Mgoyangi
Senior Member
- Feb 6, 2008
- 184
- 9
Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya Mwaka 2009 iliyosainiwa kwa mbwe mbwe na Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete ambayo ina lengo lake ni kudhibiti vitendo vinavyoonekana kuwa rushwa, imetahiniwa na Mbunge wa Solwa CCM - Ahmed Salum, ambaye ametoa magari mawili ya wagonjwa kama msaada kwa wananchi ikiwa ni siku chache baada ya sheria hiyo kutangazwa kuwa ianze kutumika.
Akifungua Mkutano wa kazi wa mwaka wa TAKUKURU, jijini Mwanza, Rais Kikwete katika hatua ya kutangaza nia yake ya kidhinisha sheria hiyo kwa mbwembwe alihoji vitendo kama hivi, kwamba kwa nini iwe sasa hivi, wakati tukielekea uchaguzi mkuu na isiwe kabla.
Lakini Mbunge huyu wa Solwa kaamua kuweka pamba Masikioni na kutoa misaada hii, ukiacha kampeni yake ya kuingiza wananchama wapya kwa kuwanunulia kadi na semina za hapa na pale na posho mbali mbali kwa wapambe.
Akifungua Mkutano wa kazi wa mwaka wa TAKUKURU, jijini Mwanza, Rais Kikwete katika hatua ya kutangaza nia yake ya kidhinisha sheria hiyo kwa mbwembwe alihoji vitendo kama hivi, kwamba kwa nini iwe sasa hivi, wakati tukielekea uchaguzi mkuu na isiwe kabla.
Lakini Mbunge huyu wa Solwa kaamua kuweka pamba Masikioni na kutoa misaada hii, ukiacha kampeni yake ya kuingiza wananchama wapya kwa kuwanunulia kadi na semina za hapa na pale na posho mbali mbali kwa wapambe.