanayotoa mabosi wao wameridhia? Kama hawajaridhia mbona hatuoni hata moja akiomba walau msamaha kwa niaba ya hao vijana waoliopotoka? Kama hawajapotoka, na wanachofanya ni sahihi nani kawatuma? Wanapata nguvu wapi ya kuwatukana wazee wa nyumbani mwao hadharani? Je, kama wamefanya hayo kwa wazee wa nyumbani mwao- tena waasisi wa chama chao, itakuwaje kwa vyama vingine?

WanaJF, ndiyo maana sasa naanza kuamini walichosema katika kikao chao cha Dodoma kuwa wanajipanga kuwa kila hali kupambana na Chadema.

Tutashangaa nini kwa chochote kutoka kwa hao vijana ambao wameonesha utovu wa adabu hadharani dhidi ya wazee wao, wakiwafanyia chochote Chadema?

Kwa busara ya kawaida mtoto ambaye hana heshima kwa wazazi wake hawezi kuwaheshimu wazazi wa mwingine.

Tutafakari haya kwa mtazamo wa siasa, na sio vinginevyo.

upumbavu wao wafanyie hukohuko CCM.

Kabla ya kukishughulikia chadema na wafuasi wake, ambao ni sisi, wanapashwa kujua jambo moja muhimu:

Chadema siyo chama cha wazee. Kwa hiyo wasiseme kireja-reja ati watatushughulikia. Tutashughulikiana. Wala wasitarajie mteremko katika hilo. we are ready, they can pull the trigger if they mean business. waachane na kuchonga kwenye microphone za media. shenz kabisa.
 
Mimi sisomi tena threads zinazohusu UVCCM na CCM...... naomba mlete za katiba mpya,Dowans na umeme.....
 
upumbavu wao wafanyie hukohuko CCM.

Kabla ya kukishughulikia chadema na wafuasi wake, ambao ni sisi, wanapashwa kujua jambo moja muhimu:

Chadema siyo chama cha wazee. Kwa hiyo wasiseme kireja-reja ati watatushughulikia. Tutashughulikiana. Wala wasitarajie mteremko katika hilo. we are ready, they can pull the trigger if they mean business. waachane na kuchonga kwenye microphone za media. shenz kabisa.

Unajua inavyoonekana wana mpango wa kuanza kuleta tena fujo kama za mwaka jana na kusema ni sisi Chadema. Nadhani kwa sasa hawatafanikiwa kwani tumeona nia na azma yao mapema. Ila namsikitikia huyo aliye nyuma yao. Atajuta
 
WanaJF salam

Ninavyofahamu kati ya wanyama wafugwao, mbwa hufugwa kwaajili ya ulinzi. Mbwa mlinzi mzuri huwafahamu mabosi wake, kwa kawaida mbwa huwafahamu wakazi wote wa nyumba kupitia kwa bosi wake. Kama mbwa anakuwa rafiki wa kila afikaje nyumbani sio tena mbwa mlinzi, bali 'pet'.

Ikiwa mbwa anambwekea mgeni na hata kumng'ata mgeni il hali bosi wake anatazama tu, wa kulaumiwa kwa kawaida si mbwa bali ni bosi wake.

WanaJF wiki yote tumeshuhudia matusi ya UVCCM hususan yaliyoelekezwa kwa baadhi ya wazee wa chama chao. Lawama nyingi tumewatupia hao vijana kwa kukosa adabu hiyo. Hapo hatuzunguzumzii waliyosema kuhusu upinzani hasa Chadema. Pengine tungeona hiyo ni kawaida, tumezoea.

Kweli matusi wanayowaelekezea wazee wao hadharani ni bure? Hiyo UVCCM ndiyo chombo cha juu katika uongozi wa CCM? Kama sio chombo cha juu hayo matusi wanayotoa mabosi wao wameridhia? Kama hawajaridhia mbona hatuoni hata moja akiomba walau msamaha kwa niaba ya hao vijana waoliopotoka? Kama hawajapotoka, na wanachofanya ni sahihi nani kawatuma? Wanapata nguvu wapi ya kuwatukana wazee wa nyumbani mwao hadharani? Je, kama wamefanya hayo kwa wazee wa nyumbani mwao- tena waasisi wa chama chao, itakuwaje kwa vyama vingine?

WanaJF, ndiyo maana sasa naanza kuamini walichosema katika kikao chao cha Dodoma kuwa wanajipanga kuwa kila hali kupambana na Chadema.

Tutashangaa nini kwa chochote kutoka kwa hao vijana ambao wameonesha utovu wa adabu hadharani dhidi ya wazee wao, wakiwafanyia chochote Chadema?

Nadhani inatosha kuwalaumu hao vijana. Inafaa kumtambua aliye nyuma yao. Kwa bahati mbaya yeyote ambaye yuko nyuma yao hatambui anaongeza mgawanyiko ndani ya chama chao na kuharakisha kifo chake. Leo ni zamu ya Sumaye na Sita kutukanwa, kesho itakuwa zamu yake. Anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga. Tusubiri...

Tutafakari haya kwa mtazamo wa siasa, na sio vinginevyo.
Babu wao Makamba ndio mwanza anawashangilia kwa kupiga miluzi na kuwahamasisha watoto wawatukane wazee wao,hakika busara za wazee wengine hupungua kwa jinsi muda wa kukaa duniani unavyozidi kuwa mdogo,ukiwa na kiongozi sampuli ya Makamba unategemea nini?yeye anajifanya eti anamsemea mwenyekiti wake
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom