Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Suzy Butondo na Shija Felician, Shinyanga
MBUNGE wa jimbo la Bukombe mkoani hapa, Emmanuel Luhahula juzi alivamiwa na majambazi waliompora fedha taslimu na vitu vingine, ikiwemo bastola ambayo aliporwa baada ya kushindwa kuitumia.
Kabla ya uporaji huo, majambazi hayo yalimshambulia mbunge huyo pamoja na katibu wa CCM wa wilaya ya Bukombe, Mberito Magova, ambaye alikuwa akisafiri naye, kwa kuwakata na mapanga
Kwa mujibu wa habari hizo mbali na bastola hiyo majambazi hao pia walimpora mbunge huyo fedha taslimu takriban Sh14 milioni zilizokuwa katika dola 10,000 za Kimarekani na Sh50,000 za Kitanzania pamoja na simu mbili za mkononi.
Kabla ya kuwapora mali hizo, majambazi hao waliwashambulia viongozi hao wa chama na serikali kwa kuwakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili. Imesemekana kuwa dereva wao alifanikiwa kuwakimbia watekaji hao.
Katibu wa CCM, Mberito Magova aliliambia gazeti hili jana kuwa walikutwa mkasa huo majira ya saa 3.15 usiku wa kuamkia jana kwenye eneo la Kijiji cha Nasikukulu wilayani Bukombe wakati walipokuwa wanatokea Kahama kwenda Bukombe.
Alisema walipokaribia eneo la tukio walikuta mawe barabarani na kulazimika kusimama na ndipo majambazi hao sita walipowavamia na kuwapiga.
Tukiwa hatujui tufanye nini, majambazi hao walituteka na kutuamuru kuteremka; ile kushuka tu, walianza kutushambulia kwa kutupiga marungu na mapanga, alieleza katibu huyo wa CCM.
Alisema mbuge huyo alijaribu kupiga risasi hewani ili kuwatishia majambazi hao wakimbie, lakini risasi ziligoma na ndipo waporaji walipompora bastola na baadaye kuwanyanganya simu za mikononi na fedha.
Baada ya kumpora bastola mbunge, majambazi hao walianza kuitumia papo hapo... walifyatua risasi hewani na kuteka magari mengine yaliyokuwa yakitokea Kahama kuelekea Bukombe, alieleza Magova.
Alisema katika uvamizi huo yeye (Magova) alijeruhiwa kichwani na ameshonwa nyuzi tano. Alisema amepata maumivu zaidi miguuni na maeneo mengine ya mwili.
Mheshimiwa mbunge alikatwa panga sehemu za kichwani, mkono wake wa kulia wakati akiporwa bastola na mgongoni, lakini hali yake siyo mbaya sana, japo hivi tunapoongea (saa 4.59 asubuhi) alikuwa bado yupo chumba cha upasuaji akipatiwa matibabu, alieleza.
Alisema yeye na mbunge huyo wote walipatiwa matibabu Hospitali ya Wilaya ya Bukombe, Shinyanga.
Alisema katika tukio hilo majambazi hao pia walitumia bastola ya mbunge huyo kuteka lori na katika purukushani hizo, ndipo waliwatoroka na kukimbilia porini ambako baadaye waliomba msaada.
Bahati nzuri dereva wetu alipata gari lililopenya katika kizuizi hicho na kwenda kutoa taarifa kwa polisi wa Bukombe ambao walifika na kutoa msaada zaidi, alieleza Magova.
Alisema baada ya muda mfupi, polisi pamoja na wanakijiji walifika eneo hilo na ndipo walipokimbizwa hospitalini.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daudi Siasi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini akasema hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa na wanaendelea na msako wa watu waliohusika
SOURCE: Mwananchi
MBUNGE wa jimbo la Bukombe mkoani hapa, Emmanuel Luhahula juzi alivamiwa na majambazi waliompora fedha taslimu na vitu vingine, ikiwemo bastola ambayo aliporwa baada ya kushindwa kuitumia.
Kabla ya uporaji huo, majambazi hayo yalimshambulia mbunge huyo pamoja na katibu wa CCM wa wilaya ya Bukombe, Mberito Magova, ambaye alikuwa akisafiri naye, kwa kuwakata na mapanga
Kwa mujibu wa habari hizo mbali na bastola hiyo majambazi hao pia walimpora mbunge huyo fedha taslimu takriban Sh14 milioni zilizokuwa katika dola 10,000 za Kimarekani na Sh50,000 za Kitanzania pamoja na simu mbili za mkononi.
Kabla ya kuwapora mali hizo, majambazi hao waliwashambulia viongozi hao wa chama na serikali kwa kuwakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili. Imesemekana kuwa dereva wao alifanikiwa kuwakimbia watekaji hao.
Katibu wa CCM, Mberito Magova aliliambia gazeti hili jana kuwa walikutwa mkasa huo majira ya saa 3.15 usiku wa kuamkia jana kwenye eneo la Kijiji cha Nasikukulu wilayani Bukombe wakati walipokuwa wanatokea Kahama kwenda Bukombe.
Alisema walipokaribia eneo la tukio walikuta mawe barabarani na kulazimika kusimama na ndipo majambazi hao sita walipowavamia na kuwapiga.
Tukiwa hatujui tufanye nini, majambazi hao walituteka na kutuamuru kuteremka; ile kushuka tu, walianza kutushambulia kwa kutupiga marungu na mapanga, alieleza katibu huyo wa CCM.
Alisema mbuge huyo alijaribu kupiga risasi hewani ili kuwatishia majambazi hao wakimbie, lakini risasi ziligoma na ndipo waporaji walipompora bastola na baadaye kuwanyanganya simu za mikononi na fedha.
Baada ya kumpora bastola mbunge, majambazi hao walianza kuitumia papo hapo... walifyatua risasi hewani na kuteka magari mengine yaliyokuwa yakitokea Kahama kuelekea Bukombe, alieleza Magova.
Alisema katika uvamizi huo yeye (Magova) alijeruhiwa kichwani na ameshonwa nyuzi tano. Alisema amepata maumivu zaidi miguuni na maeneo mengine ya mwili.
Mheshimiwa mbunge alikatwa panga sehemu za kichwani, mkono wake wa kulia wakati akiporwa bastola na mgongoni, lakini hali yake siyo mbaya sana, japo hivi tunapoongea (saa 4.59 asubuhi) alikuwa bado yupo chumba cha upasuaji akipatiwa matibabu, alieleza.
Alisema yeye na mbunge huyo wote walipatiwa matibabu Hospitali ya Wilaya ya Bukombe, Shinyanga.
Alisema katika tukio hilo majambazi hao pia walitumia bastola ya mbunge huyo kuteka lori na katika purukushani hizo, ndipo waliwatoroka na kukimbilia porini ambako baadaye waliomba msaada.
Bahati nzuri dereva wetu alipata gari lililopenya katika kizuizi hicho na kwenda kutoa taarifa kwa polisi wa Bukombe ambao walifika na kutoa msaada zaidi, alieleza Magova.
Alisema baada ya muda mfupi, polisi pamoja na wanakijiji walifika eneo hilo na ndipo walipokimbizwa hospitalini.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daudi Siasi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini akasema hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa na wanaendelea na msako wa watu waliohusika
SOURCE: Mwananchi