Mbunge akombwa kila kitu gesti

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, amevamiwa na wezi katika nyumba ya kulala wageni na kuibiwa fedha taslimu pamoja na kila kitu alichokuwa nacho chumbani kwake.
Tukio hilo lilitokea juzi katika nyumba ya kulala wageni ya Sangos Lodge, iliyoko mjini hapa, saa 8.00 usiku wakati Mchungaji Msigwa akiwa amelala.
Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge walioko katika ziara ya operesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Tayari Mchungaji Msigwa ameripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha mjini hapa, ambako jalada namba SUM/RB/3087/2011 limefunguliwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mchungaji Msigwa, alisema wakati akiwa amelala, wezi hao walivamia nyumba hiyo na kisha wakafungua dirisha la chumba alichokuwa amepanga. Alisema baada ya kufungua dirisha hilo, waliiba pochi iliyokuwa na vitu hivyo pamoja na fedha taslimu Sh. 400,000.
Alivitaja vitu vingine vilivyoibwa kuwa ni kitambulisho cha ubunge na simu mbili za mkononi ikiwemo moja inayofanyakazi kama kompyuta, vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 1.2.
“Kati ya simu hizo, moja ni ‘Iphone’ (simu ya kompyuta). Hiyo, niliinunua kwa Dola za Marekani 900. Ilikuwa na picha zangu nyingi,” alisema Mchungaji Msigwa.
Vitu vingine vilivyoibwa, alisema ni leseni ya udereva, kadi za benki na waraka wa huduma ya lipa umeme kadri unavyotumia (Luku).
Mchungaji Msigwa alisema alifika wilayani Sumbwanga siku hiyo saa 6:00 usiku na kukuta vyumba katika nyumba karibu zote za kulala wageni za mjini humo vikiwa vimejaa wageni.
Alisema kutokana na hali hiyo, muda huo alilazimika kwenda nje ya mji kutafuta vyumba katika nyumba nyingine za kulala wageni na kufanikiwa kupanga katika nyumba hiyo.
CHANZO: NIPASHE
 
pole sana mchungaji, police jjitahidini kufanya uchunguz na muwafikishe mahakan watuhumiwa wote ili nao wapate haki yao..
 
Pole mchungaji
ila nafurahi vyote vinalipika kwa mshahara wenu mmoja.....,
 
Pole sana mchungai mungu asaidie hao wezi waliotumwa na magamba kudhohofisha maandamano wakamatwe
 
Pole sana Mchungaji Msigwa, mapambano yaendelee kama kawaida, inawezekana CCM wametuma vibaka wao ili waichukue hiyo iphone ili kupata taarifa za chama. Isije kuwa CCM walifanya uhuni ambao haukugundulika mara moja kuhakikisha unapata chumba cha kulala nje ya mji mahali ambapo security wise yake si nzuri in general
 
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, amevamiwa na wezi katika nyumba ya kulala wageni na kuibiwa fedha taslimu pamoja na kila kitu alichokuwa nacho chumbani kwake.
Tukio hilo lilitokea juzi katika nyumba ya kulala wageni ya Sangos Lodge, iliyoko mjini hapa, saa 8.00 usiku wakati Mchungaji Msigwa akiwa amelala.
Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge walioko katika ziara ya operesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Tayari Mchungaji Msigwa ameripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha mjini hapa, ambako jalada namba SUM/RB/3087/2011 limefunguliwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mchungaji Msigwa, alisema wakati akiwa amelala, wezi hao walivamia nyumba hiyo na kisha wakafungua dirisha la chumba alichokuwa amepanga. Alisema baada ya kufungua dirisha hilo, waliiba pochi iliyokuwa na vitu hivyo pamoja na fedha taslimu Sh. 400,000.
Alivitaja vitu vingine vilivyoibwa kuwa ni kitambulisho cha ubunge na simu mbili za mkononi ikiwemo moja inayofanyakazi kama kompyuta, vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 1.2.
“Kati ya simu hizo, moja ni ‘Iphone’ (simu ya kompyuta). Hiyo, niliinunua kwa Dola za Marekani 900. Ilikuwa na picha zangu nyingi,” alisema Mchungaji Msigwa.
Vitu vingine vilivyoibwa, alisema ni leseni ya udereva, kadi za benki na waraka wa huduma ya lipa umeme kadri unavyotumia (Luku).
Mchungaji Msigwa alisema alifika wilayani Sumbwanga siku hiyo saa 6:00 usiku na kukuta vyumba katika nyumba karibu zote za kulala wageni za mjini humo vikiwa vimejaa wageni.
Alisema kutokana na hali hiyo, muda huo alilazimika kwenda nje ya mji kutafuta vyumba katika nyumba nyingine za kulala wageni na kufanikiwa kupanga katika nyumba hiyo.
CHANZO: NIPASHE
Pole sana mchungaji ila pokea hiyo kama changamoto sisi hayo yanatupata kila siku kwa vile hayafiki kwenye vyombo vya habari. Natumai kwamba utawatetea pamoja na hao vibaka wanakesha kusaka kwa njia za haramu kwa kukosa mambo muhimu ya kufanya mchana kwani ukali wa maisha unasikika zaidi kwa maskini.
 
Vijana wanaiba, wanakaba, wafanye nini sasa wakati maisha yamekuwa tight! Hakuna pakupumulia.
 
Pole sana Mpiganaji wetu Mchungaji !

Hii yote ni shauri ya CCM kulea wezi na majambazi. Badala ya watoto wetu kwenda shuleni, wako mitaani kwa kukosa ada, madawati na waalimu. Na hata wale waliomaliza elimu, wako mitaani hawana kazi !Haya sasa, bila kuiondoa CCM madarakani, Tanzania itaendelea kuwa nchi ya majanga tu ! Endelezeni mapambano huko Songea mpaka kieleweke !
 
Pole mchungaji.

Endelea na kupambana,hilo lililokutokea ni mojawapo ya maozo ya serikali kulea wezi na magenge ya majambazi; system ni kubwa mno.
 
Mchungaji gani huyo kaachwa na Mlupo wa pale pale katika hiyo hotel na isitoshe Mlupo wenyewe ushasepa zake Tunduma kitambo baada ya tukio tupunguze zinaa ehhh! Hata watumishi wa mungu! Hatariii
 
Pole sana Mchungaji Msigwa, mapambano yaendelee kama kawaida, inawezekana CCM wametuma vibaka wao ili waichukue hiyo iphone ili kupata taarifa za chama. Isije kuwa CCM walifanya uhuni ambao haukugundulika mara moja kuhakikisha unapata chumba cha kulala nje ya mji mahali ambapo security wise yake si nzuri in general

Red: Unawaza mbali sana na ninapenda sana watu wa namna yako. I wish wapiganaji tuwe na intelijensia iliyokwenda shule na inafuatilia mienendo yote michafu ya kuzolotesha harakati hizi za ukombozi. Naunga hoja kiongozi
 
duh, kila baya linalotokea bongo ni ccm..tumekosa vya kusingizia mazee? japo siipend ccm lakn siyo kihivyo duh!
 
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, amevamiwa na wezi katika nyumba ya kulala wageni na kuibiwa fedha taslimu pamoja na kila kitu alichokuwa nacho chumbani kwake.
Tukio hilo lilitokea juzi katika nyumba ya kulala wageni ya Sangos Lodge, iliyoko mjini hapa, saa 8.00 usiku wakati Mchungaji Msigwa akiwa amelala.
Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge walioko katika ziara ya operesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Tayari Mchungaji Msigwa ameripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha mjini hapa, ambako jalada namba SUM/RB/3087/2011 limefunguliwa.
Akizungumza na NIPASHE jana, Mchungaji Msigwa, alisema wakati akiwa amelala, wezi hao walivamia nyumba hiyo na kisha wakafungua dirisha la chumba alichokuwa amepanga. Alisema baada ya kufungua dirisha hilo, waliiba pochi iliyokuwa na vitu hivyo pamoja na fedha taslimu Sh. 400,000.
Alivitaja vitu vingine vilivyoibwa kuwa ni kitambulisho cha ubunge na simu mbili za mkononi ikiwemo moja inayofanyakazi kama kompyuta, vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 1.2.
“Kati ya simu hizo, moja ni ‘Iphone’ (simu ya kompyuta). Hiyo, niliinunua kwa Dola za Marekani 900. Ilikuwa na picha zangu nyingi,” alisema Mchungaji Msigwa.
Vitu vingine vilivyoibwa, alisema ni leseni ya udereva, kadi za benki na waraka wa huduma ya lipa umeme kadri unavyotumia (Luku).
Mchungaji Msigwa alisema alifika wilayani Sumbwanga siku hiyo saa 6:00 usiku na kukuta vyumba katika nyumba karibu zote za kulala wageni za mjini humo vikiwa vimejaa wageni.
Alisema kutokana na hali hiyo, muda huo alilazimika kwenda nje ya mji kutafuta vyumba katika nyumba nyingine za kulala wageni na kufanikiwa kupanga katika nyumba hiyo.
CHANZO: NIPASHE

Isije ikawa kamanda alikuwa amejizolea changu.Maana ma-Rev. nao noma.Hata hivyo pole kamanda, aluta continua.
 
Back
Top Bottom