Elections 2010 Mbunge mteule CCM Shinyanga alindwa na Polisi

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
5,471
733
Ana kweli madaraka yana gharama zake, mbunge mteule wa CCM jimbo Shinyanga mjini akiyepita kimazabe analindwa na ulinzi mkali wa polisi sasa sijui watamlinda mpaka lini na watawalinda wengi sana kama yule wa Tarime...
 
Naona sasa wabadilishe yale maneno yanayoambatana na nembo ya polisi kutoka 'Usalama wa Raia' na kusomeka 'Usalama wa Wabunge':doh:
 
Yule atavuna alichokipanda alifikiri JK na Ridhiwani atakuwepo maisha shy town.Yule atakiona cha moto amedhurumu haki ya watu awaulize vikongwa wa huko ndiyo atajua adha ya kula cha mtu.
 
Hivi kama alishinda kwa halali si ina maana anao watu wengi wanaomuunga mkono? Aliyechaguliwa kihalali na wapiga kura hulindwa na kupendwa kwake na waliompa kura sasa yeye waliompa kura wako wapi mpaka alindwe na polisi?
 
Eeee amekoma tena kama mnaweza polisi msimlinde huyo mchakachuaji
mkubwa .
 
labda aendelee kulindwa hivyo hivyo, vinginevyo vijana watamshukia kama eagle anavyoweza kushuka ardhini ghafla na kuchukua mawindo yake. Gharama ya kuchakachua tayari ameanza kuilipa. atakiona cha mtema kuni.
 
na analindwa na polisi wakutoka nje ya Shinyanga. CCM Inadai polisi wa hapa shinyanga ni wamekisaliti chama, wanataka wachukuliwe hatua kali.
 
na analindwa na polisi wakutoka nje ya Shinyanga. CCM Inadai polisi wa hapa shinyanga ni wamekisaliti chama, wanataka wachukuliwe hatua kali.

Haya bwana! Ingawa naamini hujui ulisemalo!
 
Back
Top Bottom