Mbunge wa Ubungo John Mnyika anyimwa na polisi kufanya mkutano

Kwa mujibu wa status katika facebook wall ya John Mnyika muda mchache uliopita ametoa taarifa ya Uongozi wa Chadema Jimbo la Ubungo kupokea simu toka Jeshi la Polisi yenye kumzuia kufanya mkutano ambao ilikuwa auanze kuufanya mnamo saa kumi kamili alasiri eneo la uwanja wa Yenu Bar mkabala na Kituo cha Mabasi-Ubungo.

Mnyika, ametoa msimamo wa kuendelea na mkutano huo sambamba na mikutano mingine yote aliyokuwa amepanga kuifanya kwani hajapatiwa taarifa kwa maandishi.

Alisema katika status yake hiyo kuwa Jeshi la Polisi lilishapatiwa taarifa mnamo tarehe 3 na kukumbushwa tarehe 4 ya mwezi huu, (Novemba), 2011 bila ya wao kutoa majibu yoyote.
 
sasa mbunge atawasikilizia wapi wapiga kura wake kama sio mikutano ya hadhara?
 
Irrelevant argument since government of Tz and its people do not seem to fear each other but we are all fearing the common foe Al-Shabaab.

Please do not insult our intellegency! Al-Shaabab did not emerge yesterday. And it was only last week Tanzanians in thier thosounds were chearing thier teams (Simba & Yanga) at the National Stadium why didnt you stop the match? Childshid and silly excuses!
 
Police nilyekuwa namwona ana akili sana alikwa Tibaigana tu wengine sijui vilaza maana mara intellegensia mara all-shabib labda CCM wana hisa kenya wanawatwanga sie twawapokea, Tibagaina wakati wake maandamano yalikuwa kama kawaida na anawasindikiza kwa amani hata akikataza anaonyesha ukweli wa jambo labda na CDM waanzishe alishabbbi ya kuwalinda
 
Why do we always question our intelligence?lets start being positive,i still have faith with IGP Mwema.
 
Hivi hawa polisi wamezaliwa na mwanamke kweli.Kila kukicha visavisa,mbona hakuna mkutano wa magamba unaowekewa ngumu kivile kama wa sungura V.Mara intelijensia,mara interpool,mara FBI,mara Alcaida,mara wasomali.Nashindwa kuamini kama nchi yenu ina usalama,mara mkuu wa polisi mkoa anatabasamu kwenye TV eti amekamata wahamiaji haramu kwenye milima fulani,walikuwa wanapelekewa chakula,wamepitia wapi si kazi,kazi kukamata.Wananchi kuwasikiliza viongoz wao,hawana silaha,Unasema marufuku,bado mtasema sasa kwenda maliwatoni ni marufuku.Ntanunua rungu.
 
Alshababu hawana shida na wananchi wao wanashida na magogoni na wote waliotoa kauli za kuunga mkono Kenya kuwashambulia.Mnyika Business as Usual ongea na wapiga kura wako hiyo ndiyo njia pekee ya kupata mrejesho kwa wapigakura.
 
Waendelee na mkutano wao ila wawe makini kwani ccm na serikali yake walivyo sasa wanaweza kuwashambulia kwenye huo mkutano na wakawasingizia al-shabab. Nasema hilo linawekana na wala si lakupuuziwa.
Hapa kuna jambo linaandaliwa kujustfy intelejensia yao,lengo hasa nikuwazuia kabisa chadema kufanya mikutano yao hasa wakati huu wa vuguvugu la KATIBA mpya na huu ufisadi unaondelea kuibuliwa na kamati za bunge.Kwa hali ilivyo sasa serikalini wanaweza kufanya chochote ili kuhamisha mawazo ya wananchi kwa hii hali ngumu tokea nchi hii ipate uhuru,ukiondoa wakati wa vita ya kagera.Huku mtaani kimenuka sasa watu kulala na njaa ni kawaida.
 
Inabidi kutii amri ya polisi maana hao Al shabab wamekuwa tishio...
 
Polisi wamepiga simu kwa viongozi wa Chadema Ubungo kuzuia mkutano wa hadhara wa mbunge wa kueleza kazi za mbunge kwa mwaka mmoja pamoja na kupokea maoni ya wananchi kuhusu muswada wa katiba mpya usifanyike.

