Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,172
Diwani Chadema kuwania umeya Arusha

Imeandikwa na John Mhala, Arusha; Tarehe: 13th December 2010 @ 11:08

DIWANI wa Kata ya Kimandolu katika Jiji la Arusha, Estomi Mallah amepitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuwania kiti cha umeya wa jiji hilo.

Mallah aliyekuwa akitajwa kwa muda mrefu kuwania nafasi hiyo, alipitishwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya Chadema ya Wilaya ya Arusha kilichofanyika juzi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu wa Chadema wa Wilaya ya Arusha, Derick Magoma, Kamati ya Utendaji iliamua kupitisha jina la Mallah bila ya kipingamizi chochote baada ya kuungwa mkoani na wajumbe wote waliohudhuria kikao hicho.

Magoma alisema Kamati ya Utendaji ilizingatia vigezo mbalimbali kupitisha jina la mgombea huyo huku akitaja mojawapo ya kigezo kuwa ni uzoefu katika nafasi ya uongozi pamoja na uadilifu.

“Tumepitisha jina la Diwani wa Kata ya Kimandolu, Estomi Mallah, hivyo ule uvumi wa muda mrefu tumeukata mzizi na huyo ndiye atakayepeperusha bendera yetu katika kuwania kiti cha umeya wa jiji la Arusha,” alisema Magoma.

Mshindi wa kiti cha umeya wa Jiji Arusha atapatikana kwa wingi wa kura za wajumbe kutoka vyama tofauti huku Chadema ikifungana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wote kwa kuwa na wajumbe 14, wakati Tanzania Labour Party (TLP) ina kura moja ya diwani mmoja.

Chadema ina madiwani wanane, madiwani watatu wa Viti Maalumu, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini pamoja na wabunge wawili wa Viti Maalumu, wakati CCM ina wajumbe 14; madiwani 10, Mbunge wa Viti Maalumu na madiwani watatu wa Viti Maalumu.

Hata hivyo, kura moja ya TLP kupitia kwa diwani wake wa Kata ya Sokoni One, Michael Kivuyo, ndiyo huenda ikaamua kitendawili cha umeya wa jiji kwa upande atakaamua kuupigia kura. (tamati).

Caption Page 27 Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo akimkabidhi Meneja Mkuu Msaidizi wa Benki ya Exim, Vamadevan Sreeekuma (wa pili kushoto) tuzo ya utayarishaji mzuri wa hesabu ya mwaka 2009 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha.

Kushoto ni Meneja Mwandamizi wa benki hiyo, Lydia Kokugonza na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Silla. (Na Mpigapicha Maalumu).
 
Hadi sasa CCM ina kura 14 na Chadema ina kura 14 na ni diwani wa TLP ambaye ataamua ni nani kati ya CCM na Chadema kuubeba Umeya...............................CCM na makundi yao ni zigo jingine................wapo ambao hawaafiki na maamuzi ya kamti Kuu ya uteuzi wa mgombea wa nafasi hii.................................
 
hadi sasa ccm ina kura 14 na chadema ina kura 14 na ni diwani wa tlp ambaye ataamua ni nani kati ya ccm na chadema kuubeba umeya...............................ccm na makundi yao ni zigo jingine................wapo ambao hawaafiki na maamuzi ya kamti kuu ya uteuzi wa mgombea wa nafasi hii.................................

huyo wanamhonga tu kama zito siku ya siku aonekani kwenye uchaguzi anaarisha
kura zinapigwa hiyo ndio siasa aina adabu kabisa
 
Diwani Chadema kuwania umeya Arusha

Imeandikwa na John Mhala, Arusha; Tarehe: 13th December 2010 @ 11:08

DIWANI wa Kata ya Kimandolu katika Jiji la Arusha, Estomi Mallah amepitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuwania kiti cha umeya wa jiji hilo.

Mallah aliyekuwa akitajwa kwa muda mrefu kuwania nafasi hiyo, alipitishwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya Chadema ya Wilaya ya Arusha kilichofanyika juzi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu wa Chadema wa Wilaya ya Arusha, Derick Magoma, Kamati ya Utendaji iliamua kupitisha jina la Mallah bila ya kipingamizi chochote baada ya kuungwa mkoani na wajumbe wote waliohudhuria kikao hicho.

Magoma alisema Kamati ya Utendaji ilizingatia vigezo mbalimbali kupitisha jina la mgombea huyo huku akitaja mojawapo ya kigezo kuwa ni uzoefu katika nafasi ya uongozi pamoja na uadilifu.

