Mbunge Peter Msigwa aichana Kamati ya manunuzi kwa mswaada mbovu!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Mh Peter Msigwa amewachana kamati nzima ya manunuzi kuleta mswaada Bungeni wenye pendekezo wa ununuzi vifaa chakavu kama Meli,Ndege,Mabehewa,na Matrain!!
Mpaka wabungi wa CCM wamenywea mpaka Mkullo ameinamisha kichwa!!
 
Mwenyekiti wa hiyo kamati ni nani hasa? Bunge letu lina historia ya kupitisha sheria za aibu kwa mfano ile ya Takrima! Tatizo la mabehewa matumba linaeleweka vyema baada ya experience ya RITES, sasa inakuwaje watu wazima na akili timamu watake kuweka sheria ya kununua mitumba? Wana wazimu?
 
mkiambiwa serikali imefilisika mnakataa iweje tununue used item? kama pesa tunayo......hata fifaru pia
 
hivi kama nchi inanunua vichakavu tenda kwa kutangaza bila aibu, hata huduma si tunapewa chakavu?? Na wanajua hata hospital chakavu ndio maana wanakimbilia India.
 
Msigwa anatisha: ameliambia bunge kwamba
..you better run inches in right direction than running miles in wrong way...kitendo cha kununua vifaa chakavu cheaper baadae inaweza ikawa gharama kubwa kwa taifa kuliko kununua vipya atakama gharama yake iko juu..
 
Muleta maada ungesatupa uhondo huo japo kwa ufupi ulivyochana Mbunge wa Iringa mjini ili nasi tusiopata kuona wala kusikia yanayoendelea bungeni tuwe karibu zaidi.
 
Msigwa anatisha: ameliambia bunge kwamba
..you better run inches in right direction than running miles in wrong way...kitendo cha kununua vifaa chakavu cheaper baadae inaweza ikawa gharama kubwa kwa taifa kuliko kununua vipya atakama gharama yake iko juu..

Ahsante mkuu!! Nimepata point ya mchungaji Peter!!
 
A good thing about CDM mps ni kwamba kila mbunge ni kichwa b4 dr slaa alichanguliwa na chama kugombea upresident tulijua hakuna mbunge mwenye hoja nzito kama yy but now CDM imekuwa hatari zaidi maana kila mbunge amekuwa kichwa badala ya kuacha fulani aongee hii inaonyesha kwamba hata kama leo kiongozi yeyote akiondoka chama hakitatetereka maana vichwa vipo vya kutosha achilia mbali hivi vya mtaani vinavyosubr hiyo 2015...big up Mchungaji...big up CDM!
 
Msigwa anatisha: ameliambia bunge kwamba
..you better run inches in right direction than running miles in wrong way...kitendo cha kununua vifaa chakavu cheaper baadae inaweza ikawa gharama kubwa kwa taifa kuliko kununua vipya atakama gharama yake iko juu..

Hivi tutaendelea kula matapishi yetu wenyewe mpaka lini?
 
Huo ni kati ya miswada ya kipuuzi kabisa. Serikali itajihalalishiaje kununua mitumba? Wanataka tu wapate njia za kutuuzia makanyabwoya ili wale pesa ya walipa kodi. I wish this government would go to hell.
 
tunataka wawakiishi wa aina hii wenye kujali maslahi ya wanyonge,tumechoshwa kuwa taifa la dharura,bora baba Ridh atangaze rasmi jina jipya la taifa letu ni TANZADHARURA,hapo tutamuelewa.Nchi hii si kichwa cha mwendawazimu,kila kinyozi anajifunza,mpaka lini tutawavumilia ilihali wameshindwa.Ni madhumuni ya serikali kuja na muswada wa kununuwa vichakavu nini hatima yake?lengo ni kuunda tume mara baada ya matokeo ya vichakavu vyao?kwanini tunaweka rehani maisha ya wapiga kura wenu,Kosa la wapiga kura hawa ni kuwachagua?Tunataka viongozi wenye uchungu na taifa hili,magamba wameshachoka na sisi,kuongoza miaka hamsini si mchezo ndo maana uchakavu wa fikra unajidhihirisha.Wakati mwingine nashindwa kuamini kama kweli hawa watawala wana umakini kiasi gani.Siamini kama kweli wanakutana katika kikao cha baraza la mawaziri na kupresent mada zao,kabla ya kukurupuka na kunotice kwa wananchi.Na kama ni kweli wanakaa na kukubaliana basi kuna ombwe kubwa la uongozi,ambalo linahitaji think capacity ambayo hawa jamaa wameikosa.Mungu tusaidie wananchi tuepukane na kikombe hiki.Tanzania is not the dumping place!kwanini tuwe na sheria ya kununua uchafu?
 
Huyu na yeye anawaambia ukweli...........why tununue vitu used, ina maana hatuna hela si ndio??
 
Hela zinatumiwa vibaya kwa kuwalipa watu posho at the end of the day tunanunua vitu used........
 
Aisee kweli Mh mchungaji Msigwa kichwa,wabunge wote wa CCM kimya,hi nchi tunaipeleka wapi jamani mbona CCM imesharibu nchi,ukombozi wa pili unahitajika.
 
YANI SIJUI NASEMA SIJUI!!!Hii nchi ya watanzania siielewi sasa sijui watanzania ndo tulivyo??au ni ukomo wakufikiria??au tumelogwaaa??mimi sinajibu!!Haiwezekani tusimame mbele ja jamii yakimataifa kwakusema tumepitisha mswaada kwa kununu used items!!mbele ya jamii ya kimataifa tutachekwa kama tulinunua used items wakati wa nyerere serikali haikuwa na hela!!kipindi tunapigania uhuru!Leo miaka 50 tunajadiri kununua Used Items????kweli mimi nilipo ninaumwa nakichwa kwakuwaza hawa wawakilishi wetu kwakutojua wanatupeleka wapi!!Nawaomba wabunge mnaopitia humu jamani msikubali kupitisha huu uhoza wa mswada wamafisadi na msitumike kama mihuri jamani!!Nimeshangaa hata mawaziri Mh Nundu,Mwanri hapana nanilichokiona hapa wabunge wachama tawala wanshindwa kwakuwa wanaogopa kusutwa kwenyekikao maana ukiona unamsimamo ujue next term haupo wanakuwekea zengwe lakini unawaona wandhamila yakutaka kuukataa ila wanashindwa naile kasumba ya ntaonekanaje kwenye chama changu!!!Upuuzi huu mimi naweza kuuita kama ndege ya Rais natukaambiwa hata nyasi tutakula like donkey!1leo mnashindwa kununua vitu vipya??nasema sasa hii serikali imefirisika kifikira hata kiutendaji!!Wakati umefika watanzania wenzangu wakuiondoa serikali kwanjia ya Box la kura hakuna kingine!!maana kesho tutalishwa chakula kilicho expire kwakuwa kinabei ndogo!!!
 
Hii mipango yote wanalenga kununua Dowans tu, hakuna jingine
 
Back
Top Bottom