Sababu walizotoa polisi kwa simu ni kuwa kuna tishio la Alshabab. Polisi walipewa taarifa ya mkutano toka tarehe 3 wakakumbushwa tena tarehe 4 lakini hawakujibu. Taarifa ndani ya Chadema zinasema kwamba mbunge ameamua kuendelea na mkutano kama kawaida kwa kuwa hakuna katazo la maandishi lililotolewa na polisi. Mkutano unatarajiwa kuanza saa 10 jioni eneo la Ubungo mwisho pembeni ya stand ya daladala karibu na yenu bar.

hapa napita tu.

mpaka nitakapofahamishwa kuwa zuio la maandishi limetolewa.

serekali yenye akili haifanyi kazi kwa simu.
 
Inshu hapa ni kuwa CCM wamepata sehemu ya kupumulia, subirini hiyo game haitaishia mapema!!
 
Irrelevant argument since government of Tz and its people do not seem to fear each other but we are all fearing the common foe Al-Shabaab.

tumeichokoza lini hyo al shabab mpaka wahangaike na sisi? Labda tungekua tumetoa majeshi yaende somalia...hyo ni mbinu chafu tu ya kuzuia huo mkutano usiendelee, halafu unasema polisi wametoa taarifa mapema wakati taarifa imetoka leo na kwa kupiga simu? Taarifa gani ya mapema unapiga simu? Try to thnk like u ve got a brain usibebwe tu na wimbi kama nazi mbovu baharini
 
Btw, what's the difference between ccm and al shabaab?
Mi naona wote ni magenge ya mumiani tu, wauaji na wanywa damu za watu. Ccm wameua raia wangapi wasio na hatia? Yawezekana ccm wanashirikiana na al shabaab.
 
Btw, what's the difference between ccm and al shabaab?
Mi naona wote ni magenge ya mumiani tu, wauaji na wanywa damu za watu. Ccm wameua raia wangapi wasio na hatia? Yawezekana ccm wanashirikiana na al shabaab.

Hapo kwenye red linawezekana maana hata Makyembe alisema katika taarifa ya kutaka kuuawa kwake
 
Mbona hawazuhii friday night clubs kule Michokeni,mbalamwezi?mbona hawazuhii mihadhara ya ijumaa pale Manzese darajani tena eneo la wazi?ama wanataka tuamini kwamba CDM ina affiriation na Al-Sh?

Wapumbavu wakubwa hawa ndo maana wana madarasa ya kuhesabu vidole vya kuku,wanadili na watu badala ya vitu
 
Waendelee na mkutano wao ila wawe makini kwani ccm na serikali yake walivyo sasa wanaweza kuwashambulia kwenye huo mkutano na wakawasingizia al-shabab. Nasema hilo linawekana na wala si lakupuuziwa.

Kabisa Mkuu, hata mimi nimeona wanatafuta kisingizio cha kuwashambulia cdm halafu waseme ni alshabaab.
 
Hivi hawa polisi wamezaliwa na mwanamke kweli.Kila kukicha visavisa,mbona hakuna mkutano wa magamba unaowekewa ngumu kivile kama wa sungura V.Mara intelijensia,mara interpool,mara FBI,mara Alcaida,mara wasomali.Nashindwa kuamini kama nchi yenu ina usalama,mara mkuu wa polisi mkoa anatabasamu kwenye TV eti amekamata wahamiaji haramu kwenye milima fulani,walikuwa wanapelekewa chakula,wamepitia wapi si kazi,kazi kukamata.Wananchi kuwasikiliza viongoz wao,hawana silaha,Unasema marufuku,bado mtasema sasa kwenda maliwatoni ni marufuku.Ntanunua rungu.

Mkuu hii serikali ya ccm imeacha kuhangaikia wananchi wake wamebaki kupambana na cdm, wajinga hawa wanazidi kupoteza mda tu. Kama ndo hivyo basi hata cku za ijumaa na jumapili watu wasiende ibadani kwa sababu ni mkusanyiko pia.
 
Back
Top Bottom