Kwani familia yake haipo mbona unachekeshaOna sasa, huyu yuko taabani tangu mwaka jana, lakini posho ya mafuta analipwa kila siku!
Tunamwombea apone haraka, lakini hapa tunajifunza kitu gani, unafiki wa CCM kujifanya wanawapenda sana viongozi wao huku wakiwaacha wananchi hasa wa jimbo lake wakihangaika bila mwakilishi, naomba akirudi awe amepona au...aapishwe ili aendelee kupokea posho hadi bunge livunjwe mwaka 2015 kama katiba inavyosema.Ubinadamu mbele namtakia asafiri salama na Mwenye enzi Mungu ampe baraka apone na kurudia afya yake. Masikini watu wa jimbo lake wamekaa miezi mingi bila mwakilishi wao kufika bungeni, hata kule kluapishwa tu, sijui CCM yetu ilianfgalia wapi ikachagua mgombea mgonjwa!! Ushauri wa bure, akipata nafuu ajiuzuru ubunge kutoa nafasi uchaguzi kurudiwa na wengine wagombee na kuwapa uiwakilishi wananchi.
unaelewa maana ya RIP?
Kwani familia yake haipo mbona unachekesha
Mungu amponye mzee Sumari!Naomba kujulishwa kama huyu mheshimiwa aliwahi kuapishwa kwenye bunge hili la Makinda..!
Umeielewa post ya kwanza mkuu?
kama alichaguliwa halali na wananchi wake mungu amjalie apone haraka,kama aliiba kura kama walivyozoea na chama chake mungu amuwaishe mbinguni akajibu kesi yake
Tunashukuru kwa taarifa yako, na tumwombee Mungu amjalie afya njema arudi kuliwakilisha jimbo lake na kuendelea utumishi wake kwa taifa.
Tofauti za kiitikadi si chuki kama wengi wetu tulivyozoea kuziendesha hapa, tunashindana kwa hoja ndio maana ya demokrasi, lakini wakati huo huo tunatakiwa kudumisha utu na upendo kati yetu ndiyo silaha kubwa ya kutunza amani katika nchi yetu.
Sawasawa kabisa, hospitali za India kwa sasa ndio zimekua hospitali zetu kubwa za rufaa! Why not? Tuko busy na kuponda hela kusherekea miaka 50 ya uhuru, hatuna pesa za kurekebisha na kununua vifaa vya kisasa Muhimbili, sisi sio wajinga bwana, we know what we are doing!
Pasco, utu haupimwi kwa kumhurumia mgonjwa tuangalie pia upande wa pili anaowawakilisha, alipogundua kuwa anaumwa na hawezi kuwahudumia kwa nini hajiuzulu kupisha mwingine, ina maana yeye hawahurumii akina mama wajawazito pale Tengeru wanaosumbuka kupanda bajaji kwa kukosa mwakilishi bungeni?Halisi, asante kwa taarifa hii.
Wana jf wenzangu, hawa hate preachers humu, wasio na ubinaadamu, wataifikisha jf pabaya!.
Kama alivyosisitiza Halisi, utu na ubinaadamu mbele.
Get well soon Mhe. Jerry Solomon!.
Pasco.
Japo magamba siwapendi lakini kama binadamu tunamtakia heri apone haraka aje kutekeleza ahadi alizo ahidi kwenye kampeni.
Pipoz power!
Pasco, utu haupimwi kwa kumhurumia mgonjwa tuangalie pia upande wa pili anaowawakilisha, alipogundua kuwa anaumwa na hawezi kuwahudumia kwa nini hajiuzulu kupisha mwingine, ina maana yeye hawahurumii akina mama wajawazito pale Tengeru wanaosumbuka kupanda bajaji kwa kukosa mwakilishi bungeni?
Ugua pole Sumari
Sasa kama haelewi unafikiri ameandikiwa?