Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Wasalaam,
Baada ya kelele nyingi za ushirikiano wa vyama vya upinzani vya siasa nimeona ni bora niwalete tena mbele yenu Wenyeviti wa Vyama vya Upinzani vyenye Wabunge ili tuweze kujiridhisha tena kuhusu ushirikiano wa vyama hivyo.
Nafahamu fika kwamba vyama ni zaidi ya watu lakini pia mawazo ya watu na fikra zao zinaathiri au zinasaidia kwa kiasi kikubwa muonekano wa chama husika.
Hawa wenyeviti kila mmoja ana lake zuri na baya; nitatoa mifano michache kwa kila mwenyekiti kwa zuri na baya lake;
Freeman Mbowe:
Baya: Inasemekana hana elimu ya kutosha (elimu ya chuo kikuu ndiyo inayozungumziwa hapa). anadaiwa kuihujumu NSSF kwa kutokulipa deni la kutengenezewa.
Zuri: ni kiongozi ambaye ameweza kuivusha chadema kutoka kipindi kimoja hadi kingine kwa kushawishi vijana kushiriki katika uongozi na siasa za nchi. Ameweza kurudi bungeni kwa mara nyingine baada ya kumshinda mgombea wa CCM.
Ibrahimu Lipumba:
Baya: Ni mwenyekiti aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi ya wenyeviti wenzake wa vyama vyenye wabunge bungeni na ni mtanzania pekee aliyegombea mara nyingi nafasi ya uraisi na kushindwa. Ni mgombea pekee ambaye hajafanikiwa kufikisha idadi ya kura Milioni 2 kwa chaguzi zote alizoshiriki.
Zuri: Ni profesa wa kwanza kugombea uraisi na profesa pekee aliyemshinda kwa kishindo profesa mwenzake kwenye uchaguzi wa mwenyekiti wa chama chake. Ni mwenyekiti mwenye mafanikio makubwa kuweza kuunganisha chama chake na chama cha mapinduzi kwa maslahi ya wazanzibari na kuacha maslahi ya bara pembeni mpaka kipindi kijacho.
James Mbatia:
Baya: ni mwenyekiti pekee ambaye kwa muda mrefu amekuwa na kashfa ya kuwa hayuko sawa kimaumbile (haijathibitishwa). Ni mwenyekiti pekee ambaye alishindwa vibaya kwenye kugombea ubunge kupitia jimboni. Ni mwenyekiti wa kwanza wa chama cha siasa kushindwa kwenye uchaguzi na kijana. Ni mwenyekiti wa kwanza wa chama cha siasa kushindwa uchaguzi na mwanamke.
Zuri: Ni mwenyekiti pekee aliyeweza kushinda viti vingi vya wabunge mkoa wa kigoma pekee. Ameweza kujenga chama ambacho wanaokimbia CDM wanafikia kabla ya kurudi CCM.
Augustine Lyatonga:
Baya: ni mwenyekiti mzee kuliko wote. Amekuwa haeleweki kuhusu msimamo wake. Alitangaza hadharani kwamba anamkubali Kikwete na Chama chake kikasimamisha mgombea uraisi. Hakumpigia kampeni mgombea uraisi wake. Mwenyekiti pekee aliyewahi kucheza jukwaani kumsifia Kikwete na CCM.
Zuri: ameweza kurudi bungeni baada ya muda mrefu nje. amefanikikwa kuwapa tumaini jipya wananchi wake wa Vunjo. Ni mshauri mzuri sana kuhusu hujuma na wizi wa CCM.
John Cheyo:
Baya: hajulikani kwa zuri lolote zaidi ya kwamba ni bwana mapesa. hachimbi visima kama Sabodo ingawaje watanzania wanaamini kwamba anapesa nyingi. ni mwenyekiti pekee aliyeamua kutumia chama kama taasisi ya kuendelea kupata ubunge. Kuna mikoa zaidi ya 10 ya tanzania hajawahi kufika tangu awe mwenyekiti kufanya siasa.
Zuri: hajulikani anasimamia siasa za aina gani. ni msemaji mzuri kupinga baadhi ya masuala bungeni ambayo hana maslahi nayo.
Ndugu WanaJF, baada ya hayo machache na yale mengi ambay wote mnayajua ni vizuri tukajiuliza hawa tunataka au tunategemea watuunganishe vipi?
Huko Bungeni tunataka washirkiane vipi. Watatu kati yao wako bungeni wengine hawapo, je ni ushirikiano gani ulikuwa unahitajika?
