nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Edward Kinabo
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema chama chake kitahakikisha kinalitumia Bunge lijalo la bajeti kuishinikiza serikali kupunguza kodi zinazotozwa kwenye bidhaa na huduma muhimu ili maisha ya wananchi yawe nafuu.
Mbowe alitoa msimamo huo jana wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Makambako katika mfululizo wa ziara ya maandamano na mikutano ya hadhara ya chama hicho inayoendelea kwenye mikoa ya nyanda za juu kusini.
Alisema ikiwa wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) watatumia wingi wao vibaya kupinga ajenda ya kupunguzwa kwa kodi, CHADEMA itarudi kwa wananchi kutumia nguvu ya umma mpaka kieleweke.
Alisema hali ngumu ya maisha inayowakabili Watanzania hivi sasa inasababishwa na kodi kubwa ya ongezeko la thamani (VAT) iliyowekwa katika bidhaa na huduma mbalimbali hivyo kufanya bei za mahitaji mbalimbali ya kimaisha kuwa juu.
Alisema CHADEMA haipingi serikali kutoza kodi lakini inapinga kodi kuwa kubwa katika bidhaa na huduma mbalimbali bila kujali uwezo wa mdogo wa kipato walio nao wananchi.
Watanzania wanataabika kwa sababu ya kodi zinazotozwa. Laiti Watanzania wangejua serikali inachukua kodi kiasi gani, laiti Watanzania wangejua. Tutapiga mzigo ndani na nje ya nchi mpaka kieleweke, tunakwenda kuwasha moto kwenye bunge la bajeti, alisema Mbowe.
Mbowe alitoa mfano wa bei ya sukari akisema katika kilo moja inayonunuliwa mwananchi hukatwa kodi ya sh 750.
Pia alitoa mfano wa soda ambazo alibainisha kuwa bei yake kiwandani haizidi sh 150 lakini kwa sababu ya kodi ya takriban sh 300 iliyowekwa, gharama za usafiri na faida ya muuzaji, soda moja huuzwa kwa sh 500 hadi 600.
Mfuko mmoja wa simenti unapoununua unakatwa kodi ya sh 8,000, ukinunua bia unakatwa kodi ya sh 750 kila kitu unachonunua ni kodi kodi kodi. Ukilipia umeme kodi..kama kodi hizi zingepunguzwa maisha yenu yangekuwa nafuu sana. Tutawasha moto katika Bunge la bajeti, wakiutumia vibaya wingi wao tutarudi kwa wananchi nchi nzima, tutatumia nguvu ya umma mpaka kieleweke, alisema Mbowe na kushangiliwa.
Alisema serikali ya CCM licha ya kukusanya kodi kubwa kwa mwezi ya sh bilioni 27 wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi, bilioni 295 wakati wa Rais Benjamin Mkapa na bilioni 430 kwa mwezi ya hivi sasa chini ya Rais Jakaya Kikwete, bado maisha ya Watanzania yamezidi kuwa magumu kwa sababu ya pesa hizo kuibwa na kutumiwa vibaya.
Alitoa mfano wa matumizi mabaya ya kodi ya wananchi yaliyowahi kufanywa na serikali kuwa ni kudai imenunua ndege ya Rais kwa takribani sh bilioni 40 wakati ndege hiyo ikiwa na thamani ya takribani sh bilioni 20.
Mifano mingine ya matumizi mabaya ya kodi ya wananchi aliyoitoa Mbowe katika mkoa huo, ni viongozi kutumia pesa nyingi kujilipa mishahara, posho na kugharamia matibabu yao nje ya nchi.
Katika mkutano huo Mbowe alipokea wanachama wapya kutoka kwenye vyama mbalimbali vya siasa akiwemo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Makambako, Edson Msigwa.
Msigwa alisema ameamua kuachana na CUF baada ya kuona chama hicho kinashirikiana na CCM kutumia vibaya raslimali za taifa. Nimeamua kuachana na CUF kwa sababu imefunga ndoa na CCM, sasa CHADEMA ndio chama pekee cha upinzani cha kutumainiwa katika kupigania haki na maslahi ya Watanzania, alisema Msigwa.
