Mkuu hapa unaonyesha umbumbu wako katika biashara ya kahawa. Ukweli ni kwamba siyo sahihi kulinganisha bei ya cherry na bei ya kahawa safi mnadani bila ya kuzingatia gharama za kumenya,kuvundika, kuosha, kuanika, kuhifadhi, kukoboa , gharama za magunia, gharama za kuipeleka mnadani na gharama zingine za uendeshaji.
Hata hivyo bei ya kahawa mnadani hakuna ambaye uwa anaifahamu wakati wa kununua cherry hivyo ni kucheza kamari kwa mnunuzi atakapoifikisha mnadani ikiwa imepanda ananufaika ikishuka anaumia. Na ili uwa linatokea. Hivyo bei pekee ya kuweza kulinganisha ni ile inayotembea ngazi ya mkulima ya Parchment kwa wakati huo.Mathalani huku Mbinga bei ya cherry ni shs 500 kwa kilo wakati bei ya parchment ni shs 2500 yaani shs 500 x 5 = 2500.
Kwa bei hii mkulima anayeuza cherry ananufaika kwa vile haingii gharama zinazohitajika kuifanya iwe parchment. Si hilo tu, mkulima ananufaika endapo maamuzi ya kuuza cherry yanatokana kutaka kumaliza shida za dharura kama kulipa ada za shule. Kama kutakuwa hakuna soko rasmi inamlazimu kuuza kahawa yake kwa walanguzi ambao mara nyingi ni wamiliki wa vikundi ili akidhi shida zinazomkabiri.
Je hupo hapo, kajifunze tena ili uweze kutoa somo.
Hata hivyo bei ya kahawa mnadani hakuna ambaye uwa anaifahamu wakati wa kununua cherry hivyo ni kucheza kamari kwa mnunuzi atakapoifikisha mnadani ikiwa imepanda ananufaika ikishuka anaumia. Na ili uwa linatokea. Hivyo bei pekee ya kuweza kulinganisha ni ile inayotembea ngazi ya mkulima ya Parchment kwa wakati huo.Mathalani huku Mbinga bei ya cherry ni shs 500 kwa kilo wakati bei ya parchment ni shs 2500 yaani shs 500 x 5 = 2500.
Kwa bei hii mkulima anayeuza cherry ananufaika kwa vile haingii gharama zinazohitajika kuifanya iwe parchment. Si hilo tu, mkulima ananufaika endapo maamuzi ya kuuza cherry yanatokana kutaka kumaliza shida za dharura kama kulipa ada za shule. Kama kutakuwa hakuna soko rasmi inamlazimu kuuza kahawa yake kwa walanguzi ambao mara nyingi ni wamiliki wa vikundi ili akidhi shida zinazomkabiri.
Je hupo hapo, kajifunze tena ili uweze kutoa somo.