The Informer
Senior Member
- Jun 14, 2010
- 119
- 29
Salaam kutoka Dodoma,
Nimeamua kuileta habari hii humu JF kwani vyombo vyote vya habari Tanzania viko mfukoni mwa Gullam Dewji, mwenyekiti wa Mohamed Enterprises, pamoja na mtoto wake, Mbunge Mohamed Dewji. Kwa masikitiko makubwa sana, najua nikiipeleka habari hii newsroom kwetu Mhariri Mtendaji wetu haiwezi kuitoa habari hii. Sijui na humu JF hii post haitaondolewa?
Nimeamua kuileta habari hii humu JF kwani vyombo vyote vya habari Tanzania viko mfukoni mwa Gullam Dewji, mwenyekiti wa Mohamed Enterprises, pamoja na mtoto wake, Mbunge Mohamed Dewji. Kwa masikitiko makubwa sana, najua nikiipeleka habari hii newsroom kwetu Mhariri Mtendaji wetu haiwezi kuitoa habari hii. Sijui na humu JF hii post haitaondolewa?
Mbunge ailipua Mohamed Enterprises Bungeni
Na MWANDISHI WETU
Dodoma
Mbunge wa Viti Maalumu kutoka Lindi, Riziki Lulida, amemtolea uvivu Mkurugenzi Mkuu wa Mohamed Enterprises, Mohamed 'Mo' Dewji, kwa kusema kuwa kampuni yake inachangia kuzorotesha uchumi wa Tanzania.
Riziki alisema kuwa kuna wafanyabiashara wakubwa, wengine wako humu ndani Bungeni, wananunua korosho, ufuta na mazao mengine kwa bei nafuuu kwa kuwalalia wakulima wa Tanzania na kuuza mazao hayo India.
Mohamed Enterprises ambayo inaongozwa na Mbunge wa Singida, Mohamed Dewji, ndiyo kampuni inayoongoza Tanzania kwa export ya ufuta, korosho, dengu na mazao mengine kutoka Tanzania kwenda India.
Riziki alisema kuwa wafanyabiashara kama hao wanaisababishia Tanzania ikose kutumia fursa ya AGOA ya kuuza mazao Marekani kwa bei nzuri zaidi kwa kuwadhulumu wakulima na kuuza mazao yao India kwa bei chee.
Alinukuu takwimu zilizosomwa Bungeni leo na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu, kuwa wakati Tanzania mpaka sasa imeuza $13m tu kwa AGOA, Kenya imeweza kuuza bidhaa za $200m mpaka sasa.
Riziki alitoa malalamiko hayo dhidi ya Mohamed Enterprises wakati akichangia hotuba ya makadirio ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.