nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*Hasa waropokaji na wapotoshaji wa sera za chama
Rai | Alhamisi, Septemba 27, 2012
IMEBAINIKA mambo si shwari kabisa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Hayaendi sanjari na juhudi za viongozi wa juu na kada za kati, kuacha kuzingatia misingi na sera za kukiwezesha kujenga muonekano na mwelekeo mzuri. Hususani kuepuka kuwa chanzo cha vurugu, badala ya kuhimiza shughuli za maendeleo ambayo ndiyo misingi mikuu ya kukiwezesha kupata ushawishi katika umma. Kuaminika kuwa kinaweza kuwa mbadala wa CCM.
Habari za kiuchunguzi zilizofanywa na gazeti la Rai, kwa kufanya mahojiano, tathmini na tafsiri za wataalamu wa masuala ya siasa, wengi wana maoni mchanganyiko juu ya CHADEMA. Wanakieleza kama chama cha siasa, ambacho kimekuwa katika harakati za kujijenga, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa, kwa kupitia kaulimbiu za operesheni sangara, vua gamba vaa gwanda, na M4C-Movement for Chage.
Miongoni mwa maoni ni ya kuutaka uongozi wa ngazi ya taifa hasa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwa kutumia busara zake, ndiye mtu pekee mwenye uwezo wa kuwafunga "Spidi Gavana" wanachama wa Chadema, wakiwemo wabunge, madiwani na viongozi wa ngazi mbalimabali. Ni kukifanya chama kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni zilizopo za uendeshaji wa shughuli za vyama vya siasa nchini.
Ni wazi kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ni mwenye kauli ya mwisho katika uendeshaji wa vikao kwa mujibu wa sera, taratibu na sheria ambazo kila mwanachama anapaswa kuzizingatia na kuzifuata. Hivyo Mwenyekiti, sambamba na Katibu Mkuu Dk. Willbod Slaa, ni nguzo muhimu juu ya kutoa uamuzi sahihi wenye maslahi ya chama, alibainisha mchambuzi ambaye ni mwanachama hai na mkereketwa na mdau mkuu ndani ya CHADEMA.
Katika kipindi chote tangu kuanza kwa zile zinazoitwa operesheni za kukijenga na kukiimarisha chama, kumekuwepo na matukio yasiyoonyesha mwelekeo mzuri katika mustakabali wa mfumo wa uendeshaji wa vyama vingi vya siasa nchini.
Hali ilivyo sasa nchini siyo shwari, hali imekuwa ikishuhudiwa kuibuka kwa tabia ya kupenda kuendekeza zaidi kufanya ghasia, kupambana na mamlaka za dola. Baadhi ya wanasiasa akiwamo kiongozi wa operesheni sangara, Benson Kagaila, wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha vijana, na wadau. Mara nyingi wadau wamejazwa hasira na kupandishwa jazba, kiasi cha kudiriki kukaidi amri na sheria na kusababisha kuingia katika mitafaruku na mikanganyiko katika jamii yenye utulivu.
Mwenendo huu unaweza kuchafua taswira, malengo na makusudio ya CHADEMA, chama ambacho kimekuwa kikivutia maelfu ya watu kushiriki katika kujiunga, na kukiimarisha kuanzia ngazi ya shina kwa kunadi sera zake katika jamii.
Tangu kumalizika kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, inaonekana wazi kuna watu wasioona mbele wakiwamo wabunge, madiwani na wadau mbalimbali kwa makusudi kuacha kuzingatia taratibu na sheria, hasa baada ya matokeo ya uchaguzi huo.
Yako mambo mengi ambayo yanaelezwa na wachambuzi na kutafsiriwa kwa mtazamo kuwa baadhi ya watu kwenye jamii wamebadilika mienendo yao. Kila kukicha wanadai nchi imeharibika, eti hakuna jema bali mambo yote ni mabaya (hasi) tu.
Yamkini wanasiasa na wadau wanapaswa kutuliza akili na mawazo yao. Waanze kupima mambo yote wanayofanya, watathmini na kuchambua kwa kina ni masuala gani yana mashiko na faida, katika taifa letu na jamii kwa ujumla.
Hali katika baadhi ya mikoa haitabiriki, siyo shwari, tafsiri hii inatokana na duru za uchunguzi na mahojiano na watu mbalimbali katika mikoa hiyo. Matukio yasiyo ya kawaida ya uvunjifu wa amani yameongezeka kuanzia majiji ikiwamo Arusha, Mwanza, Mbeya, na miji ya Morogoro na Iringa.