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema chama chake kitahakikisha kinalitumia Bunge lijalo la bajeti kuishinikiza serikali kupunguza kodi zinazotozwa kwenye bidhaa na huduma muhimu ili maisha ya wananchi yawe nafuu.
Mbowe alitoa msimamo huo jana wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Makambako katika mfululizo wa ziara ya maandamano na mikutano ya hadhara ya chama hicho inayoendelea kwenye mikoa ya nyanda za juu kusini.
Alisema ikiwa wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) watatumia wingi wao vibaya kupinga ajenda ya kupunguzwa kwa kodi, CHADEMA itarudi kwa wananchi kutumia nguvu ya umma mpaka kieleweke.
Alisema hali ngumu ya maisha inayowakabili Watanzania hivi sasa inasababishwa na kodi kubwa ya ongezeko la thamani (VAT) iliyowekwa katika bidhaa na huduma mbalimbali hivyo kufanya bei za mahitaji mbalimbali ya kimaisha kuwa juu.
Alisema CHADEMA haipingi serikali kutoza kodi lakini inapinga kodi kuwa kubwa katika bidhaa na huduma mbalimbali bila kujali uwezo wa mdogo wa kipato walio nao wananchi.
Watanzania wanataabika kwa sababu ya kodi zinazotozwa. Laiti Watanzania wangejua serikali inachukua kodi kiasi gani, laiti Watanzania wangejua. Tutapiga mzigo ndani na nje ya nchi mpaka kieleweke, tunakwenda kuwasha moto kwenye bunge la bajeti, alisema Mbowe.
Mbowe alitoa mfano wa bei ya sukari akisema katika kilo moja inayonunuliwa mwananchi hukatwa kodi ya sh 750.
Pia alitoa mfano wa soda ambazo alibainisha kuwa bei yake kiwandani haizidi sh 150 lakini kwa sababu ya kodi ya takriban sh 300 iliyowekwa, gharama za usafiri na faida ya muuzaji, soda moja huuzwa kwa sh 500 hadi 600.
Mfuko mmoja wa simenti unapoununua unakatwa kodi ya sh 8,000, ukinunua bia unakatwa kodi ya sh 750 kila kitu unachonunua ni kodi kodi kodi. Ukilipia umeme kodi..kama kodi hizi zingepunguzwa maisha yenu yangekuwa nafuu sana. Tutawasha moto katika Bunge la bajeti, wakiutumia vibaya wingi wao tutarudi kwa wananchi nchi nzima, tutatumia nguvu ya umma mpaka kieleweke, alisema Mbowe na kushangiliwa.
Alisema serikali ya CCM licha ya kukusanya kodi kubwa kwa mwezi ya sh bilioni 27 wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi, bilioni 295 wakati wa Rais Benjamin Mkapa na bilioni 430 kwa mwezi ya hivi sasa chini ya Rais Jakaya Kikwete, bado maisha ya Watanzania yamezidi kuwa magumu kwa sababu ya pesa hizo kuibwa na kutumiwa vibaya.
Alitoa mfano wa matumizi mabaya ya kodi ya wananchi yaliyowahi kufanywa na serikali kuwa ni kudai imenunua ndege ya Rais kwa takribani sh bilioni 40 wakati ndege hiyo ikiwa na thamani ya takribani sh bilioni 20.
Mifano mingine ya matumizi mabaya ya kodi ya wananchi aliyoitoa Mbowe katika mkoa huo, ni viongozi kutumia pesa nyingi kujilipa mishahara, posho na kugharamia matibabu yao nje ya nchi.
Katika mkutano huo Mbowe alipokea wanachama wapya kutoka kwenye vyama mbalimbali vya siasa akiwemo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Makambako, Edson Msigwa.
Msigwa alisema ameamua kuachana na CUF baada ya kuona chama hicho kinashirikiana na CCM kutumia vibaya raslimali za taifa. Nimeamua kuachana na CUF kwa sababu imefunga ndoa na CCM, sasa CHADEMA ndio chama pekee cha upinzani cha kutumainiwa katika kupigania haki na maslahi ya Watanzania, alisema Msigwa.