dm2000inter
Member
- Oct 27, 2010
- 29
- 10
Mbunge wa CCM Jimbo la Mbozi Mashariki, Mheshimiwa Godfrey Weston Zambi Jumatano wiki hii mjini Moshi amefunguliwa kesi ya madai na kampuni ya Lima Limited akidaiwa fidia ya shilingi 2.4 bilioni kwa tuhuma za kutoa matamshi ya kuikashifu kampuni hiyo.
Katika gazeti la Mwanahalisi la Juni 13-19,2012, Mheshimiwa Zambi anadaiwa kutamka" Lima imekuwa ikiwashawishi wakulima kuuza kahawa mbivu kwa bei ndogo sana".
Kampuni hiyo inamtuhumu Zambi kuanzisha kampeni mbaya dhidi ya kampuni hiyo ili kuondoa ushindani wa soko ili kuvipa fursa vikundi vya wakulima ambavyo Zambi ana maslahi navyo visipate ushindani wowote katika soko la Kahawa. K
esi hiyo namba CC 7/2012 imefunguliwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi,Eric Ng'maryo ambaye pia ni Advocate Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.
Katika gazeti la Mwanahalisi la Juni 13-19,2012, Mheshimiwa Zambi anadaiwa kutamka" Lima imekuwa ikiwashawishi wakulima kuuza kahawa mbivu kwa bei ndogo sana".
Kampuni hiyo inamtuhumu Zambi kuanzisha kampeni mbaya dhidi ya kampuni hiyo ili kuondoa ushindani wa soko ili kuvipa fursa vikundi vya wakulima ambavyo Zambi ana maslahi navyo visipate ushindani wowote katika soko la Kahawa. K
esi hiyo namba CC 7/2012 imefunguliwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi,Eric Ng'maryo ambaye pia ni Advocate Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.