Serayamajimbo
Senior Member
- Apr 15, 2009
- 191
- 38
Mbowe: Rasimali za Watanzania zimeuzwa
na Asha Bani
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema umasikini wa Watanzania umetokana na viongozi wakuu wa nchi kuuza nchi na rasilimali zake kwa wageni kutoka nje ya nchi.
Mbowe alisema hayo jana katika Kijiji cha Moa wilayani hapa, wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mfululizo wa mikutano ya chama hicho maarufu kama Operesheni Sangara inayoendelea mkoani hapa.
Alisema, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejiuzia na kujilimbikizia rasilimali za nchi, huku zingine zikiuzwa kwa Wazungu wakati Watanzania walio wengi wakiendelea kuteseka kwa umaskini.
Nchi imeuzwa, nchi imekuwa maskini, CCM inawatenga Watanzania, inamilikisha rasilimali za taifa nje ya nchi pamoja na nyingine kujimilikisha wao wenyewe ili waweze kuitawala nchi kwa mabavu na nguvu za dola, ni lazima kuwe na mabadiliko ya dhati ili kila Mtanzania aweze kunufaika na rasilimali za taifa, alisema Mbowe. Aidha, alisema kutokana na hali hiyo kuna haja ya Watanzania kuwa kitu kimoja ili kuingoa CCM madarakani kwa kuwa wameiangamiza nchi na kuwafanya wananchi kama mtaji wao. Naye Mkurugenzi wa Vijana wa chama hicho, John Mnyika alisema serikali imewasahau wakazi wa wilaya hii kutokana na kushindwa hata kuwajengea hospitali na kuwaletea wauguzi wa kutosha, kuwa na maji safi na salama na hata shule.
na Asha Bani
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema umasikini wa Watanzania umetokana na viongozi wakuu wa nchi kuuza nchi na rasilimali zake kwa wageni kutoka nje ya nchi.
Mbowe alisema hayo jana katika Kijiji cha Moa wilayani hapa, wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mfululizo wa mikutano ya chama hicho maarufu kama Operesheni Sangara inayoendelea mkoani hapa.
Alisema, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejiuzia na kujilimbikizia rasilimali za nchi, huku zingine zikiuzwa kwa Wazungu wakati Watanzania walio wengi wakiendelea kuteseka kwa umaskini.
Nchi imeuzwa, nchi imekuwa maskini, CCM inawatenga Watanzania, inamilikisha rasilimali za taifa nje ya nchi pamoja na nyingine kujimilikisha wao wenyewe ili waweze kuitawala nchi kwa mabavu na nguvu za dola, ni lazima kuwe na mabadiliko ya dhati ili kila Mtanzania aweze kunufaika na rasilimali za taifa, alisema Mbowe. Aidha, alisema kutokana na hali hiyo kuna haja ya Watanzania kuwa kitu kimoja ili kuingoa CCM madarakani kwa kuwa wameiangamiza nchi na kuwafanya wananchi kama mtaji wao. Naye Mkurugenzi wa Vijana wa chama hicho, John Mnyika alisema serikali imewasahau wakazi wa wilaya hii kutokana na kushindwa hata kuwajengea hospitali na kuwaletea wauguzi wa kutosha, kuwa na maji safi na salama na hata shule.