Uvumilivu na upendo umeanza kutoweka, imebainika zaidi ni miongoni mwa vijana, wadau na wakereketwa wa siasa. Wamekuwa watu wa jazba na hasira za kutisha. Wengi wao wanaonekana kupandisha mori kutokana na matamko ya wanasiasa, wakiwamo wabunge na madiwani.
Taswira sahihi juu ya matokea ya operesheni zote kuanzia sangara, vua gamba vaa gwanda, na vuguvugu na harakati za mabadiliko (M4C), yamkini zimechangia kuwepo mikanganyiko. Ni mwendelezo wa matukio ambayo yanabainisha kuongeza kwa uhasama kuliko uhusiano mwema.
Wataalamu, wanazuoni wa masuala ya siasa, wana mtazamo na tathmini endelevu, wanafafanua kuwa siasa ya vyama vya upinzani siyo ugomvi wala uhasama. Ni njia ya kupanua wigo wa demokrasia kwa kukosoa, kusahihisha na kurekebisha kasoro. Kutumia njia ya majadiliano kwa kujenga hoja zenye nguvu kwa ustaarabu. Kuvumiliana hata kama kuna kutofautiana kimawazo na kimtizamo juu ya masuala mbalimbali.
Mwenyekiti wa CHADEMA, ambaye pia ni kiongozi wa upinzani kitaifa, ndiye mwenye uwezo wa kuwafunga "Spidi gavana" wale wakorofi na wavurugaji wa sera sahihi za chadema.
Baba wa taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kukisifu na kukiunga mkono chama cha CHADEMA kwamba kina sera nzuri. Mwalimu hakukosea hata kidogo, lakini baada ya miaka 13 tangu ametutoka, CHADEMA kimeweka kando zile sera nzuri alizozisifia Mwalimu, sasa kimeamua kukumbatia na kuendesha chama kwa sera za wanaharakati.
Mwenyekiti na Katibu Mkuu CHADEMA, waongoze wadau kufanya kazi ya kunadi sera kwa njia ya amani na mshikamano wa kitaifa, badala ya kubomoa misingi ya utaifa tuliyoachiwa na Mwalimu Nyerere.
Rai | Alhamisi, Septemba 27, 2012
IMEBAINIKA mambo si shwari kabisa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Hayaendi sanjari na juhudi za viongozi wa juu na kada za kati, kuacha kuzingatia misingi na sera za kukiwezesha kujenga muonekano na mwelekeo mzuri. Hususani kuepuka kuwa chanzo cha vurugu, badala ya kuhimiza shughuli za maendeleo ambayo ndiyo misingi mikuu ya kukiwezesha kupata ushawishi katika umma. Kuaminika kuwa kinaweza kuwa mbadala wa CCM.
Habari za kiuchunguzi zilizofanywa na gazeti la Rai, kwa kufanya mahojiano, tathmini na tafsiri za wataalamu wa masuala ya siasa, wengi wana maoni mchanganyiko juu ya CHADEMA. Wanakieleza kama chama cha siasa, ambacho kimekuwa katika harakati za kujijenga, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa, kwa kupitia kaulimbiu za operesheni sangara, vua gamba vaa gwanda, na M4C-Movement for Chage.
Miongoni mwa maoni ni ya kuutaka uongozi wa ngazi ya taifa hasa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwa kutumia busara zake, ndiye mtu pekee mwenye uwezo wa kuwafunga "Spidi Gavana" wanachama wa Chadema, wakiwemo wabunge, madiwani na viongozi wa ngazi mbalimabali. Ni kukifanya chama kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni zilizopo za uendeshaji wa shughuli za vyama vya siasa nchini.
Ni wazi kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ni mwenye kauli ya mwisho katika uendeshaji wa vikao kwa mujibu wa sera, taratibu na sheria ambazo kila mwanachama anapaswa kuzizingatia na kuzifuata. Hivyo Mwenyekiti, sambamba na Katibu Mkuu Dk. Willbod Slaa, ni nguzo muhimu juu ya kutoa uamuzi sahihi wenye maslahi ya chama, alibainisha mchambuzi ambaye ni mwanachama hai na mkereketwa na mdau mkuu ndani ya CHADEMA.
