asha ngedere
Member
- Nov 6, 2009
- 92
- 11
Wadau, this is very very serious.
Nakumbuka wakati fulani mwaka jana kuna mwandishi wa gazeti moja aliwahi ku-uncover vitendo vichafu vya aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini (CCM) ambaye kwa bahati 'nzuri' sasa ndiye mbunge rasmi baada ya matokeo yale 'kuchakachuliwa'.
Miongoni mwa vitendo vichafu vilivyotajwa ni pamoja na kudanganya elimu kwamba yeye ni form four wakati kumbe alifukuzwa shule kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. Pia alidaiwa kukwepa kodi na kashfa nyingine, ikiwemo kudaiwa kumteka mtu na kumfanyia unyama kinyume cha maumbile, kashfa ambayo amejitahidi kuikanusha akisaidiwa na baadhi ya viongozi wa chama chake.
Lakini ndugu zangu, kinachonisikitisha ni kashfa yake nyingine kubwa ya kumpa mimba mwanafunzi wa chini ya miaka 18, wa kidato cha tatu na kumsababishia kukatisha masomo.
Kwa muda mrefu amekuwa akipigana kufa na kupona kuhakikisha suala hilo haliyafikii masikio ya Watanzania na inasemekana hata taasisi zile za kuwatetea akina mama nazo zimekuwa kimya ingawa zilikwishapelekewa taarifa hizo siku nyingi.
Mimi nauliza, hivi kuna mtu anayemlinda Mbunge huyu? Mbona raia wa kawaida - hata wasio na fedha - wakihusishwa na vitendo vya ubakaji ama kuwapa mimba wanafunzi wanashikiwa bango na wengine tumesikia wamehukumiwa jela? Hivi Serikali inasubiri mzazi wsa binti ndiye aende akashtaki wakati hili ni kosa la jinai ambalo yenyewe ndiyo inapaswa kushtaki?
Jamani, naogopa kumwaga machozi JF, hebu wadau nisaidieni mwanaharakati mwenzenu. Nchi hii tunaipeleka wapi?
Wasaalamu.
Nakumbuka wakati fulani mwaka jana kuna mwandishi wa gazeti moja aliwahi ku-uncover vitendo vichafu vya aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini (CCM) ambaye kwa bahati 'nzuri' sasa ndiye mbunge rasmi baada ya matokeo yale 'kuchakachuliwa'.
Miongoni mwa vitendo vichafu vilivyotajwa ni pamoja na kudanganya elimu kwamba yeye ni form four wakati kumbe alifukuzwa shule kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. Pia alidaiwa kukwepa kodi na kashfa nyingine, ikiwemo kudaiwa kumteka mtu na kumfanyia unyama kinyume cha maumbile, kashfa ambayo amejitahidi kuikanusha akisaidiwa na baadhi ya viongozi wa chama chake.
Lakini ndugu zangu, kinachonisikitisha ni kashfa yake nyingine kubwa ya kumpa mimba mwanafunzi wa chini ya miaka 18, wa kidato cha tatu na kumsababishia kukatisha masomo.
Kwa muda mrefu amekuwa akipigana kufa na kupona kuhakikisha suala hilo haliyafikii masikio ya Watanzania na inasemekana hata taasisi zile za kuwatetea akina mama nazo zimekuwa kimya ingawa zilikwishapelekewa taarifa hizo siku nyingi.
Mimi nauliza, hivi kuna mtu anayemlinda Mbunge huyu? Mbona raia wa kawaida - hata wasio na fedha - wakihusishwa na vitendo vya ubakaji ama kuwapa mimba wanafunzi wanashikiwa bango na wengine tumesikia wamehukumiwa jela? Hivi Serikali inasubiri mzazi wsa binti ndiye aende akashtaki wakati hili ni kosa la jinai ambalo yenyewe ndiyo inapaswa kushtaki?
Jamani, naogopa kumwaga machozi JF, hebu wadau nisaidieni mwanaharakati mwenzenu. Nchi hii tunaipeleka wapi?
Wasaalamu.