Nadhani kwa kupata mawazo ya wachangiaji tutapata angalau mwanga kuhusu wale wanaoongoza vyama vya upinzani tunavyovitaka vishirikiane!!:sad:
Baada ya kelele nyingi za ushirikiano wa vyama vya upinzani vya siasa nimeona ni bora niwalete tena mbele yenu Wenyeviti wa Vyama vya Upinzani vyenye Wabunge ili tuweze kujiridhisha tena kuhusu ushirikiano wa vyama hivyo.
Nafahamu fika kwamba vyama ni zaidi ya watu lakini pia mawazo ya watu na fikra zao zinaathiri au zinasaidia kwa kiasi kikubwa muonekano wa chama husika.
Hawa wenyeviti kila mmoja ana lake zuri na baya; nitatoa mifano michache kwa kila mwenyekiti kwa zuri na baya lake;
Freeman Mbowe:
Baya: Inasemekana hana elimu ya kutosha (elimu ya chuo kikuu ndiyo inayozungumziwa hapa). anadaiwa kuihujumu NSSF kwa kutokulipa deni la kutengenezewa.
Zuri: ni kiongozi ambaye ameweza kuivusha chadema kutoka kipindi kimoja hadi kingine kwa kushawishi vijana kushiriki katika uongozi na siasa za nchi. Ameweza kurudi bungeni kwa mara nyingine baada ya kumshinda mgombea wa CCM.
Ibrahimu Lipumba:
Baya: Ni mwenyekiti aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi ya wenyeviti wenzake wa vyama vyenye wabunge bungeni na ni mtanzania pekee aliyegombea mara nyingi nafasi ya uraisi na kushindwa. Ni mgombea pekee ambaye hajafanikiwa kufikisha idadi ya kura Milioni 2 kwa chaguzi zote alizoshiriki.
Zuri: Ni profesa wa kwanza kugombea uraisi na profesa pekee aliyemshinda kwa kishindo profesa mwenzake kwenye uchaguzi wa mwenyekiti wa chama chake. Ni mwenyekiti mwenye mafanikio makubwa kuweza kuunganisha chama chake na chama cha mapinduzi kwa maslahi ya wazanzibari na kuacha maslahi ya bara pembeni mpaka kipindi kijacho.
James Mbatia:
Baya: ni mwenyekiti pekee ambaye kwa muda mrefu amekuwa na kashfa ya kuwa hayuko sawa kimaumbile (haijathibitishwa). Ni mwenyekiti pekee ambaye alishindwa vibaya kwenye kugombea ubunge kupitia jimboni. Ni mwenyekiti wa kwanza wa chama cha siasa kushindwa kwenye uchaguzi na kijana. Ni mwenyekiti wa kwanza wa chama cha siasa kushindwa uchaguzi na mwanamke.
Zuri: Ni mwenyekiti pekee aliyeweza kushinda viti vingi vya wabunge mkoa wa kigoma pekee. Ameweza kujenga chama ambacho wanaokimbia CDM wanafikia kabla ya kurudi CCM.
Augustine Lyatonga:
Baya: ni mwenyekiti mzee kuliko wote. Amekuwa haeleweki kuhusu msimamo wake. Alitangaza hadharani kwamba anamkubali Kikwete na Chama chake kikasimamisha mgombea uraisi. Hakumpigia kampeni mgombea uraisi wake. Mwenyekiti pekee aliyewahi kucheza jukwaani kumsifia Kikwete na CCM.
Zuri: ameweza kurudi bungeni baada ya muda mrefu nje. amefanikikwa kuwapa tumaini jipya wananchi wake wa Vunjo. Ni mshauri mzuri sana kuhusu hujuma na wizi wa CCM.
John Cheyo:
Baya: hajulikani kwa zuri lolote zaidi ya kwamba ni bwana mapesa. hachimbi visima kama Sabodo ingawaje watanzania wanaamini kwamba anapesa nyingi. ni mwenyekiti pekee aliyeamua kutumia chama kama taasisi ya kuendelea kupata ubunge. Kuna mikoa zaidi ya 10 ya tanzania hajawahi kufika tangu awe mwenyekiti kufanya siasa.
Zuri: hajulikani anasimamia siasa za aina gani. ni msemaji mzuri kupinga baadhi ya masuala bungeni ambayo hana maslahi nayo.
Ndugu WanaJF, baada ya hayo machache na yale mengi ambay wote mnayajua ni vizuri tukajiuliza hawa tunataka au tunategemea watuunganishe vipi?
Huko Bungeni tunataka washirkiane vipi. Watatu kati yao wako bungeni wengine hawapo, je ni ushirikiano gani ulikuwa unahitajika?
Nadhani kwa kupata mawazo ya wachangiaji tutapata angalau mwanga kuhusu wale wanaoongoza vyama vya upinzani tunavyovitaka vishirikiane!!:sad: