Mbunge wa Sumbawanga Mjini aliyempa mimba mwanafunzi mbona hashughulikiwi au Serikali inamlinda?

asha ngedere

Member
Nov 6, 2009
92
11
Wadau, this is very very serious.

Nakumbuka wakati fulani mwaka jana kuna mwandishi wa gazeti moja aliwahi ku-uncover vitendo vichafu vya aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini (CCM) ambaye kwa bahati 'nzuri' sasa ndiye mbunge rasmi baada ya matokeo yale 'kuchakachuliwa'.

Miongoni mwa vitendo vichafu vilivyotajwa ni pamoja na kudanganya elimu kwamba yeye ni form four wakati kumbe alifukuzwa shule kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. Pia alidaiwa kukwepa kodi na kashfa nyingine, ikiwemo kudaiwa kumteka mtu na kumfanyia unyama kinyume cha maumbile, kashfa ambayo amejitahidi kuikanusha akisaidiwa na baadhi ya viongozi wa chama chake.

Lakini ndugu zangu, kinachonisikitisha ni kashfa yake nyingine kubwa ya kumpa mimba mwanafunzi wa chini ya miaka 18, wa kidato cha tatu na kumsababishia kukatisha masomo.

Kwa muda mrefu amekuwa akipigana kufa na kupona kuhakikisha suala hilo haliyafikii masikio ya Watanzania na inasemekana hata taasisi zile za kuwatetea akina mama nazo zimekuwa kimya ingawa zilikwishapelekewa taarifa hizo siku nyingi.

Mimi nauliza, hivi kuna mtu anayemlinda Mbunge huyu? Mbona raia wa kawaida - hata wasio na fedha - wakihusishwa na vitendo vya ubakaji ama kuwapa mimba wanafunzi wanashikiwa bango na wengine tumesikia wamehukumiwa jela? Hivi Serikali inasubiri mzazi wsa binti ndiye aende akashtaki wakati hili ni kosa la jinai ambalo yenyewe ndiyo inapaswa kushtaki?

Jamani, naogopa kumwaga machozi JF, hebu wadau nisaidieni mwanaharakati mwenzenu. Nchi hii tunaipeleka wapi?

Wasaalamu.
 
Aeshy Khalfan Hilary ana miaka 38, alifukuzwa shule kidato cha pili akahamia shule gani sijui (wadau wataongezea). Alikuwa kwenye kikundi cha wahuni kilichokuwa kinajihusisha kuvuta bhangi, kutukana walimu na kubaka wasichana.

Mfanyabiashara wa sukari ya 'magendo' kutoka Zambia, na huko anadaiwa Dola 39,000 alizokopa kwa maandishi yake mwenyewe. Kesi imetolewa hukumu Mahakama Kuu Lusaka na hajajibu chochote. Sijui anajiamini nini?!
 
Mama Ananilea Nkya uko wapi mama, angalia kazi ndizo hizi jamii ya kitanzania inayotegemea ufanye, mko wapi mama.
 
Alifukuzwa shule ya sekondari Mazwi kwa utovu wa nidhamu, lakini kwa kuwa ni muda mrefu labda kabadilika na mambo hayo aliyafanya akiwa mwanafunzi. Ila kwa kweli jamaa hakubaliki hata ndani ya chama chake, bila "mtoto wa mkulima" asingekuwepo mjengoni!
 
Mama Ananilea Nkya uko wapi mama, angalia kazi ndizo hizi jamii ya kitanzania inayotegemea ufanye, mko wapi mama.

Alipelekewa taarifa hizi mapema akasema yuko bize.
Bosi wa TGNP naye alipelekewa pamoja na ushahidi mwingine, hawajafanya lolote zaidi ya kumwahidi source kwamba wangewasiliana naye.

Ni upuuzi mtupu kwa taasisi hizo ambazo ziko kimbelembele kupigia kelele unyanyasaji lakini zinapopelekewa taarifa kama hizo, ambazo zimefanyiwa kazi kikamilifu na watu, halafu wahhusika wanashindwa kuchukua hatua.

Lakini anyway, tusilaumu sana, huenda 'wamezungukiwa' maana jamaa yuko tayari kwa gharama yoyote kuzima skendo hiyo.

Taarifa zilizopo ni kwamba jamaa anatamba kwamba yuko tayari kwenda kupima DNA lakini kwa mbinu chafu, na kwamba atamuandaa kijana (inasemekana ameandaliwa tayari) na kumpatia kiasi cha Dola 500 ili ajitokeze na kusema kwamba yeye ndiye aliyempa mimba binti huyo.

Tamwa na TGNP wanataka wafanyiwe kazi gani, ama wanataka ushirikiano gani zaidi ya huu jamani?
 
JoachimLouis.png


Huyu ndiye baba mzazi wa binti mzee Joachim Louis. Haya si majungu.

Kuhusu kubadilika, jamaa hajabadilika kabisa, vinginevyo asingeweza kumfanyia kitu mbaya Mhindi kwa kumtuhumu kummega mkewe mwaka 2008.

Jamaa ni noma, hata wadogo zake nao ni viwembe kweli kweli na wanawafanyizia wanawake wa Kiafrika.

Taarifa zinasema pia kwamba yeye mwenyewe ni mtoto haramu! Pengine ndiyo maana anafanya mambo haya ya kiharamu haramu.

Nashangaa viongozi wengine wanapojitokeza na kumtetea kwamba eti hakumfanyia unyama yule Mhindi wakati mhusika mwenyewe yupo na mashahidi wapo, akiwemo kijana aliyekodiwa kwenda kumrubuni Mhindi huyo na kumfikisha mikononi mwa Aeshy na kundi lake.

Jamani, ifikie mahali haki itendeke, tusiwaonee haya wanaokwenda kinyume na haki za binadamu na maadili ya kiutu. Ni upumbavu kuia kuita chepeo kijiko!!
 

Attachments

  • Joachim Louis.png
    Joachim Louis.png
    29.4 KB · Views: 49
Aeshy Khalfan Hilary ana miaka 38, alifukuzwa shule kidato cha pili akahamia shule gani sijui (wadau wataongezea). Alikuwa kwenye kikundi cha wahuni kilichokuwa kinajihusisha kuvuta bhangi, kutukana walimu na kubaka wasichana.Mfanyabiashara wa sukari ya 'magendo' kutoka Zambia, na huko anadaiwa Dola 39,000 alizokopa kwa maandishi yake mwenyewe. Kesi imetolewa hukumu Mahakama Kuu Lusaka na hajajibu chochote. Sijui anajiamini nini?!
mwanzo niliielewa lakini unavyozidi kwenda inaonyesha kama majungu? Ukishaingiza mambo ya mahakama ya zambia sidhani kama ina ingia akilinisimamia moja
 
Alipelekewa taarifa hizi mapema akasema yuko bize.
Bosi wa TGNP naye alipelekewa pamoja na ushahidi mwingine, hawajafanya lolote zaidi ya kumwahidi source kwamba wangewasiliana naye.

Ni upuuzi mtupu kwa taasisi hizo ambazo ziko kimbelembele kupigia kelele unyanyasaji lakini zinapopelekewa taarifa kama hizo, ambazo zimefanyiwa kazi kikamilifu na watu, halafu wahhusika wanashindwa kuchukua hatua).

Not sure kwanini halijashughulikiwa lakini unapopeleka lalamiko, hakikisha complete information ziko na zaidi ya hapo "victim" awe tayari kutoa ushirikiano otherwise kesi itagonga mwamba. Mwenye full information please wapelekee TAWLA, ENVIROCARE etc. Au tupatie full info tuweze kuziwakilisha kwa wahusika. Nategemea victim kwenye hili pia hatatuangusha, akikubali kununuliwa then case itakua ngumu. Anyways lets see.
 
mwanzo niliielewa lakini unavyozidi kwenda inaonyesha kama majungu? Ukishaingiza mambo ya mahakama ya zambia sidhani kama ina ingia akilinisimamia moja
kuhusu mimba na kumlawiti mtu sio majungu ni ukweli ambao upo wazi na picha za kumlawiti mtu zipo zilipigwa washkaji wake na mmoja akazisambaza ili kumdhalilisha huyo jamaa aliyelawitiwa ila sasa jamaa aliyelawitiwa anogopa kusimama mahakamani kwa kuogopa aibu na alishakimbia mji yupo mbeya. kwa hilo la mahakama ya zambia ni jipya kwangu so siwezi nika-confirm au kukataaa.

huyo jamaaa bila order kutoka magogoni asingekuwa mbunge....coz pinda alipewa maelekezo kuwa kama mtu mwenye nguvu mkoa wa rukwa ahakikishe jimbo la sumbawanga mjini hilipotei so akafanya kila mbinu hadi matokeo yakageuzwa na mpaka sasa kuna kesi inaendelea kupinga matokeo ya uchaguzi.

concidence ni kuwa huyo mbunge (Aeshy) alikuwa anagombea jimbo na head master wake (nyamsebo) aliyemfukuza shule (sekondari Mazwi).
 
Back
Top Bottom