Mbunge wa Jimbo la Hai mh. Freeman Mbowe amewatembelea wakazi wa Mtaa wa Lerai wilayani Hai na kuwakuta wakiwa kwenye kikao cha kupanga mkakati wa kujenga Darasa katika shule ya sekondary lerai, Mbunge alipofika wananchi Hao walifarijika nakufurahi kumuona mbunge wao akiendelea kuwatembelea ambapo mbunge kama ilivyo kawaida kwake aliwapongeza wananchi kwa jitihada zao na kuwaambia wanachi wao yeye akiwa kama mwana Hai atachangia ujenzi wa darasa hilo na hatimae kuukamilisha.
Mbunge amewapa wakazi hao mchanga kwa ajili ya ujenzi wa shule , Matofali 1100 na tractor pamoja na mafuta kwa ajili ya kufanya shughuli hiyo. mbunge ametoa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni tatu amewasaidia wananchi hao na wameshukuru sana kwani wananchi wanasema mh. Mbunge amewapunguzia mzigo mkubwa sana ambao ulikuwa unawakabili wananchi.
Wananchi wamefurahi na kumpongeza mbunge huyo kwa kuendelea kuwakumbuka na kuwatembelea mara kwa mara. Huu ni utaratibu wa mh. Mbunge huyu kuwasaidia watu wake ambapo mpaka sasa ameshasaidia shughuli za maendeleo zenye thamani zaidi ya Tsh. Milioni mia tau tangu kuchaguliwa kwake.