Mbowe: Kikwete ameelemewa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Mbowe: Kikwete ameelemewa

na Salehe Mohamed
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema Rais Jakaya Kikwete anahitaji msaada wa haraka kiuongozi kwa sababu ameelemewa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama hicho jana, Mbowe alisema kuwa mambo yanayotokea sasa hivi nchini ni dalili tosha kuwa uongozi wa Rais Kikwete umeelemewa na unahitaji kusaidiwa.

Alisema matukio yanayoiandama serikali ya Rais Kikwete kwa sasa ni ya kusikitisha kwa sababu yanaashiria kuwa nchi ipo hatarini kuelekea katika machafuko ya kijamii na kuanguka.

Alisema kwa kiasi kikubwa, hali hiyo inatokana na kile alichodai kuwa ni uongozi wa Rais Kikwete kushindwa kuongoza kwa matakwa ya wananchi na badala yake kutekwa na mafisadi.

Alisema taifa linahitaji mabadiliko ya haraka ya utawala, ili kudhibiti hali iliyoanza kujitokeza hivi sasa.

Akizungumza kwa sauti tulivu lakini yenye masikitiko na huruma, Mbowe alisema kupigwa mawe kwa msafara wa rais, kuzomewa kwa viongozi, migomo ya walimu, madaktari na kufungia ofisini kwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi na wastaafu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ni ishara ya nchi kuelekea katika machafuko ambayo mwisho wake ni kuanguka kwa taifa la Tanzania.

Alisema matukio yote hayo ya kusikitisha yametokana na uongozi wa Rais Kikwete kutekwa na mafisadi na kusahau kuwahudumia wananchi ambao hivi sasa wana maisha magumu na wamekata tamaa kiasi cha kuwa tayari kufanya jambo lolote baya.

“Uongozi wa Kikwete umeshindwa kuongoza, ndiyo maana wananchi wamekata tamaa na wanaanza kumrushia mawe na kuwazomea viongozi wake. Hali hii ni mbaya na kuna haja ya kufanya mabadiliko ya mfumo wa utawala,” alisema Mbowe.

Aidha, Mbowe alionyesha masikitiko yake kwa msafara wa Rais Kikwete kupigwa mawe huko Mbeya na kusema jambo kama hilo halikupaswa kutokea, lakini wananchi wamelazimishwa kufikia hali hiyo.

Kuhusu kulegalega kwa ushirikiano wa CHADEMA na vyama vya upinzani vilivyokuwa katika ushirikiano vya TLP, NCCR-Mageuzi na CUF, alisema wameamua kurudi nyuma kujipanga lakini hawajavunja ushirikiano huo.

Kwamba wamegundua baadhi ya washirika wa umoja huo wamekuwa wakitumika kuibomoa CHADEMA, hivyo wanapaswa wajipange upya na ikiwezekana kuchagua vyama watavyoshirikiana navyo.

“Kurudisha nyuma majeshi si kushindwa vita, bali ni kujipanga, hivyo na sisi tumefanya hivyo huku tukitafakari ushirikiano wetu ili uwe na tija, tumegundua kuwa washirika wetu wengine wanatumiwa na CCM kutubomoa,” alisema Mbowe.

Akizungumzia uchaguzi mdogo wa Tarime uliofanyika wiki iliyopita, alisema walichokifanya Wanatarime ni mfano wa kuigwa na kinaonyesha ukomavu wa demokrasia, kwani hawakujali vitisho vya dola, fedha zilizokuwa zikitolewa na CCM na maneno ya uzandiki yaliyokuwa yakitolewa na watu.

Alisema pamoja na kupigwa risasi, mapanga, mabomu ya machozi na maji ya kuwasha, Wanatarime waliamua kumchagua Charles Mwera (CHADEMA) kuwa mbunge wao, hali inayodhihirisha kuwa wananchi wakiamua jambo, wanaweza.

Aliongeza kuwa kulikuwa na njama za kuiba kura pamoja na kubadilisha matokeo, lakini wakazi wa Tarime walikuwa macho kuhakikisha hakuna hila inayofanyika na kumpata kiongozi waliyekuwa wakimtaka badala ya aliyekuwa akitakiwa na CCM.

Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema Watanzania wanapaswa kuamka, kwa vile maisha bora waliyoahidiwa na Rais Kikwete hayaonekani na kadiri siku zinavyokwenda ndivyo yanazidi kuwa magumu.

Alisema utawala uliopo hivi sasa haufuati sheria na kutoa mfano wa watuhumiwa wa ufisadi kupewa muda wa kurejesha kile walichokiiba na kuachiwa badala ya kufikishwa mahakamani kama wanavyofanywa wezi wa kuku au wengineo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe, alisema kama Watanzania wataliacha taifa mikononi mwa CCM, litaangamia na vizazi vijavyo vitakuja kulaumu kizazi kilichopo sasa kwa kutoungana na kufanya mapambano ya kudai uhuru kutoka kwa watawala wasiojali masilahi ya wananchi.

Na katika kile kinachoonyesha kuwa Kikwete amelemewa na majukumu, jana alilazimika kufuta baadhi ya shughuli zilizokuwa zimepangwa katika ziara yake mkoani Mbeya, kutokana na kubana kwa ratiba hiyo.

Ilidaiwa kuwa Kikwete alilazimika kuahirisha baadhi ya shughuli hizo kutokana na ratiba kubana, huku akisubiriwa Dar es Salaam kuongoza harambee iliyoandaliwa na Chama cha Maalbino nchini. Harambee hiyo ilipangwa kufanyika jana na kufuatiwa na maandamano leo.

Moja ya shughuli aliyoifuta ni mkutano wa hadhara wa majumuisho, uliokuwa umepangwa kufanyika katika Uwanja wa Sokoine, mjini Mbeya.

Ilitarajiwa kuwa katika uwanja huo, pamoja na kuelezea masuala mengine kadhaa, Rais Kikwete angepata fursa ya kujibu hoja za wafanyabiashara wa Soko la Mwanjelwa, ambao katika siku ya pili ya ziara yake, waliuzuia msafara wake kwa kulala barabarani.


Aliposimama, kundi kubwa la wafanyabiashara walianza kupiga makelele, na hivyo kusababisha kutoelewana baina yao na rais, jambo lililomfanya Rais Kikwete awatake waorodheshe matatizo yao na atayajibu kwenye mkutano wa hadhara wa jana, ambao ulifutwa dakika za mwisho.

Aidha, Rais Kikwete alishindwa kwenda kukabidhi hundi ya fedha za ujenzi wa soko hilo la Mwanjelwa, ambalo liliungua moto siku zilizopita, na badala yake shughuli hiyo aliifanya katika mkutano wa majumuisho wa ndani.


Akizungumza katika mkutano huo, Rais Kikwete aliwataka viongozi wa mkoa huo kufanya kazi kwa pamoja na kuacha kupigana vijembe na kuwekeana vikwazo.

Hizi inaelekea kuwa ni salamu nzito kwa viongozi wa mkoa huo, ambao wanasifika kwa uhasama miongoni mwao, kiasi cha kuhujumiana wao kwa wao.
 
Kikwete asitafute mchawi kwa matatizo ya Mbeya. Kwanza matatizo hayako Mbeya tu bali yako karibu Tanzania nzima.
Nina hakika maeneo mengi wana shida kweli. Ebu aende mahali kama Kigoma aone. Watampokea kwa mishumaa na viabatari na jerry cans zakuchotea maji.
Akienda kila mahali kuna shida na shida na ni yeye aliyeahidi maisha borakwa kila mtanzania wakati anajua wazi alikuwa anawadanganya.
Sasa anakuja na lugha zipi tena za kulaumu viongozi wenzie wakati wengi ni yeye amechora ramani ya kuwaweka katika madaraka kwa kuwa walimpigia kampeni?
Kwanza yeye aondoke kwa kutudanganya watanzania ingawa mimi binafsi sikushiriki kabisa kumpa kura yngu maana niligundua kuwa anatudanganya.
 
Is Tanzania facing leadership crisis?

2008-10-19 11:51:17
By Rodgers Luhwago

People had high hopes for better life under the CCM slogan of New Zeal, New Speed and New Vigour. People were filled with high dreams of improving their lives under the banner ``Better Life for Every Tanzanian.``

But, today it seems majority of people are losing hope. From mega corruption scandals to the current strikes facing the nation. Their hopes for better life have vanished in thin air.

Trade unions are now up in arms with the government. Worse still, some voters have gone further, opting to stone the president`s motorcade as a way of expressing their anger. What has gone wrong? Who is to blame?


Professor Mwesiga Baregu (pictured), a seasoned lecturer in political science at the University of Dar es Salaam granted an exclusive interview to The Guardian On Sunday this week in which he explored several reasons that have brought about this state of mistrust to the government.

According to him, the government started losing its credibility to the public right from the time when the nation plunged into a power crisis way back in early 2006, a few months after President Jakaya Kikwete entered State House.

He said it was during the same period when the public witnessed President Kikwete`s close friends playing a central role in appointing a briefcase firm - Richmond Development Company- to generate emergency power to alleviate the situation.

The seasoned lecturer rewinds his memory back, revisiting a political atmosphere that reigned a few months after the President took an oath of office in which he was subjected to serious public criticism for forming a big cabinet based on friendship.

He said both incidents (formation of the big, friendship-based friendship and Richmond saga) were the first issues that shed light on how the leadership of the country would be, raising doubt on the competency of the government in terms of job performance.

``Observation shows that people began losing hope right from the beginning when the President formed the cabinet on friendship basis. Things got even worse after some people believed to be his (President) close friends caused a huge loss to the nation by engaging a fake company to produce power,`` he says.

According to the lecturer, the theft of Sh 133bn/- from the Bank of Tanzania`s External Payment Arrears (EPA) account and the manner in which the president handles the matter has again fuelled people�s anger on the national leadership.

``People were expecting the President to take stern measures against all individuals involved in looting the cash from the public coffers but nothing tangible appears to be done. Do you expect people to be happy with all this?


You should take note that people are now associating their poverty with EPA looters thinking they are the ones making their lives hard, the Professor says.

He said the CCM government made a great mistake by giving too many promises during the 2005 general election while its ability to deliver was poor.

Young people who had high hopes of securing jobs are now languishing in abject poverty with no solution in sight.

The don said a wave of strikes by workers that now engulf the nation combined by the isolated incidents in Mbeya Region where some people stoned the president�s motorcade shows that people are now tired of empty promises and a hard life.

`` Basically, the President has failed to form a government that can fight for the welfare of the public and now what we are witnessing, can be described as a leadership crisis, he added.

According to him, leadership crisis also occurs when people lose confidence in their national leadership.

Qualifying his argument Prof Baregu said it has reached a point where people do not know what tomorrow will bring, adding that it has now been proved that leaders in the country are not sensitive to public sentiments.

He said the government should have come up with an affirmative action on Agriculture and Mining sectors. He said there is no doubt that the fourth phase has until now proved a failure. But, can the President turn the tide before the next general election a mere 24 months away?

SOURCE: Sunday Observer
 
Ni movement nzuri..Ila mimi sielewi situation on the ground.
Ninachofahamu ni kuwa ushirikiano ni lazima ili kuweza kupata ushindi.
Naelewa kuhusu baadhi ya wapinzani wengine kutumika na ccm..Ila tunaomba wawekwe wazi wale wanaofanya hivyo ili mambo yaanze sasa.
Inawezekana chadema wanataka kujaribu mara baada ya ushindi wa Tarime ili kuendeleza wimbi hilo la mageuzi...Tusubiri tuone direction...Movement nakubaliana nayo ila ni lazima tuwekewe wazi kuwa nani ni nani.
Mtikila tumeshamweka pembeni...Tunataka kusikia kuhusu wengine.
 
Kuna mengi JF ila muda hauruhusu kusoma yote. Asante Bubu ataka kusema kwa ku-highlight some parts on the articles.



.
 
Ni movement nzuri..Ila mimi sielewi situation on the ground.
Ninachofahamu ni kuwa ushirikiano ni lazima ili kuweza kupata ushindi.
Naelewa kuhusu baadhi ya wapinzani wengine kutumika na ccm..Ila tunaomba wawekwe wazi wale wanaofanya hivyo ili mambo yaanze sasa.
Inawezekana chadema wanataka kujaribu mara baada ya ushindi wa Tarime ili kuendeleza wimbi hilo la mageuzi...Tusubiri tuone direction...Movement nakubaliana nayo ila ni lazima tuwekewe wazi kuwa nani ni nani.
Mtikila tumeshamweka pembeni...Tunataka kusikia kuhusu wengine.

Mushi, acha utani ndugu yangu, kwani naamini uchaguzi wa Tarime umeweka wazi vyama pandikizi vya CCM kama ifuatavyo:
1) DP cha Mtikila
2) NCCR
3) kile chama cha Mzirai sijui sauti ya ... sorry sikikumbuki vyema
4) TLP sina uhakika sana kwani mwenyeketi wake naye haeleweki eleweki vyema

Katika vyote ambacho kinaonekana mafisadi hawakiingii ni CUF sema walisha kichafua katika chaguzi zilizo pita kwamba ni cha kidini..
Kwahiyo kwa maoni yangu kama CUF na CHADEMA vikungana, vinaweza leta mabadiliko makubwa!

Ila si bora ushirika kumbe wengine vibaraka na mapandikizi ya mafisadi kama alivo jisemea Mtikila live Tarime kwamba kazi yake na NCCR ni moja!
 
Anayosema Mh. Mbowe juu ya JK kulemewa (mimi naiita kushindwa kazi) ni kweli kabisaa. Wengine tulishayaona haya siku nyingi sana.

Unfortunately uongozi wa Mbowe ndani ya CHADEMA haujaonyesha uwezo wowote wa kuongoza nchi ili kuvutia watu wenye uwezo wa kukisogeza CHADEMA a step further ili waweze kuiondoa CCM. Huu ni wakati wa vyama vya upinzani, iwe CHADEMA, CUF n.k., kutumia udhaifu alionao JK na CCM kujipanua kisiasa. Je wanayaona hayo au nao wamezungukwa zaidi na maslahi binafsi kwanza?

Time is a good thing if used appropriately, but if not, it turns against you in a harsher and irrevessible way. Mwenye macho haambiwi tazama.
 
.... ingawa mimi binafsi sikushiriki kabisa kumpa kura yangu .........

Mkuu mchukia ufisadi,
Naomba mwongozo wako!
Unaposema hukushiriki kabisa kumpa kura yako ina maana hukupiga kura kabisa ama kura ulimpa mgombea mwingine wa urais?
Ufafanuzi please!

With thanks
 
Sidhani kama inahitaji mtu mwenye akili nyingi sana kuona dhahiri kabisa kwamba JK has proved failure!

Hebu naomba mniambie tangu aingie madarakani karibu miaka mitatu sasa, amefanya nini cha maana? Hata Mawaziri wake wanajifanyia shughuli zao binafsi tu kwa kuwa hakuna wa kuwauliza mambo yanakwendaje Wizarani, na wala hakuna malengo madhubuti ya kufikiwa waliyopewa! Kwa kifupi ni kwamba hakuna kinachoendelea. The county has come to a stand still!
 
........ wala hakuna malengo madhubuti ya kufikiwa waliyopewa!.........

Chukua tano mkubwa!
Shida kubwa kwa serikali zetu ni hiyo, kukosa vipaumbele na dira (malengo mahsusi).
Mpaka saa sijajua serikali yetu ina kipaumbele gani, kwamba waanze kutekeleza kipi ambacho ndicho hasa wananchi wanakereka nacho.
Huweza kuwa unatekeleza kila kitu, eti kwa sababu tu kipo katika ilani, "This is complete madness". Si kila kitu kilichomo katika ilani inaweza kutekelezeka.

We need priorities! Period!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom