Je Dr. Slaa kugombea urais TZ mwakani?
Kuna kila dalili kwamba CHADEMA wanamuandaa Dr. Slaa kugombea urais 2010. Mpambano huo utakuwa mzuri sana, huenda tukamkosa sana Dr. Slaa kwenye bunge la kuanzia 2010.
Jana CHADEMA walipokuwa Karatu waligusia kitu kama hicho kwamba wanatafuta mtu mwingine kugombea ubunge Karatu. Na sasa Mbowe kaamua kurudi Hai, basi mpambano mwakani nadhani utakuwa JK vs Dr. Slaa.
Naye Mbowe si angesema tu kwamba ameamua kugombea? Hii ya kwamba wananchi wamemuomba na propaganda tu za kisiasa.
Mbowe kugombea ubunge Hai 2010
na Grace Macha, Hai
WANANCHI wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, wamemuomba Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kugombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; naye amekubali.
Kutokana na Mbowe kukubali ombi hilo, ni wazi sasa atapambana na mbunge wa jimbo hilo hivi sasa, Fuya Kimbita (CCM), katika uchaguzi mkuu ujao.
Alisema amefikia hatua hiyo, baada ya kuombwa na wananchi wake ambao walisema wamekosa mwakilishi makini tangu alipoachia ubunge kwenye jimbo hilo mwaka 2005.
Wananchi hao ambao walikuwa wakipaza sauti wakati wote, hali iliyosababisha Mbowe akatishe hotuba zake mara kwa mara kwa ajili ya kuwasikiliza, walisema wakati akiwa mbunge alianzisha miradi mingi ikiwemo ya elimu , kijamii na kiuchumi ambayo kwa sasa imekufa.
Hata hivyo, Mbowe aliwasisitizia wananchi hao kuwa lazima wampe watu wa kufanya naye kazi ambao ni wenye viti wa vitongoji na vijiji kwani kinyume cha hapo atafanya kazi katika mazingira magumu.
Alisema katika kipindi cha miaka mitano alichowaongoza kuanzia 2000-2005, jambo kubwa lililokuwa likimsumbua ni vikwazo alivyokuwa anawekewa na viongozi wa vitongoji na vijiji ambao kwa wakati huo walikuwa wanatoka Chama Cha Mmapinduzi (CCM), ambao alikuwa akipanga nao shughuli lakini walikuwa wagumu kutekeleza.
Mbowe ambaye kabla ya kuwanadi wagombea wa Chadema, aliwauliza wananchi hao iwapo wagombea wake walikuwa na sifa na wananchi walisisitiza kuwa wote walikuwa wanafaa. Kwa upande wake, Mbowe aliwataka wananchi hao kuwapuuza wanaodai kuwa mahindi ya chakula cha msaada yanayotolewa ni mali ya CCM. Mbowe alifanya mikutano kwenye vijiji vya Kilanya , Narumu , Machame - Uroki , Kyuu - Masama Magharibi na Mbweera Mula - Masama Mashariki eneo analotokea mbunge wa jimbo hilo Fuya Kimbita (CCM).
Kuna kila dalili kwamba CHADEMA wanamuandaa Dr. Slaa kugombea urais 2010. Mpambano huo utakuwa mzuri sana, huenda tukamkosa sana Dr. Slaa kwenye bunge la kuanzia 2010.
Jana CHADEMA walipokuwa Karatu waligusia kitu kama hicho kwamba wanatafuta mtu mwingine kugombea ubunge Karatu. Na sasa Mbowe kaamua kurudi Hai, basi mpambano mwakani nadhani utakuwa JK vs Dr. Slaa.
Naye Mbowe si angesema tu kwamba ameamua kugombea? Hii ya kwamba wananchi wamemuomba na propaganda tu za kisiasa.
Mbowe kugombea ubunge Hai 2010
na Grace Macha, Hai
WANANCHI wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, wamemuomba Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kugombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; naye amekubali.
Kutokana na Mbowe kukubali ombi hilo, ni wazi sasa atapambana na mbunge wa jimbo hilo hivi sasa, Fuya Kimbita (CCM), katika uchaguzi mkuu ujao.
Alisema amefikia hatua hiyo, baada ya kuombwa na wananchi wake ambao walisema wamekosa mwakilishi makini tangu alipoachia ubunge kwenye jimbo hilo mwaka 2005.
Wananchi hao ambao walikuwa wakipaza sauti wakati wote, hali iliyosababisha Mbowe akatishe hotuba zake mara kwa mara kwa ajili ya kuwasikiliza, walisema wakati akiwa mbunge alianzisha miradi mingi ikiwemo ya elimu , kijamii na kiuchumi ambayo kwa sasa imekufa.
Hata hivyo, Mbowe aliwasisitizia wananchi hao kuwa lazima wampe watu wa kufanya naye kazi ambao ni wenye viti wa vitongoji na vijiji kwani kinyume cha hapo atafanya kazi katika mazingira magumu.
Alisema katika kipindi cha miaka mitano alichowaongoza kuanzia 2000-2005, jambo kubwa lililokuwa likimsumbua ni vikwazo alivyokuwa anawekewa na viongozi wa vitongoji na vijiji ambao kwa wakati huo walikuwa wanatoka Chama Cha Mmapinduzi (CCM), ambao alikuwa akipanga nao shughuli lakini walikuwa wagumu kutekeleza.
Mbowe ambaye kabla ya kuwanadi wagombea wa Chadema, aliwauliza wananchi hao iwapo wagombea wake walikuwa na sifa na wananchi walisisitiza kuwa wote walikuwa wanafaa. Kwa upande wake, Mbowe aliwataka wananchi hao kuwapuuza wanaodai kuwa mahindi ya chakula cha msaada yanayotolewa ni mali ya CCM. Mbowe alifanya mikutano kwenye vijiji vya Kilanya , Narumu , Machame - Uroki , Kyuu - Masama Magharibi na Mbweera Mula - Masama Mashariki eneo analotokea mbunge wa jimbo hilo Fuya Kimbita (CCM).