Katika kipindi chote tangu kuanza kwa zile zinazoitwa operesheni za kukijenga na kukiimarisha chama, kumekuwepo na matukio yasiyoonyesha mwelekeo mzuri katika mustakabali wa mfumo wa uendeshaji wa vyama vingi vya siasa nchini.
Hali ilivyo sasa nchini siyo shwari, hali imekuwa ikishuhudiwa kuibuka kwa tabia ya kupenda kuendekeza zaidi kufanya ghasia, kupambana na mamlaka za dola. Baadhi ya wanasiasa akiwamo kiongozi wa operesheni sangara, Benson Kagaila, wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha vijana, na wadau. Mara nyingi wadau wamejazwa hasira na kupandishwa jazba, kiasi cha kudiriki kukaidi amri na sheria na kusababisha kuingia katika mitafaruku na mikanganyiko katika jamii yenye utulivu.
Mwenendo huu unaweza kuchafua taswira, malengo na makusudio ya CHADEMA, chama ambacho kimekuwa kikivutia maelfu ya watu kushiriki katika kujiunga, na kukiimarisha kuanzia ngazi ya shina kwa kunadi sera zake katika jamii.
Tangu kumalizika kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, inaonekana wazi kuna watu wasioona mbele wakiwamo wabunge, madiwani na wadau mbalimbali kwa makusudi kuacha kuzingatia taratibu na sheria, hasa baada ya matokeo ya uchaguzi huo.
Yako mambo mengi ambayo yanaelezwa na wachambuzi na kutafsiriwa kwa mtazamo kuwa baadhi ya watu kwenye jamii wamebadilika mienendo yao. Kila kukicha wanadai nchi imeharibika, eti hakuna jema bali mambo yote ni mabaya (hasi) tu.
Yamkini wanasiasa na wadau wanapaswa kutuliza akili na mawazo yao. Waanze kupima mambo yote wanayofanya, watathmini na kuchambua kwa kina ni masuala gani yana mashiko na faida, katika taifa letu na jamii kwa ujumla.
Hali katika baadhi ya mikoa haitabiriki, siyo shwari, tafsiri hii inatokana na duru za uchunguzi na mahojiano na watu mbalimbali katika mikoa hiyo. Matukio yasiyo ya kawaida ya uvunjifu wa amani yameongezeka kuanzia majiji ikiwamo Arusha, Mwanza, Mbeya, na miji ya Morogoro na Iringa.
Uvumilivu na upendo umeanza kutoweka, imebainika zaidi ni miongoni mwa vijana, wadau na wakereketwa wa siasa. Wamekuwa watu wa jazba na hasira za kutisha. Wengi wao wanaonekana kupandisha mori kutokana na matamko ya wanasiasa, wakiwamo wabunge na madiwani.
Taswira sahihi juu ya matokea ya operesheni zote kuanzia sangara, vua gamba vaa gwanda, na vuguvugu na harakati za mabadiliko (M4C), yamkini zimechangia kuwepo mikanganyiko. Ni mwendelezo wa matukio ambayo yanabainisha kuongeza kwa uhasama kuliko uhusiano mwema.
Wataalamu, wanazuoni wa masuala ya siasa, wana mtazamo na tathmini endelevu, wanafafanua kuwa siasa ya vyama vya upinzani siyo ugomvi wala uhasama. Ni njia ya kupanua wigo wa demokrasia kwa kukosoa, kusahihisha na kurekebisha kasoro. Kutumia njia ya majadiliano kwa kujenga hoja zenye nguvu kwa ustaarabu. Kuvumiliana hata kama kuna kutofautiana kimawazo na kimtizamo juu ya masuala mbalimbali.
Mwenyekiti wa CHADEMA, ambaye pia ni kiongozi wa upinzani kitaifa, ndiye mwenye uwezo wa kuwafunga "Spidi gavana" wale wakorofi na wavurugaji wa sera sahihi za chadema.
Baba wa taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kukisifu na kukiunga mkono chama cha CHADEMA kwamba kina sera nzuri. Mwalimu hakukosea hata kidogo, lakini baada ya miaka 13 tangu ametutoka, CHADEMA kimeweka kando zile sera nzuri alizozisifia Mwalimu, sasa kimeamua kukumbatia na kuendesha chama kwa sera za wanaharakati.
Mwenyekiti na Katibu Mkuu CHADEMA, waongoze wadau kufanya kazi ya kunadi sera kwa njia ya amani na mshikamano wa kitaifa, badala ya kubomoa misingi ya utaifa tuliyoachiwa na Mwalimu Nyerere.