kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, amevamiwa na wezi katika nyumba ya kulala wageni na kuibiwa fedha taslimu pamoja na kila kitu alichokuwa nacho chumbani kwake.
Tukio hilo lilitokea juzi katika nyumba ya kulala wageni ya Sangos Lodge, iliyoko mjini hapa, saa 8.00 usiku wakati Mchungaji Msigwa akiwa amelala.
Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge walioko katika ziara ya operesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Tayari Mchungaji Msigwa ameripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha mjini hapa, ambako jalada namba SUM/RB/3087/2011 limefunguliwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mchungaji Msigwa, alisema wakati akiwa amelala, wezi hao walivamia nyumba hiyo na kisha wakafungua dirisha la chumba alichokuwa amepanga. Alisema baada ya kufungua dirisha hilo, waliiba pochi iliyokuwa na vitu hivyo pamoja na fedha taslimu Sh. 400,000.
Alivitaja vitu vingine vilivyoibwa kuwa ni kitambulisho cha ubunge na simu mbili za mkononi ikiwemo moja inayofanyakazi kama kompyuta, vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 1.2.
Kati ya simu hizo, moja ni Iphone (simu ya kompyuta). Hiyo, niliinunua kwa Dola za Marekani 900. Ilikuwa na picha zangu nyingi, alisema Mchungaji Msigwa.
Vitu vingine vilivyoibwa, alisema ni leseni ya udereva, kadi za benki na waraka wa huduma ya lipa umeme kadri unavyotumia (Luku).
Mchungaji Msigwa alisema alifika wilayani Sumbwanga siku hiyo saa 6:00 usiku na kukuta vyumba katika nyumba karibu zote za kulala wageni za mjini humo vikiwa vimejaa wageni.
Alisema kutokana na hali hiyo, muda huo alilazimika kwenda nje ya mji kutafuta vyumba katika nyumba nyingine za kulala wageni na kufanikiwa kupanga katika nyumba hiyo.
CHANZO: NIPASHE
Tukio hilo lilitokea juzi katika nyumba ya kulala wageni ya Sangos Lodge, iliyoko mjini hapa, saa 8.00 usiku wakati Mchungaji Msigwa akiwa amelala.
Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge walioko katika ziara ya operesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Tayari Mchungaji Msigwa ameripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha mjini hapa, ambako jalada namba SUM/RB/3087/2011 limefunguliwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mchungaji Msigwa, alisema wakati akiwa amelala, wezi hao walivamia nyumba hiyo na kisha wakafungua dirisha la chumba alichokuwa amepanga. Alisema baada ya kufungua dirisha hilo, waliiba pochi iliyokuwa na vitu hivyo pamoja na fedha taslimu Sh. 400,000.
Alivitaja vitu vingine vilivyoibwa kuwa ni kitambulisho cha ubunge na simu mbili za mkononi ikiwemo moja inayofanyakazi kama kompyuta, vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 1.2.
Kati ya simu hizo, moja ni Iphone (simu ya kompyuta). Hiyo, niliinunua kwa Dola za Marekani 900. Ilikuwa na picha zangu nyingi, alisema Mchungaji Msigwa.
Vitu vingine vilivyoibwa, alisema ni leseni ya udereva, kadi za benki na waraka wa huduma ya lipa umeme kadri unavyotumia (Luku).
Mchungaji Msigwa alisema alifika wilayani Sumbwanga siku hiyo saa 6:00 usiku na kukuta vyumba katika nyumba karibu zote za kulala wageni za mjini humo vikiwa vimejaa wageni.
Alisema kutokana na hali hiyo, muda huo alilazimika kwenda nje ya mji kutafuta vyumba katika nyumba nyingine za kulala wageni na kufanikiwa kupanga katika nyumba hiyo.
CHANZO: NIPASHE