"Tumepitisha jina la Diwani wa Kata ya Kimandolu, Estomi Mallah, hivyo ule uvumi wa muda mrefu tumeukata mzizi na huyo ndiye atakayepeperusha bendera yetu katika kuwania kiti cha umeya wa jiji la Arusha," alisema Magoma.

Mshindi wa kiti cha umeya wa Jiji Arusha atapatikana kwa wingi wa kura za wajumbe kutoka vyama tofauti huku Chadema ikifungana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wote kwa kuwa na wajumbe 14, wakati Tanzania Labour Party (TLP) ina kura moja ya diwani mmoja.

Chadema ina madiwani wanane, madiwani watatu wa Viti Maalumu, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini pamoja na wabunge wawili wa Viti Maalumu, wakati CCM ina wajumbe 14; madiwani 10, Mbunge wa Viti Maalumu na madiwani watatu wa Viti Maalumu.

Hata hivyo, kura moja ya TLP kupitia kwa diwani wake wa Kata ya Sokoni One, Michael Kivuyo, ndiyo huenda ikaamua kitendawili cha umeya wa jiji kwa upande atakaamua kuupigia kura. (tamati).

Caption Page 27 Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo akimkabidhi Meneja Mkuu Msaidizi wa Benki ya Exim, Vamadevan Sreeekuma (wa pili kushoto) tuzo ya utayarishaji mzuri wa hesabu ya mwaka 2009 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha.

Kushoto ni Meneja Mwandamizi wa benki hiyo, Lydia Kokugonza na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Silla. (Na Mpigapicha Maalumu).

Ili kushinda umeya kati ya CCM au CHADEMA waingie mkataba na MH Michael Kivuyo yeye awe Kaimu Meya ili kupata kura yake
 
Nina wasiwasi na kura ya diwani wa Themi kupitia CHADEMA. Huyu bwana alikamia sana nafai hii hivyo anaweza akaharibu kura kwa maksudi ili kumpisha wa CCM.
Lakini zaidi ni diwani wa Olorien (CCM) ambaye ni rafiki mzuri tu wa Lema. Hapa lazima patakuwa na tick tak za kuua mtu.
Nawashauri akina Ndesa na wengineo wapige kqmbi Arusha maana Mzee wa Mamvi hawezi kukubali ashindwe katika hili.......
 
Wandugu, sio kwamba jimbo la Arusha mjini lina madiwani 20? na hivyo kufanya...

CHADEMA ina kura 15(Mbunge 1 + wabunge 2 viti maalumu+madiwani 9+ madiwani viti maalimu 3 = 15

CCM 14 (mbunge viti maalumu 1 + madiwani 10 + madiwani viti maalumu 3 = 14

TLP diwani 1.

Therefore Kura zisipoharibika matokeo yatakuwa
a. CHADEMA 15, CCM 14 , TLP 1 au CCM+TLP =15

B CHADEMA 15, CCM+TLP 15 = Kuongoza kwa kuachiana

C . CHADEMA + TLP 16 na CCM 14

Au mimi nimekosea?

au
 
Hizi ni habari za kufurahisha sana tunasubiri kwa hamu kubwa sana ya kumpata Meya mteule wa jiji la Arusha Raha!
 
Diwani wa TLP alipigiwa debe na CHADEMA Since campaign HOPEFUL,ATATOA maamuzi ya busara
 
Kitimtimu kinaendelea Mjini Arusha baada ya CCM kuchakachua diwani mmoja kwa jina la Malo Sokoine na kujumlishwa kuwa mmoja wa madiwa wakuteuliwa kutoka Arusha ilihali si mkazi wa Arusha zaidi ya miaka mitano hivyo CCM kuwa na madiwa 15 tofauti na CHADEMA wenye jumla ya kura 14 hivy CCM imejiweka kwenye nafsi ya kuongoza Manispaa ya Arusha, uchanguzi unategemewa kufanyika tarehe 17-12-2010.. pamoja na hali hiyo CCM wana haha kuwatafuta madiwani wa CDM ili kuwa nunua au kuwakamatisha pesa za moto ilimradi wasiwepo siku ya uchaguzi hali ambayo imepelekea madiwani karibu wote kufishwa na chama chao (CDM) kwa hofu hiyo kwani inasemekana Lowasa kasha mwanga Mil 200 ili kuhakikisha Manispaa ya Arusha inakuwa chini ya CCM kwani ndipo vilipo vitega uchumi vyake, wasiwasi wa CCM unakuwepo hasa kutokana na mgawanyiko ulioko ndani ya Chama CCM wilaya ya arusha ambao uliongezeka baada ya aliekuwa mbunge Bw Mrema kuchakachuia na kambi ya Batilda inayoungwa mkono na Lowasa.... kama CDM watapata kura ya Bw Kivuyo diwani kupitia TLP kimahesabu watakuwa ngoma droo hivyo itategemea muasi yoyte kutoka chama chochote kati ya CDM na CCM kuunga mkono upande wa pili...kutokana na wasiwasi huo Kikwete natalajiwa kujua Arusha siku yoyote kabla ya uchanguzi ili kuongeza ushawishi huku CDM ikimtegemea Tindu Lisu kutua Arusha....
 
Sasa wanawanunua ya kazi gani na wakati wana madiwani 15 tayari. Kura si itakuwa 15-14?
 
Sasa wanawanunua ya kazi gani na wakati wana madiwani 15 tayari. Kura si itakuwa 15-14?
huja nisoma vizuri mkuu, wasiwasi wao ni kusalitiwa na baadhi ya madiwani kwani kuna baadhi yao wana uhusiano wa karibu kabisa na Mh Lema na swala pili ni mgawanyiko ulioko ndani ya CCM...
 
Ni lazima apige kura maana bila yeye matokeo yatakuwa droo kama ilivyokuwa Kigoma hadi waliamua kufanya umeya kwa zamu ya miaka 2 unusu
Asipo piga au akipigia CCM...Chadema watakuwa wameshidwa na hata akiwaunga mkono CDM bado ngoma itakuwa droo soma post hapo juu
 
Kitimtimu kinaendelea Mjini Arusha baada ya CCM kuchakachua diwani mmoja kwa jina la Malo Sokoine na kujumlishwa kuwa mmoja wa madiwa wakuteuliwa kutoka Arusha ilihali si mkazi wa Arusha zaidi ya miaka mitano hivyo CCM kuwa na madiwa 15 tofauti na CHADEMA wenye jumla ya kura 14 hivy CCM imejiweka kwenye nafsi ya kuongoza Manispaa ya Arusha, uchanguzi unategemewa kufanyika tarehe 17-12-2010.. pamoja na hali hiyo CCM wana haha kuwatafuta madiwani wa CDM ili kuwa nunua au kuwakamatisha pesa za moto ilimradi wasiwepo siku ya uchaguzi hali ambayo imepelekea madiwani karibu wote kufishwa na chama chao (CDM) kwa hofu hiyo kwani inasemekana Lowasa kasha mwanga Mil 200 ili kuhakikisha Manispaa ya Arusha inakuwa chini ya CCM kwani ndipo vilipo vitega uchumi vyake, wasiwasi wa CCM unakuwepo hasa kutokana na mgawanyiko ulioko ndani ya Chama CCM wilaya ya arusha ambao uliongezeka baada ya aliekuwa mbunge Bw Mrema kuchakachuia na kambi ya Batilda inayoungwa mkono na Lowasa.... kama CDM watapata kura ya Bw Kivuyo diwani kupitia TLP kimahesabu watakuwa ngoma droo hivyo itategemea muasi yoyte kutoka chama chochote kati ya CDM na CCM kuunga mkono upande wa pili...kutokana na wasiwasi huo Kikwete natalajiwa kujua Arusha siku yoyote kabla ya uchanguzi ili kuongeza ushawishi huku CDM ikimtegemea Tindu Lisu kutua Arusha....


Crashwise,
Umekuja na maneno mengi matamu ila yenye utata pia.
Ili kuondoa utata huo tunaomba utuwekee huo mchanganuo ulioongeza madiwani wa ccm na aliyetangaza ni nani.

Hii ni kw alengo zuri, tunataka Jf liwe jamvi lenye discussions zenye vielelezo. Udaku na mengoneyo ya aina hiyo tunawachia Shigongo na globalpublishers
 
Crashwise,
Umekuja na maneno mengi matamu ila yenye utata pia.
Ili kuondoa utata huo tunaomba utuwekee huo mchanganuo ulioongeza madiwani wa ccm na aliyetangaza ni nani.

Hii ni kw alengo zuri, tunataka Jf liwe jamvi lenye discussions zenye vielelezo. Udaku na mengoneyo ya aina hiyo tunawachia Shigongo na globalpublishers
Hata hapa JF kuna udaku pia kama hujui ila huu siyo udaku ndiyo maana sija post kwenye udaku soma post vizuri na mchanganuo umesha tolewa huko juu....
 
Back
Top Bottom