nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
TATIZO la udanganyifu wa umri na elimu limeibuka tena baada ya Mbunge wa Viti Maalumu kupitia UVCCM Zanzibar, Asha Muhamed Omar, kugundulika kuwa amefanya hivyo na kujipatia nafasi hiyo katika uchaguzi uliofanyika Agosti 2010.
Hayo yalisemwa na Tarehe Hamad wakati alipozungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam. Alisema kutokana na udanganyifu huo, wa umri na elimu aliweka pingamizi la kumpinga mgombea huyo, Asha ambaye hivi sasa ni mbunge.
"Asha Omari amechaguliwa wa nafasi ya ubunge kupitia Viti Maalumu UVCCM katika uchaguzi uliofanyika Dodoma Agosti 3, 2010 ambapo nilimuwekea pingamizi ili haki itendeke lakini hakuna hatua za kuridhisha zilizochukuliwa dhidi yake," alisema Tarehe.
Alisema kwa mujibu wa taratibu za UVCCM, kiongozi anatakiwa asizidi umri wa miaka 35 na elimu isiyokuwa chini ya kidato cha nne.
Alisema baada ya kufuatilia kwa karibu ndipo alipogundua kuwa katika utambulisho wa umri na elimu yake anatumia vyeti vya Asha Mohamed Omar wa Kiwani ambae ni mwalimu katika shule ya Pemba.
Alibainisha kuwa kinachoendelea ni ahadi toka kwa viongozi kuwa wangeshughulikia suala hilo lakini hadi leo hakuna hatua zozote za kuridhisha zilizochukuliwa zaidi ya mlalamikiwa kushawishi kulimaliza suala hilo nje ya vikao.
Hayo yalisemwa na Tarehe Hamad wakati alipozungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam. Alisema kutokana na udanganyifu huo, wa umri na elimu aliweka pingamizi la kumpinga mgombea huyo, Asha ambaye hivi sasa ni mbunge.
"Asha Omari amechaguliwa wa nafasi ya ubunge kupitia Viti Maalumu UVCCM katika uchaguzi uliofanyika Dodoma Agosti 3, 2010 ambapo nilimuwekea pingamizi ili haki itendeke lakini hakuna hatua za kuridhisha zilizochukuliwa dhidi yake," alisema Tarehe.
Alisema kwa mujibu wa taratibu za UVCCM, kiongozi anatakiwa asizidi umri wa miaka 35 na elimu isiyokuwa chini ya kidato cha nne.
Alisema baada ya kufuatilia kwa karibu ndipo alipogundua kuwa katika utambulisho wa umri na elimu yake anatumia vyeti vya Asha Mohamed Omar wa Kiwani ambae ni mwalimu katika shule ya Pemba.
Alibainisha kuwa kinachoendelea ni ahadi toka kwa viongozi kuwa wangeshughulikia suala hilo lakini hadi leo hakuna hatua zozote za kuridhisha zilizochukuliwa zaidi ya mlalamikiwa kushawishi kulimaliza suala hilo nje ya vikao.