Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,295
- 33,079
MWENYEKITI Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, amepandishwa kizimbani katika Mahakamani ya Hakimu Mkazi Arusha kwa kosa la kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria na kukaidi amri ya jeshi la polisi
Mbowe ameunganishwa na wenzake waliopandishwa kizimbani juzi Dk. Slaa na Lissu ambapo imetimia idadi ya washitakiwa 28 katika kesi hiyo
Watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kufanya kusanyiko isivyo halali katika viwanja vya NMC, eneo la Unga Ltd, Arusha Novemba 7 mwaka huu .
Mbowe alipandishwa kizimbani jana katika mahakama hiyo mara baada ya kujisalimisha polisi kwa kutakiwa kufanya hivyo na jeshi hilo kwa kuwa siku ya tukio hakupatikana
Alisomewa mashtiaka hayo mawili mbele ya Hakimu Devotha Kamuzora na kukana mashitaka hayo na kuwa nje kwa dhamana kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho na barua ya utambulisho kutoka kwa Ofisa Mtendaji wa Kata wanakotoka kutia saini hati ya dhamana ya Shilingi milioni tano kila mmoja.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 22, mwaka huu itakapotajwa
Chanzo: Mbowe aunganishwa kesi ya Slaa, Lissu
Mbowe ameunganishwa na wenzake waliopandishwa kizimbani juzi Dk. Slaa na Lissu ambapo imetimia idadi ya washitakiwa 28 katika kesi hiyo
Watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kufanya kusanyiko isivyo halali katika viwanja vya NMC, eneo la Unga Ltd, Arusha Novemba 7 mwaka huu .
Mbowe alipandishwa kizimbani jana katika mahakama hiyo mara baada ya kujisalimisha polisi kwa kutakiwa kufanya hivyo na jeshi hilo kwa kuwa siku ya tukio hakupatikana
Alisomewa mashtiaka hayo mawili mbele ya Hakimu Devotha Kamuzora na kukana mashitaka hayo na kuwa nje kwa dhamana kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho na barua ya utambulisho kutoka kwa Ofisa Mtendaji wa Kata wanakotoka kutia saini hati ya dhamana ya Shilingi milioni tano kila mmoja.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 22, mwaka huu itakapotajwa
Chanzo: Mbowe aunganishwa kesi ya Slaa, Lissu